Thursday, February 20, 2020

SOMO: BALAA LA DHAMBI (Samson Mollel 0767/0713 – 664 338)


UTANGULIZI

Tafsiri rahisi ya dhambi ni uasi/kuhalifu maagizo/sheria za Mungu, unapokuwa nje ya maelekezo ya Mungu wewe unatenda dhambi sawa na neno la Mungu 1Yohana 3:4 “Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi.”
Neno la Mungu linaenda mbele zaidi kwamba kama unajua/unafahamu kutenda mambo mema na ukaacha kuyatenda hayo mema kwako hilo ni dhambi (kumbuka hapa haujakosea kwenye amri za Mungu); Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi.”

Dhambi ikimpata mtekelezaji wake (mtenda dhambi) basi inazaa mauti. Neno la Mungu linatufundisha kwamba uchungu wa mauti ni dhambi 1Kor 15:56 “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati.”, katika tafsiri ya kiingereza “The sting of death is sin” yaani sumu inayoletelezea au inayopelekea mauti ni dhambi, ni sawa na kusema matokeo ya dhambi ni mauti. Mtu wa Mungu hata dhambi irembwe kiasi gani au iwe tamu na nzuri kiasi gani matokeo yake ni mauti kuanzia rohoni hadi mwilini. (Rumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.”)

ASILI YA DHAMBI

        i.            Dhambi ni danganyifu
Waebrania 3:13 Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
Mtu wa Mungu napenda ufahamu kwamba kila dhambi unayoiona lazima ikujie kwa jinsi ya udanganyifu pasipo kuonesha matokea yake halisi au pasipo kujionesha yenyewe. Pale bustani ya Edeni Mwanamke alipotokewa na nyoka na kudanywa na baadae Adamu hawakuwa na taarifa sahihi ya tukio walilokuwa wanalifanya (uasi), shetani alifahamu lakini aliwandanya kwa maneno ya kuwavutia na kuwaonesha kwamba watapanda cheo na kufanana na Mungu kama tunavyosoma katika Mwanzo 3:4-5 “4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, 5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.” shetani anawaeleza habari za kuwa sawa na Mungu lakini hawaambii kwamba watakufa, na baada ya kula tunda dhambi ikaingia duniani na hatimaye mauti ikatuvaa wakati huo.

     ii.            Dhambi inatoa furaha ya muda tu
Waebrania 11:25 “akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo;”
Jambo lingine la muhimu sana la kufahamu ni kwamba dhambi hutoa furaha au starehe ya muda mfupi na mateso ya milele hufuata baadae. Dhambi inatokana na mambo ya mwili na baada ya mwili kuipoteza roho kwa starehe za muda mfupi roho inapokea adhabu ya milele
Luka 16:19-23 “19 Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa. 20 Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi, ……….. 22 Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. 23 Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.”
Tajiri alipata raha ya muda mfupi tu akiwa duniani lakini mateso ya milele

   iii.            Dhambi ni uharibifu/inaangamiza
Mithali 11:3 “Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza Bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.” Yakobo 1:15 “Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.”
Matokeo ya mwisho ya dhambi ni mauti, pasipo kujali aina ya dhambi na namna ya udanganyifu wake lazima mwisho wa dhambi iwe ni uharibifu na maangamizo yaani mauti.

MAMBO AMBAYO DHAMBI INAWEZA KUYAFANYA

1.     Dhambi inakutenganisha na Mungu
Kitu kikubwa kabisa na cha kwanza ambacho dhambi hufanya kwenye maisha ya mwanadamu ni kumtenganisha na Mungu na baada ya kumtenganisha na Mungu, shetani anapata nafasi ya kumtesa mwanadamu.
Dhambi inapokutenganisha na Mungu inasababisha hasira ya Mungu kuwaka juu yako na shetani anafurahia kwani ndiomwanya wake wa kuingiza uharibifu wake katika misha yako
Isaya 59:1-2 “1 Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; 2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.”

2.     Dhambi inaleta aibu
Mwanzo 3:10 “Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha.”
Mithali 28:13 “Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.”
2Thesalonike 2:7 “Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.”

3.     Dhambi huleta uharibifu
Mithali 11:3 “Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza Bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.”

4.     Dhambi huleta udhaifu (Magonjwa/kufungwa na ibilisi)
Mithali 14:30 “Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili; Bali husuda ni ubovu wa mifupa.”
Yesu alimwambia Yule mgonjwa amesamehewa dhambi na akapona Mathayo 9:2-7 “2 Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako. 3 Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru. 4 Naye Yesu, hali akijua mawazo yao, akasema, Mbona mnawaza maovu mioyoni mwenu? 5 Kwa maana rahisi ni lipi, ni kusema, Umesamehewa dhambi zako, au ni kusema, Ondoka, uende? 6 Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (amwambia yule mwenye kupooza) Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako. 7 Akaondoka, akaenda zake nyumbani kwake.”

Magonjwa mengi (au yote) ni laana
Kumb 28 :15-68 “15 Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata….. 21 Bwana atakuambatanisha na tauni, hata atakapokwisha kukuondoa katika nchi uingiayo kwa kuimiliki. 22 Bwana atakupiga kwa kifua kikuu, na kwa homa, na kwa kuwashwa, na kwa hari ya moto, na kwa upanga, na kwa ukaufu, na kwa koga; navyo vitakufukuza hata uangamie….. 27 Bwana atakupiga kwa majipu ya Misri, na kwa bawasiri, na kwa pele, na kwa kujikuna, ambayo hupati kupoa…..35 Bwana atakupiga magoti na miguu kwa jipu lililo zito, usilopata kupozwa, tokea wayo wa mguu mpaka utosi wa kichwa……59 ndipo atakapofanya Bwana mapigo yako yawe ya ajabu, na mapigo ya uzao wako, mapigo makubwa kwa kweli, ya kudumu sana, na magonjwa mazito ya kudumu sana. 60 Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe. 61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa.”

5.     Dhambi huondoa amani
2Nyakati 15:3-6 “3 Basi tangu siku nyingi Israeli wamekuwa hawana Mungu wa kweli, wala hawana kuhani afundishaye, wala hawana torati; 4 lakini walipomgeukia Bwana, Mungu wa Israeli, katika msiba wao, na kumtafuta, akaonekana kwao. 5 Hata na zamani zile hakukuwa na amani kwake atokaye, wala kwake aingiaye, ila fadhaa kubwa juu yao wote wakaao katika nchi. 6 Wakavunjika-vunjika, taifa juu ya taifa, na mji juu ya mji; kwani Mungu aliwafadhaisha kwa shida zote.”
Unapokosa amani unabaki na bumbuwazi la moyo na ufahamu Kumb 28:28 “Bwana atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu, na kwa bumbuazi la moyoni;”
Amani hupatikana kwa kumlingana Mungu Ayubu 22: 21-23 “21 Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia. 22 Uyapokee, tafadhali, mafunzo yatokayo kinywani mwake, Na maneno yake yaweke moyoni mwako. 23 Ukimrudia Mwenyezi, utajengwa; Ukiuondoa udhalimu mbali na hema yako.”

DHAMBI ZENYE NGUVU ZINAZOANGAMIZA KANISA (WAKRISTO)
1.     ZINAA (UZINZI/UASHERATI)
Hakuna dhambi kwenye biblia iliyoleta maangamizo makuu kama zinaa (uzinzi na uasherati). Katika historia ya wana wa Israeli kama tunavyoisoma katika agano la kale hakuna mahali popote walifanya dhambi na dhambi hiyo ikasababisha mauaji makubwa kama dhambi ya uzinzi na uasherati wa kiroho na kimwili waliofanya wana wa Israeli na kumkasirisha Mungu kama tunavyosoma katika
1Kor 10:8 “Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu.”
Hesabu 25:1-8 “1 Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu; 2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao. 3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli. 4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli. 5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baal-peori. ……….. 9 Nao waliokufa kwa hilo pigo walikuwa watu elfu ishirini na nne hesabu yao.”

a.      Uzinzi/uasherati wa kiroho (ushirikina na uchawi)
Katika ulimwengu wa roho Mungu Jehova ni mume kwa wote wanaomwabudu na sisi tunao mwabudu ni kama wake kwake kama tunavyosoma katika maandiko
Yeremia 31:31-32 “31 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda. 32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.”

Kwa maana hiyo Yesu ni mume kwa kanisa kama tunavyosma katika Neno la Mungu
Waefeso 5:23 “Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.”
Mathayo 25:1-2 “1 Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi. 2 Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.”
Mtu yoyote anayefanya ibada za miungu mingine kama vile matambiko na kuwaendea waganga wa kienyeji na wasoma nyota na watu wa namna hiyo unakuwa umefanya zinaa kwa jinsi ya roho yaani umefanya uzinzi na uasherati na hasira ya Mungu inawaka juu yako kwa wivu mkubwa

b.     Uzinzi/uasherati wa kimwili
Katika amri kumi za Mungu tunaonywa kwamba uzinzi ni dhambi kama tunavyosoma katika kitabu cha Kutoka 20:14 “Usizini.” Vilevile tunasoma katika Waefeso 5:3 “Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;”
Mungu anazidi kutuonya kwa habari ya uzinzi na uasherati katika kitabu cha Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,”
Kumbe hapa Mungu anaonya juu ya uzinzi/uasherati wa kimwili au uanaofanyika katika miili hii tuliyonayo ndio maana mtume Paulo anaita kuwa ni matendo ya mwili.
Mtu wa Mungu anataka ujue kuwa mwili wa mtu sio mali ya mtu mwenye huo mwili bali ni mali ya Mungu sawa na Neno la Mungu “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;”. Kuna hatari kubwa katika kutumia mwili uliopewa na Mungu kwaajili ya uzinzi na uasherati kwani jambo hilo linamkasirisha sana Mungu na kuna hatari kubwa mbele yako kwa kufanya uzinzi/uasherati

1Kor 6:16-20 “16 Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja. 17 Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye. 18 Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe. 19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; 20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.”
Sasa nataka ufahamu kwamba asili ya dhambi ni uharibifu, mtu yeyote anayefanya uasherati na uzinzi anauharibu mwili wake na Mungu hawezi kukubali ukaliharibu hekalu lake au ukalichafua hekalu lake lazima akuharibu na wewe sawasawa na Neno lake

1Kor 3:17 “16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.”
Mungu anataka alitumie hekalu lake yaani wewe kwaajili ya kuipeleka injili mbele lakini wewe umeenda kuliharibu hekalu lake kwa ulevi, uzinzi na uasherati, uwe na uhakika kwamba Mungu atakuharibu kwani Neno la Mungu ni kweli na hakika

2.     KUTOKUMUAMINI MUNGU (HOFU/WOGA)

Yohana 16:7-9“7 Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu. 8 Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu. 9 Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi;”

Kama ulishawahi kufahamu kuwa kuna dhambi ambazo mtu akitenda hawezi kuurithi Ufalme wa Mungu, basi moja ya hizo dhambi ni hofu au woga. Biblia imeweka bayana kuwa waoga (wenye hofu) wote hawataurithi uzima wa milele Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.”

Unaweza kujiuliza kuwa inawezekanaje woga/hofu ikakupeleka kuzimu? Jibu ni rahisi sana, ni kwasababu hofu ni roho kutoka kwa shetani na ujasiri/nguvu ni Roho kutoka kwa Mungu, hivyo mwenye hofu ameingiwa na roho kutoka kwa ibilisi kama yanenavyo maandiko 2Tim 1:7 “Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.”

Kwa wale wasomaji wa Biblia mtafahamu kuwa katika agano la kale vitabu vitano vya Musa sehemu kubwa inazungumzia matendo makuu ya Mungu aliyowatendea wana wa Israeli kwa kuwatoa katika utumwa waliokaa kwa zaidi ya miaka mia nne, vilevile BWANA  aliwashindia dhidi ya adui waliokutana nao katika safari yao. Kwa ujumla ni kwamba wana wa Israeli walitembea kwa ushindi mkuu katika safari yao.

Lakini walipoikaribia ile nchi ya ahadi, wakawatuma wapelelezi na baadhi ya wale wapelelezi wakaleta habari mbaya ya ile nchi ni ya majtu na kwamba hawawezi kuingia katika nchi ile kwani wale watu wa nchi ile wana nguvu zaidi yao. Kama tunavyosoma katika kitabu cha Hesabu 13:31-33 “31 Bali wale watu waliopanda pamoja naye wakasema, Hatuwezi kupanda tupigane na watu hawa; kwa maana wana nguvu kuliko sisi. 32 Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno. 33 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.”

Joshua na Kalebu wakakanusha habari zile mbaya kwa imani na kusema kuwa wataingia katika nchi ya Kaanani kwa nguvu za Mungu na watawashinda adui zao kwani BWANA yupo upande wao; Hata hivyo wana wa Israeli wakachagua habari zenye hofu na kuacha habari za imani ya kushinda kama walivyosema Joshua na Kalebu kiasi cha kutaka kuwaua Joshua na Kalebu kama tunavyosoma katika Hesabu 14:6-10 “6 Na Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwao walioipeleleza nchi, wakararua nguo zao; 7 wakanena na mkutano wote wa wana wa Israeli wakasema, Nchi ile tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi njema mno ya ajabu. 8 Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali. 9 Lakini msimwasi Bwana, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye Bwana yu pamoja nasi; msiwaogope. 10 Lakini mkutano wote wakaamuru wapigwe kwa mawe. Ndipo utukufu wa Bwana ukaonekana katika hema ya kukutania, mbele ya wana wa Israeli wote.”
Kwasababu  ya wana wa Isareli kushindwa kumwamini Mungu hasira ya Mungu ikawaka juu yao na wakapewa adhabu kubwa ya kutoingia katika nchi ya ahadi kama ilivyoandikwa katika 
Hesabu 14:11, 22-24 “11 Bwana akamwuliza Musa, Je! Watu hawa watanidharau hata lini? Wasiniamini hata lini? Nijapokuwa nimefanya ishara hizo zote kati yao….. 22 kwa sababu watu hawa wote, ambao wameuona utukufu wangu na ishara zangu, nilizozitenda huko Misri, na huko jangwani, pamoja na haya wamenijaribu mara hizi kumi, wala hawakuisikiza sauti yangu; 23 hakika yangu hawataiona hiyo nchi niliyowaapia baba zao, wala katika hao wote walionidharau hapana atakayeiona; 24 lakini mtumishi wangu Kalebu, kwa kuwa alikuwa na roho nyingine ndani yake, naye ameniandama kwa moyo wote, nitamleta yeye mpaka nchi hiyo aliyoingia; na uzao wake wataimiliki.”

Mungu anasema “…..Je! Watu hawa watanidharau hata lini? Wasiniamini hata lini?..... kumbe kudharau kunatokana na kushindwa kuamini, kwahiyo unaposhindwa kumuamini Mungu tayari unakuwa umemdharau na hasira ya Mungu inawaka juu yako.
Lakini tuanaona Mungu anasema kuwa  mtumishi wake Kalebu amekuwa na roho nyingine ndani yake, maana yake ile roho ya hofu na woga iliwavaa Israeli haikumvaa Kalebu na Yoshua


3.     TAMAA YA FEDHA/MALI
Neno la Mungu linatufundisha kwamba kupenda fedha na mali ni mzizi wa uovu wa kila namna; ukiwa unapenda fedha kuliko kumpenda Mungu, yaani wewe bora uache ibada lakini uende kwenye biashara au kazi yako, kama ukiona umeweka pesa mbele kuliko kumtumikia Mungu yaani ili kutoa huduma lazima upewe fedha basi ufahamu kwamba fedha na mali zimekuwa Mungu wako.

1Timotheo 6:10-11 “10 Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi. 11 Bali wewe, mtu wa Mungu, uyakimbie mambo hayo; ukafuate haki, utauwa, imani, upendo, saburi, upole.”
Uchu wa fedha umepelekea watu wengi hata wakristo kumtenda Mungu dhambi kwani wengine wamewatoa watoto wao au ndugu zao kafara ili wapate fedha na mali. Eneo hili limeharibu utakatifu kwa sehemu kubwa kwani hata watumishi wa Mungu wamebadilishwa na kuwa kama waganga wa kienyeji kwaajili ya kupenda fedha kama ilivyokuwa kwa balamu aliyepokea ujira wa uganga (fedha na mali za kiganga) ili awalaani wana wa Israeli (Hesabu 22:7 “Wazee wa Moabu, na wazee wa Midiani, wakaenda, wakichukua ujira wa uganga mikononi mwao; wakamfikilia Balaamu, wakamwambia maneno ya Balaki.”)

Tamaa ya fedha na mali inaweza kukuingiza katika shida kubwa na hata ikakuharibu kabisa kama ilivyotokea kwa Gehazi yule mtumishi wa nabii Elisha amabye kwa kutamani fedha na mali aliingia katika matatizo makubwa ya maisha yake yote sawasawa na Neno la Mungu kwamba “Lakini hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu.” (1Tim 6:9). Hebu tazama habari hii ya Gehazi na tamaa ya fedha na mali

2Falme 5:20-22 “20 Lakini Gehazi, mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu, akasema, Tazama, bwana wangu amemwachilia huyo Naamani Mshami, asivipokee mikononi mwake vile vitu alivyovileta; kama Bwana aishivyo, mimi nitamfuata mbio, nipokee kitu kwake. 21 Basi Gehazi akamfuata Naamani. Naye Naamani, alipoona mtu apigaye mbio anakuja nyuma yake, alishuka garini amlaki, akasema, Je! Ni amani? 22 Akasema, Amani. Bwana wangu amenituma, kusema, Tazama, sasa hivi wamenijia kutoka milimani mwa Efraimu vijana wawili wa wana na manabii; uwape, nakuomba, talanta ya fedha, na mavazi mawili. 23 Naamani akasema, Uwe radhi, ukatwae talanta mbili. Akamshurutisha, akafunga talanta mbili za fedha ndani ya mifuko miwili, na mavazi mawili, akawatwika watumishi wake wawili; nao wakayachukua mbele……… 26 Akamwambia, Je! Moyo wangu haukuenda na wewe, hapo alipogeuka yule mtu katika gari ili akulaki? Je! Huu ndio wakati wa kupokea fedha, na kupokea mavazi, na mashamba ya mizeituni, na mizabibu, na kondoo, na ng'ombe, na watumwa, na wajakazi? 27 Basi ukoma wa Naamani utakushika wewe, na wazao wako hata milele. Naye akatoka usoni pake mwenye ukoma kama theluji.”

Matokeo ya tamaa ya mali na fedha ni uharibifu kama ilivyokuwa kwa gehazi na kama ilivyokuwa kwa Baalamu yule nabii mchawi aliyekuja kuuwa kwa upanga (Yoshua 13:22).

KUABUDU MALI/FEDHA (Ibada ya miungu)
Mali inaweza kukuzuia usiupate uzima wa milele yaani usiirithi ile ahadi ya Mungu Jehova ya maisha ya milele, siku moja Yesu aliuliza “Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?” (Marko 8: 36). Kumbe hakuna faida ya kuwa na mali na fedha halafu ukaukosa uzima wa milele.
Kuna watu katika maisha yao yamegeuza mali/fedha kuwa ndio Mungu wao, kuna watu wamegeuza kazi na biashara zao kuwa ndio Mungu wao kitu kinakuwa ni Mungu wako pale unapokipa kipaumbele kuliko unavyompa Mungu kipaumbele; yaani jambo lolote lililokaa katika nafasi ya Mungu ndio ibada yako, hata kama ni mke/mume/mtoto ikumuweka mbele zaidi ya mungu huyo ndiye ibada yako.
Kulikuwa na mtu mmoja kwenye Biblia ambaye aliweka mali mbele kuliko kitu chochote na Yesu akampa kazi ya kufanya na akaishindwa ile kazi kwasababu ya mali zake (mali/fedha zikamzuia)

Marko 10:17-23 “17 Hata alipokuwa akitoka kwenda njiani, mtu mmoja akaja mbio, akampigia magoti, akamwuliza, Mwalimu mwema, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele? 18 Yesu akamwambia, Kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu. 19 Wazijua amri, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usidanganye, Waheshimu baba yako na mama yako. 20 Akamwambia, Mwalimu, haya yote nimeyashika tangu utoto wangu. 21 Yesu akamkazia macho, akampenda, akamwambia, Umepungukiwa na neno moja. Enenda, ukauze ulivyo navyo vyote, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate. 22 Walakini yeye akakunja uso kwa neno hilo, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi. 23 Yesu akatazama kotekote, akawaambia wanafunzi wake, Jinsi itakavyokuwa shida wenye mali kuingia katika ufalme wa Mungu!”
Mtu wa Mungu kumbuka kuwa na fedha na mali sio dhambi kwani katika Biblia tunasoma habari za watumishi wa Mungu ambao walikuwa na fedha na mali nyingi na bado walimtumikia Mungu kwa mali zao, baadhi ya mifano ya watu hao ni Ibrahimu baba wa imani na Mariamu Magdalena ambao walimpendeza Mungu na Mungu aliwabariki.

TUNAWEZA KUSHINDA TAMAA YA FEDHA/MALI
Mtu wa Mungu kumbuka jambo hili, Yesu alikuja duniani ili aishinde dhambi na katka ushindi wa Yesu nasisi tumeishinda dhambi. Yesu alipojaribiwa katika hali ya mwili kabisa alimshinda ibilisi pale ibilisi alipomtamanisha kwa fahari ya dunia hii ni pamoja na fedha na mali, lakini Yesu alimshinda na akakataa kumsujudia shetani ili apewe mali, vivyo hivyo nasisi leo tunaishinda tamaa ya mali inayoletwa na ibilisi kwa jina la Yesu na kwa nguvu ya Neno lake.
Luka 4:5-8 “5 Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja. 6 Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo. 7 Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako. 8 Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.”

4.     DHAMBI YA UASI (NI SAWA NA DHAMBI YA UCHAWI)
Uasi ni roho kutoka kwa ibilisi mwenyewe, Neno la Mungu linaifananisha dhambi ya uasi kama ile ya uchawi (1Samweli 15:23 “Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi………..”), yaani muasi ni sawa na mchawi. Kwahiyo ukiona mtu anayo hiyo roho ya uasi katika maisha yake basi uchawi upo jirani naye sana au pengine anao pia uchawi.

a.      Uasi mbinguni
Hata kabla ulimwengu haujaumbwa roho hii ilionekana kwa mara ya kwanza ndani ya ibilisi akiwa ni malaika mbinguni.

Isaya 14:12-19 “12 Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa! 13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. 14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu. 15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo.……………”

Shetani alifanya uasi mbinguni pale aliposema …..Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu….. alitaka kukaa kwenye kiti cha Mungu Jehova au kwa lugha nyingine alitaka kumpindua Mungu, lakini uasi huu ulisababisha vita kubwa mbinguni

Ufunuo 12:7-8 “7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; 8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.”

Vita hii ilisababisha madhara makubwa mbinguni kwani theluthi ya malaika mbingu walioasi pamoja na ibilisi walitupwa pamoja na ibilisi huku duniani (Ufunuo 12:4 “Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake.”)

MUHIMU: Kabla ya mtu yoyote kuasi lazima shetani aingie ndani yake kwanza, kwa lugha nyingine shetani ndiye mhandisi (engineer) wa uasi wa aina zote. Tunasoma kwamba hata kabla yuda hajamsaliti (haja muasi) Yesu shetani aliingia ndani yake kwanza

Luka 22:2-4 “2 Na wakuu wa makuhani na waandishi walikuwa wakitafuta njia ya kumwua; maana walikuwa wakiwaogopa watu. 3 Shetani akamwingia Yuda, aitwaye Iskariote, naye ni mmoja wa wale Thenashara. 4 Akaondoka, akaenda akasema na wakuu wa makuhani na majemadari, jinsi atakavyoweza kumtia mikononi mwao.”


b.     Uasi duniani (Uasi wa Adamu)
Tangu shetani atupwe duniani roho ya uasi ikaingia duniani na ikaanza kutenda kazi kuanzia kwa mwanadamu wa kwanza yaani Adamu. Adamu alipomuasi Mungu, dhambi iliingia duniani.
Mwanzo 3:16-19 “16 Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala. 17 Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; 18 michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; 19 kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.”
Jambo baya ambalo hutokea katika kila dhambi ya uasi ni madhara ya uasi ambayo hayarekebishiki kabisa na hata yakirekebishika ni lazima Mungu aingilie kati YEYE mwenyewe.

c.      Uasi wa kora
Kora na familia yake pamoja na kundi lake la watu mia mbili na hamsini waliamka kinyume na Musa wakitaka kuchukua uongozi ambao Mungu alimpa Musa, roho hii ya uasi ilivyowaingia walijiona kwamba wao wako swan a Musa na Haruni na kwamba Mungu amewatuma na wao pia
Hesabu 16:1-49 “1 Basi Kora, mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, akatwaa watu, pamoja na Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu, na Oni, mwana wa Pelethi, waliokuwa wana wa Reubeni; 2 nao, pamoja na watu kadha wa kadha wa wana wa Israeli, watu mia mbili na hamsini, Wakuu wa mkutano, waliokuwa wateule wa mkutano, watu wenye sifa, wakainuka mbele ya Musa; 3 nao wakakusanyika kinyume cha Musa na Haruni, na kuwaambia, Ninyi inawatosha, kwa kuwa mkutano wote ni mtakatifu, kila mmoja miongoni mwao, Bwana naye yu kati yao; n'nini basi kujitukuza juu ya mkutano wa Bwana?.......... 28 Musa akasema, Kwa jambo hili mtajua ya kwamba Bwana amenituma, ili nifanye kazi hizi zote; kwa kuwa mimi sikuzifanya kwa akili zangu mwenyewe. 29 Kama watu hawa wakifa kifo cha sikuzote, kama watu wote wafavyo, au kama wakipatilizwa kwa mapatilizo ya watu wote; hapo basi Bwana hakunituma mimi. 30 Lakini Bwana akiumba kitu kipya, na hiyo nchi ikifunua kinywa chake na kuwameza, pamoja na wote walio nao, nao washukia shimoni wali hai; ndipo mtatambua ya kwamba watu hawa wamemdharau Bwana 31 Basi ilikuwa, hapo alipokwisha kusema maneno haya yote, nchi iliyokuwa chini yao ikapasuka; 32 nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na watu wa nyumba zao na wote walioshikamana na Kora, na vyombo vyao vyote. 33 Basi wao, na wote waliokuwa nao, wakashukia shimoni wali hai; nayo nchi ikawafunika wakaangamia kutoka mle mkutanoni……..49 Basi waliokufa kwa tauni walikuwa kumi na nne elfu na mia saba, zaidi ya hao waliokufa katika jambo la Kora.”

Kama ni livyosema hapo mwanzo, kila uasi hupelekea madhara makubwa sana, Hasira ya Mungu ilipowaka ardhi ilipasuka na Koran pamoja na wenzake wakamezwa wote nan chi wakiwa hai, wale watu 250 waliteketezwa kwa moto na wote waliowakuwa upande wao walipigwa kwa tauni. Watu waliokufa kutokana na uasi huo ni zaidi ya 14,950 katika siku moja. Uasi ni dhambi inayoleta maangamizo makubwa sana katika maisha ya mwanadamu.

d.     Uasi wa Absalomu
2Samweli 15:1-6 “1 Ikawa baada ya hayo, Absalomu akajiwekea tayari gari na farasi, na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake. 2 Tena Absalomu huondoka asubuhi na mapema, na kusimama kando ya njia ya lango; kisha ikawa, mtu ye yote aliyekuwa na neno, lililokuwa halina budi kufika kwa mfalme ili kuhukumiwa, Absalomu humwita mtu huyo kwake, na kumwuliza, Wewe u mtu wa mji gani? Naye akasema, Mtumwa wako ni mtu wa kabila fulani ya Israeli. 3 Naye Absalomu humwambia, Tazama, maneno yako ni mema yenye haki; lakini hapana mtu aliyeagizwa na mfalme kukusikiliza. 4 Tena Absalomu husema, Laiti mimi ningewekwa kuwa mwamuzi katika nchi hii, ili kila mtu mwenye neno au daawa aje kwangu, nimpatie haki yake! 5 Tena ikawa hapo alipokaribia mtu ye yote kumsujudia, hunyosha mkono wake, na kumshika, na kumbusu. 6 Hivyo ndivyo Absalomu alivyowatendea Israeli wote, waliomwendea mfalme ili wapate hukumu; na hivyo Absalomu akawadanganya watu wa Israeli.”

Absalomu pamoja na kuwa alikuwa ni mtoto wa Daudi aliyependwa sana na baba yake aliona kusubiri mpaka apewe madaraka itachukua muda mrefu sana hivyo akaamua kumpindua baba yake madarakani. Roho ya uasi ikamwingia naye akamsaliti baba yake na kumfanyia uovu usio tamkika ili amuondoe madarakani na lengo lake ilikuwa ni kumuua kabisa baba yake mzazi. Lakini matokeo ya uasi yalimpata, Absalomu alikufa kwasababu ya ule uasi.

2Samweli 18:32-33 32 Naye mfalme akamwambia yule Mkushi, Yule kijana, Absalomu, je! Yu salama? Yule Mkushi akajibu, Adui za bwana wangu mfalme, na wote wainukao ili kukudhuru, na wawe kama alivyo yule kijana. 33 Naye mfalme akataabika sana, akapanda juu, akaingia kile chumba kilichokuwa juu ya lango, akalia; na katika kwenda kwake alisema hivi, Mwanangu Absalomu! Ee mwanangu! Mwanangu Absalomu! Laiti ningalikufa badala yako, Absalomu, mwanangu, mwanangu!”

Mtu wa mungu Neno la Mungu linatuonya kwamba siku za mwisho kutakuwa na uasi mwingi katika ya wanadamu, kadiri unavyoona dhambi inaongeza kasi basi tambua kwamba ule mwisho uko karibu
2Timotheo 3:1-4 “1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, 3 wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, 4 wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;”

MAOVU YAKISAMEHEWA MAGONJWA/UDHAIFU/LAANA VINAONDOKA
Pamoja na balaa linaloletwa na dhambi katika maisha ya mwanadamu Mungu kwa Neema yake alimtoa mwana wake Yesu Kristo ili kwa kufa kwake sisi tupokee uzima na uponyaji na tuwe mbali na kuonewa na nguvu za giza.

Yohana 3:16, Wakolosai 1:13 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;”
Zaburi 103:3 “Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote,”

Isaya 33:24 “Wala hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa; watu wakaao humo watasamehewa uovu wao.”

Warumi 11:26-27 “26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake. 27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao.”


MAOVU, DHAMBI NA MAKOSA YAMETUWEKA MBALI NA MUNGU
Isaya 59:1-2 “1 Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; 2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.”

TOBA INALETA UPONYAJI WA MAGONJWA YA MWILI NA VITU VINGINE PIA
2Nyakati 7:13-15 “13 Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; 14 ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao. 15 Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa.”

TUKIMPA YESU MAOVU, DHAMBI NA MAKOSA YETU TUNAPONA MAGONJWA YA MIILI YETU NA MATATIZO YA MAISHA YETU
Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

KUSAMEHEWA DHAMBINI KUTOLEWA KATIKA UTAWALA WA GIZA
Wakolosai 1:13-14 “13 Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; 14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;”

HABARI YA MGONJWA ALIYESAMEHEWA DHAMBI NA KUPONA UGONJWA
Mathayo 9:1-7 “1 Akapanda chomboni, akavuka, akafika mjini kwao. 2 Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako. 3 Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru. 4 Naye Yesu, hali akijua mawazo yao, akasema, Mbona mnawaza maovu mioyoni mwenu? 5 Kwa maana rahisi ni lipi, ni kusema, Umesamehewa dhambi zako, au ni kusema, Ondoka, uende? 6 Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (amwambia yule mwenye kupooza) Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako. 7 Akaondoka, akaenda zake nyumbani kwake.”