Friday, February 26, 2016

UKOMBOZI WA ARDHI (Mwl Melechzedech Shalua)

SEMINA YA NENO LA MUNGU YA SIKU TATU (TAR 05-07/02/2016) KATIKA UKUMBI WA KWIDEKO – NGUDU KWIMBA. IMEANDALIWA NA NURU FELLOWSHIP NA UZIMA WA MILELE INTERNATIONAL MINISTRIES KWA KUSHIRIKIANA NA HUDUMA YA MANA MKOA WA MWANZA.

SIKU YA TATU (TAR 07/02/2016)
UKOMBOZI WA ARDHI ……….. Inaendelea – Mwl Melechzedech Shalua

Ø  Kwakweli ardhi inatoa maamuzi juu ya watu wanaokaa juu yake kwa kutegemea imekabidhiwa kwa Mungu yupi.
Ardhi inaweza kuolewa na kuzaa matunda kutegemea na Mungu aliyeioa, Isaya 62:4-5“4 Hutaitwa tena Aliyeachwa, wala nchi yako haitaitwa tena, Ukiwa; bali utaitwa Hefsiba; na nchi yako Beula;kwa kuwa Bwana anakufurahia ,na nchi yako itaolewa. 5 Maana kama vile kijana amwoavyo mwanamwali, ndivyo wana wako watakavyokuoa wewe; na kama vile bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.”

Ø  Ardhi haiwezi kuzaa pasipo kuolewa na kuzaa huko kunategemea na Mungu/mungu aliyeioa ardhi hiyo.

Uzao wa ardhi unaweza kubarikiwa na pia unaweza kulaaniwa, Kumb 28:4,18“4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. 18 Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.”

Ø  Ardhi inaweza kuwa haizai kutokana na laana. Ukiisemesha tu ardhi inaweza kuzaa kwaajili yako hatakama haizai kwaajili ya wengine
Asili ya kila kitu chenye uhai ni ardhi, Mwanzo 2:4-19
-          Bwana Mungu Akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi
-          Bwana Mungu akachipusha katika ardhi kila mti……….
-          Bwana Mungu akamfanyizi katika ardhi kila myama…..

Ø  Nchi/ardhi inaweza kuwatapika wenyeji na kuwatoa,
 Walawi 18:24-25“24 Msijitie unajisi katika mambo hayo hata mojawapo; kwa maana hizo taifa nitakazozitoa mbele zenu zimekuwa najisi kwa mambo hayo yote; 25 na hiyo nchi imekuwa najisi; kwa ajili ya hayo naipatiliza uovu wake juu yake, na hiyo nchi yatapika wenyeji wake na kuwatoa.”

Ø Nchi ikiwa najisi kwasababu ya wanadamu kuifanya iwe najisi, Mungu anaachilia adahbu juu ya hiyo nchi na nchi inaanza kuzaa mapooza

2Wafalme 2:19-22“19 Watu wa mjini wakamwambia Elisha, Angalia, twakusihi, mahali pa mji huu ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo; lakini maji yake hayafai, na nchi huzaa mapooza. 20 Akasema, Nileteeni chombo kipya, mtie chumvi ndani yake. Wakamletea. 21 Akatoka akaenda mpaka chemchemi ya maji, akatupa ile chumvi humo ndani, akasema, Bwana asema hivi, Nimeyaponya maji haya; hakutatoka huko tena kufa wala kuzaa mapooza. 22 Hivyo yale maji yakapona hata leo, sawasawa na neno la Elisha alilolinena.”
Ndio maana Mungu anasema ataiponya nchi ikiwa watu wake walioitwa kwa jina lake watajinyenyekesha na kuomba, hii inamaana kuwa ardhi inaweza kuwa na ugonjwa na ndio maana Mungui anaweza kuiponya kwani hauwezi kuponya kisichoumwa
Damu ikimwagika kwenye ardhi, ardhi haiwezi kunena mema

2Samwel 21:1-4“1 Kulikuwa na njaa siku za Daudi muda wa miaka mitatu, mwaka kwa mwaka; naye Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, Ni kwa ajili ya Sauli, na kwa nyumba yake yenye damu, kwa kuwa aliwaua hao Wagibeoni. 2 Ndipo mfalme akawaita Wagibeoni akawaambia; (basi Wagibeoni si wa wana wa Israeli, ila ni wa masalio ya Waamori; na wana wa Israeli walikuwa wamewaapia; lakini Sauli akatafuta kuwaua katika juhudi yake kwa ajili ya wana wa Israeli na Yuda;) 3 basi Daudi akawaambia hao Wagibeoni, Niwatendee nini? Na kwa tendo gani nifanye upatanisho, mpate kuubariki urithi wa Bwana? 4 Na hao Wagibeoni wakamwambia, Si jambo la fedha wala dhahabu lililo kati ya sisi na Sauli, au nyumba yake; wala si juu yetu kumwua mtu ye yote katika Israeli. Akasema Mtakayoyanena, ndiyo nitakayowatendea ninyi.”

Ø  Ardhi inao uwezo wa kusikia, kutunza kile ilichosikia na kutekeleza kile ilichosemeshwa
Kumb 30:19-2019 Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; 20 kumpenda Bwana, Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wako, na wingi wa siku zako; upate kukaa katika nchi Bwana aliyowaapia baba zako, Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kuwa atawapa.”

Musa anapoongea na wana wa Israel anafanya mbingu na nchi kuwa shahidi ili ikumbukwe daima

Kumb 31:14-30“24 Basi ikawa hapo Musa alipomaliza kuandika maneno ya torati hii katika chuo, hata yakaisha, 25 ndipo Musa akawaamuru Walawi waliokuwa wakilichukua sanduku la agano la Bwana akawaambia, 26 Twaeni chuo hiki cha torati, mkiweke kando ya sanduku la agano la Bwana, Mungu wenu, ili kiwepo kama shahidi juu yako. 27 Kwa kuwa uasi wako naujua, na shingo yako ngumu; angalieni, mimi nikali hai pamoja nanyi leo, mmekuwa waasi juu ya Bwana; siuze nitakapokwisha kufa! 28 Nikutanishieni wazee wote wa kabila zenu, na maakida yenu, ili niseme maneno haya masikioni mwao, na kuwashuhudizia mbingu na nchi juu yao. 29 Kwa sababu najua baada ya kufa kwangu mtajiharibu kabisa, na kukengeuka katika njia niliyowaamuru; nayo mabaya yatawapata siku za mwisho, kwa vile mtakavyofanya maovu machoni pa Bwana kumtia kasirani kwa kazi ya mikono yenu. 30 Musa akasema maneno ya wimbo huu masikioni mwa kusanyiko la wana wa Israeli hata yakaisha.”

Kumb 32:1“1 Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitanena; Na nchi isikie maneno ya kinywa changu.”

Yeremia 22:29-30“29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana. 30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.”

Ø  Unaweza kufanya eneo kwenye ardhi kuwa sehemu ya kukutana na Mungu wako
Madhabahu ya Munguu inajengwa na Yakobo katika ardhi ili pawe ukumbusho wa agano

Mwanzo 28:16-22“16 Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli Bwana yupo mahali hapa, wala mimi sikujua. 17 Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni. 18 Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake. 19 Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu. 20 Yakobo akaweka nadhiri akisema, Mungu akiwa pamoja nami, akinilinda katika njia niiendeayo, na kunipa chakula nile, na nguo nivae; 21 nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu. 22 Na jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi.”

Alama unayoiweka kwenye ardhi ni ukombusho wako na Mungu wako

Mwanzo 35:6-7“6 Basi Yakobo akafika Luzu, ulio katika nchi ya Kanaani, ndio Betheli, yeye na watu wote waliokuwa pamoja naye. 7 Akajenga huko madhabahu, akapaita mahali pale, El-Betheli; kwa sababu huko Mungu alimtokea, hapo alipomkimbia ndugu yake.”

Ø  Ardhi inao uwezo wa kufurahi na kuwafurahisha wanaokaa juu yake kwasababu ya toba iliyofanywa ili kuirejesha ardhi kwa Mungu

Ardhi inayoomboleza inanyima Baraka kwa watoto wa Mungu, Yoeli 1:10“10 Shamba limeharibika, nchi inaomboleza; maana nafaka imeharibika, divai mpya imekauka, mafuta yamepunguka.”

Baada ya kwenda mbele za Mungu kwa toba Mungu anatoa Baraka juu ya ardhi, ardhi inafurahi na kutoa matunda

Yoeli 2:21“Ee nchi, usiogope; furahi na kushangilia; kwa kuwa Bwana ametenda mambo makuu.”

Unapoomba toba na kubomoa madhabahu za giza na kubariki ardhi nayo ardhi inafurahi

Yeremia 51:48-49“48 Ndipo mbingu, na nchi, na vitu vyote vilivyomo, vitaimba kwa furaha juu ya Babeli; kwa maana watu waangamizao watamjilia kutoka kaskazini, asema Bwana. 49 Kama vile Babeli alivyowaangusha watu wa Israeli waliouawa, ndivyo watakavyoanguka katika Babeli watu wa nchi yake nzima waliouawa.”

Ø  Ardhi iano uwezo wa kumuondoa mtu na kumlinda mtu aliye juu yake. Haijalishi kama unajua au haujui kawaida ya miungu/Mungu wa mahali unapokaa, kama ukikosea utashambuliwa/utapigwa na Mungu/miungu

2Falme 17:24-28“24 Naye mfalme wa Ashuru akaleta watu kutoka Babeli, na Kutha, na Ava, na Hamathi, na Sefarvaimu, akawaweka katika miji ya Samaria badala ya wana wa Israeli; wakaumiliki Samaria, wakakaa katika miji yake. 25 Basi ikawa, wakati ule walipoanza kukaa huko, hawakumcha Bwana; kwa hiyo Bwana akapeleka simba kati yao, nao wakawaua baadhi yao. 26 Kwa hiyo wakamwambia mfalme wa Ashuru, wakasema, Wale wa mataifa uliowahamisha, na kuwaweka katika miji ya Samaria, hawaijui kawaida ya Mungu wa nchi; kwa hiyo amepeleka simba kati yao, na tazama, wanawaua, kwa sababu hawaijui kawaida ya Mungu wa nchi. 27 Ndipo mfalme wa Ashuru akatoa amri, akasema, Mpelekeni mmojawapo wa makuhani, mliowachukua kutoka huko; aende akakae huko, akawafundishe kawaida ya Mungu wa nchi. 28 Basi mmoja wa makuhani waliochukuliwa kutoka Samaria akaenda akakaa katika Betheli, akawafundisha jinsi ilivyowapasa kumcha Bwana.”

Ø  Mapepo yanaweza kumilikishwa ardhi na yakadai kisheria kuwa na uhalali wa kuwepo mahali pale walipomilikishwa

Marko 5:1-17“1 Wakafika ng'ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi. 2 Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu; 3 makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo; 4 kwa sababu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, akaikata ile minyororo, na kuzivunja-vunja zile pingu; wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu za kumshinda. 5 Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikata-kata kwa mawe. 6 Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia; 7 akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese. 8 Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu. 9 Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tu wengi. 10 Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile. 11 Na hapo milimani palikuwa na kundi kubwa la nguruwe, wakilisha. 12 Pepo wote wakamsihi, wakisema, Tupeleke katika nguruwe, tupate kuwaingia wao. 13 Akawapa ruhusa. Wale pepo wachafu wakatoka, wakaingia katika wale nguruwe; nalo kundi lote likatelemka kwa kasi gengeni, wakaingia baharini, wapata elfu mbili; wakafa baharini. 14 Wachungaji wao wakakimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani. Watu wakatoka walione lililotokea. 15 Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mwenye pepo, ameketi, amevaa nguo, ana akili zake, naye ndiye aliyekuwa na lile jeshi; wakaogopa. 16 Na wale waliokuwa wameona waliwaeleza ni mambo gani yaliyompata yule mwenye pepo, na habari za nguruwe. 17 Wakaanza kumsihi aondoke mipakani mwao.”

-          - Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi/ardhi ile……..Wakaanza kumsihi aondoke mipakani mwao……….


JINSI YA KUOMBA/KUKOMBOA ARDHI

ü  Anza na toba na kuomba utakaso wa Damu ya Yesu ili Damu iweze kufuta uhalali wa umiliki wa miungu mingine ili usishambuliwe
ü  Tumia vifungu vya Biblia kumnyang’anya na kumuondoa shetani katika ardhi. Tumia sheria ya kimbingu kumhukumu shetani
ü  Tumia nyayo katika kumiliki na kutawala (Kwanini nyayo na sio viatu?)

a.       Kumb 11:22-24“22 Kwa kuwa kwamba mtayashika kwa bidii maagizo haya yote niwaagizayo, kuyafanya; kumpenda Bwana, Mungu wenu, na kutembea katika njia zake zote, na kushikamana naye; 23 ndipo Bwana atakapowafukuza mataifa haya yote mbele yenu, nanyi mtamiliki mataifa makubwa yenye nguvu kuwapita ninyi. 24 Kila mahali mtakapokanyaga kwa nyayo za miguu yenu patakuwa penu; tokea hilo jangwa, na Lebanoni, na tokea mto wa Frati, mpaka bahari ya magharibi, itakuwa ndiyo mipaka yenu.”

b.      Yoshua 3:14-16“14 Hata ikawa, hao watu walipotoka katika hema zao, ili kuvuka Yordani, makuhani waliolichukua sanduku la agano wakatangulia mbele ya watu, 15 basi hao waliolichukua hilo sanduku walipofika Yordani, na nyayo za makuhani waliolichukua sanduku zilipotiwa katika maji ya ukingoni, (maana Yordani hujaa hata kingo zake na kufurika wakati wote wa mavuno), 16 ndipo hayo maji yaliyoshuka kutoka juu yakasimama, yakainuka, yakawa chuguu, mbali sana, huko Adamu, mji ule ulio karibu na Sarethani, na maji yale yaliyotelemkia bahari ya Araba, yaani Bahari ya Chumvi, yakatindika kabisa; watu wakavuka kukabili Yeriko.”

c.       Yoshua 1:3“Kila mahali zitakapopakanyaga nyayo za miguu yenu, nimewapa ninyi, kama nilivyomwapia Musa.”


SOMO: UKOMBOZI WA ARDHI /NGUVU INAYOTEMBEA NA MAJINA (Mwl Melechzedech Shalua na Rachel Peter)

SOMO: UKO MAHALI SAHIHI AMBAPO MUNGU AMEKUSUDIA?/UKOMBOZI WA ARDHI

(Somo limefundishwa na Mwl Melechzedeck Shalua – Huduma ya MANA Mwanza)

SEMINA YA NENO LA MUNGU YA SIKU TATU (TAR 05-07/02/2016) KATIKA UKUMBI WA KWIDEKO – NGUDU KWIMBA. IMEANDALIWA NA NURU FELLOWSHIP NA UZIMA WA MILELE INTERNATIONAL MINISTRIES KWA KUSHIRIKIANA NA HUDUMA YA MANA MKOA WA MWANZA.

SIKU YA PILI TAREHE 06/FEBRUARI/2016

3Yohana 1:2“Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo.”

MAMBO YANAYOFANYA WATU WASIFANIKIWE KWA VIWANGO MUNGU ALIVYO WAKUSUDIA
                          
Kuna mambo mbalimbali katika maisha ambayo yanawafanya walio wengi wasiweze kufanikiwa kwa viwango ambavyo Mungu aliwakusudia wafanikiwe. Biblia inatoa mifano ya watumishi wa Mungu ambao asili yao, majina yao, mazingira yao, n.k yalikuwa kikwazo katika utumishi wao.

MFANO : MTUMISHI WA MUNGU MUSA

JINA
Kutoka 2:1-10“1 Mtu mmoja wa nyumba ya Lawi akaondoka akaoa binti mmoja wa Lawi.
 2 Yule mwanamke akachukua mimba akazaa mwana, na alipoona ya kuwa ni mtoto mzuri akamficha miezi mitatu. 3 Na alipokuwa hawezi kumficha tena, akampatia kisafina cha manyasi akakipaka sifa na lami, akamtia mtoto ndani yake, akakiweka katika majani kando ya mto. 4 Umbu lake mtoto akasimama mbali ili ajue yatakayompata. 5 Basi binti Farao akashuka, aoge mtoni, na vijakazi wake wakatembea kando ya mto; naye akakiona kile kisafina katika majani, akamtuma kijakazi wake kwenda kukileta. 6 Akakifungua, akamwona mtoto, na tazama, mtoto yule analia. Basi akamhurumia, akasema, Huyu ni mmojawapo wa watoto wa Waebrania. 7 Basi umbu lake mtoto akamwambia binti Farao, Je! Niende nikamwite mlezi katika wanawake wa Kiebrania, aje kwako, akunyonyeshee mtoto huyu? 8 Binti Farao akamwambia, Haya! Enenda. Yule kijana akaenda akamwita mama yake yule mtoto. 9 Binti Farao akamwambia, Mchukue mtoto huyu, ukaninyonyeshee, nami nitakupa mshahara wako. Yule mwanamke akamtwaa mtoto, akamnyonyesha. 10 Mtoto akakua, naye akamleta kwa binti Farao, akawa mwanawe. Akamwita jina lake Musa, akasema, Ni kwa sababu nalimtoa majini.”
Jina la Musa halikutokana na majina ya kiebrania bali lilitokana na kutolewa kwenye maji na hii ikamafanya akatengeneza tabia ya jina hilo
Hivyo asili ya Musa amefungamanishwa na maji, yaani roho za majini (Tabia ya kuziba nafasi wazi/kuwakilisha)

Kutoka 3:1-14“1 Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu. 2 Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. 3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei. 4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa. 5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu. 6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu. 7 Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; 8 nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. 9 Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa. 10 Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri. 11 Musa akamwambia Mungu, Mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri? 12 Akasema, Bila shaka mimi nitakuwa pamoja nawe; na dalili ya kuwa nimekutuma ndiyo hii; utakapokuwa umekwisha kuwatoa hao watu katika Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu. 13 Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n'nani? Niwaambie nini? 14 Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO;akasema,Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli;MIMI NIKO amenituma kwenu.”

Ø  Uwepo wa Musa kwa wana wa Israel unawakilisha uwepo wa Mungu, maana yake ni kwamba uwepo wa Musa ulionesha uwepo wa Mungu wa Musa.

Kutoka 32:1-4“1 Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Haruni, wakamwambia, Haya! Katufanyizie miungu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata. 2 Haruni akawaambia, Zivunjeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee. 3 Watu wote wakazivunja pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, wakamletea Haruni. 4 Akaipokea mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha; nao wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.”

Ø  Kwa kuondoka kwa Musa kwenda mlimani kuomba, uwepo wa Mungu wa Musa uliondoka katikakati ya wana wa Israeli ndio maana wakatengeneza mungu mwingine.
Walizivunja pete za dhahabu za masikio yao ili kuondosha usikivu kwa Mungu wa Musa na kuweka kwa mungu mpya (ndama wa dhahabu)
Hivyo jina la Musa liilibeba uwakilishi wa yule (MUNGU) aliyemtuma. Katika utumishi unapaswa kutafakali jina lako linabeba ujumbe gani katika kulitimiza kusudi la Mungu.

TABIA

i.                     Tabia ya upole
Hesabu 12:3”Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.”
Mungu alimuona Musa kuwa mtu mpole kuliko watu wote wa wakati wake. Japo asili ya Musa haikuwa upole kutokana na msingi wa uzao wake wa Lawi ambao walikuwa wakali na wenye hasira.

ii.                 Tabia ya ukali
Kutoka 32:19, 26-28“19 Hata alipoyakaribia marago akaiona ile ndama, na ile michezo. Hasira ya Musa ikawaka, akazitupa zile mbao mikononi mwake, akazivunja chini ya mlima 26 ndipo Musa akasimama katika mlango wa marago, akasema, Mtu awaye yote aliye upande wa Bwana, na aje kwangu. Wana wa Lawi wote wakamkusanyikia 27 Akawaambia, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kila mtu na ajifunge upanga wake pajani mwake, akapite huko na huko toka mlango hata mlango kati ya marago, mkamchinje kila mtu ndugu yake, na kila mtu mwenziwe na kila mtu jirani yake. 28 Na hao wana wa Lawi wakafanya kama vile alivyosema Musa, wakaanguka siku ile kama watu elfu tatu.”

iii.                 Tabia kutoka kuzaliwa na kulelewa kwa Musa
Kutoka 2:1-2“1 Mtu mmoja wa nyumba ya Lawi akaondoka akaoa binti mmoja wa Lawi. 2 Yule mwanamke akachukua mimba akazaa mwana, na alipoona ya kuwa ni mtoto mzuri akamficha miezi mitatu.”

Ø  Ukoo wa Musa ulitokana na Lawi ambao Yakobo baba yao anasema walikuwa wakali na hasira

Mwanzo 49:1-7“1 Yakobo akawaita wanawe, akasema, Kusanyikeni, ili niwaambie yatakayowapata siku za mwisho. 2 Kusanyikeni, msikie, enyi wana wa Yakobo, Msikilizeni Israeli, baba yenu. 3 Reubeni, u mzaliwa wangu wa kwanza, Nguvu zangu, na malimbuko ya uwezo wangu. Umewapita wengine kwa ukuu na kwa nguvu. 4 Umeruka mpaka kama maji, basi usiwe na ukuu, Kwa sababu ulikipanda kitanda cha baba yako, Ukakitia unajisi; alikipandia kitanda changu. 5 Simeoni na Lawi ni ndugu; Panga zao ni silaha za jeuri. 6 Nafsi yangu, usiingie katika siri yao, Fahari yangu usiungane na kusanyiko lao, Maana katika ghadhabu yao walimuua mtu, Na kwa ukaidi wao walikata mshipa wa ng'ombe; 7 Ghadhabu yao na ilaaniwe, maana ilikuwa kali, Na hasira yao, maana ilikuwa haina huruma. Nitawagawa katika Yakobo, Nitawatawanya katika Israeli.”

Ø  Asili ya ukoo wa Musa ni ukali na hasira
 (Mwanzo 34:7-27“7 Wanawe Yakobo waliposikia hayo, wakaja kutoka nyikani; nao wakasikitika sana, wakakasirika mno, kwa sababu amefanya upumbavu katika Israeli kwa kulala na binti Yakobo, neno lisilojuzu kutendeka…………..25 Ikawa siku ya tatu, walipokuwa wakiumwa sana, wana wawili wa Yakobo, Simeoni na Lawi, nduguze Dina, wakatwaa kila mtu upanga wake, wakaujia mji kwa ujasiri, wakawaua waume wote. 26 Wakawaua Hamori, na Shekemu mwanawe, kwa makali ya upanga, wakamtwaa Dina katika nyumba ya Shekemu, wakatoka. 27 Wana wa Yakobo wakawajilia hao waliouawa, wakauteka nyara mji kwa sababu wamemharibu umbu lao.”)

Ø  Hasira yao (Lawi) ilikuwa imefungwa kwenye laana
(Mwanzo 49:7“Ghadhabu yao na ilaaniwe, maana ilikuwa kali, Na hasira yao, maana ilikuwa haina huruma. Nitawagawa katika Yakobo, Nitawatawanya katika Israeli.”)na laana hiyo ilimfuatilia Musa katika utumishi wake (Kutoka 32:19-20), naye aliendelea kuua (Kutoka 32:25-29)

Ø  Hasira ilipoteza tumaini la utumishi wa Musa hadi Musa akatamani kufa
(Hesabu 11:8-15“9 Umande ulipoyaangukia marago wakati wa usiku, hiyo mana ilianguka pamoja nao. 10 Basi Musa akawasikia watu wakilia katika jamaa zao zote, kila mtu mlangoni pa hema yake; na hasira za Bwana zikawaka sana; Musa naye akakasirika. 11 Musa akamwambia Bwana, Mbona umenitenda uovu mimi mtumishi wako? Kwa nini sikupata neema machoni pako, hata ukanitwika mzigo wa watu hawa wote juu yangu? 12 Je! Ni mimi niliyewatungisha mimba watu hawa wote je! Ni mimi niliyewazaa, hata ikawa wewe kuniambia, Haya, wachukue kifuani mwako, mfano wa baba mwenye kulea achukuavyo mtoto anyonyaye, uende nao mpaka nchi uliyowaapia baba zao? 13 Nipate wapi nyama ya kuwapa watu hawa wote? Kwani wanililia, wakisema Tupe nyama, tupate kula. 14 Mimi siwezi kuwachukua watu hawa wote peke yangu, kwa kuwa ni mzigo mzito sana wa kunishinda. 15 Na kama ukinitenda hivi, nakuomba uniulie mbali, kwamba nimepata fadhili mbele ya macho yako; nami nisiyaone haya mashaka yangu.”)

Ø  Musa anakasirika na kukosea maelekezo ya Mungu na kupiga mwamba mara mbili, hasira hiyo inampelekea Musa kukosa kufika katika nchi ya ahadi
(Hesabu 20:2-12“2 Na hapo hapakuwa na maji kwa ule mkutano; wakajikusanya juu ya Musa na juu ya Haruni…………………….. 7 Bwana akasema na Musa, akinena, 8 Twaa ile fimbo, ukawakusanye mkutano, wewe na Haruni ndugu yako, ukauambie mwamba mbele ya macho yao utoe maji yake, nawe utawatokezea maji katika mwamba, na hivyo utawanywesha maji mkutano na wanyama wao. ……………. 11 Musa akainua mkono wake akaupiga ule mwamba kwa fimbo yake mara mbili; maji yakatoka mengi, mkutano wakanywa na wanyama wao pia. 12 Bwana akamwambia Musa na Haruni, Kwa kuwa hamkuniamini mimi, ili kunistahi mbele ya macho ya wana wa Israeli, basi kwa sababu hiyo, hamtawaingiza kusanyiko hili katika ile nchi niliyowapa.”)




SIKU YA PILI – SEHEMU YA PILI
MAJINA – By MAMA KITULO (RACHEL PETER)

Ø  Ibrahim (Baba wa Mataifa)
Mwanzo 17:1-6 “1 Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini na kenda, Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu. 2 Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe, nami nitakuzidisha sana sana. 3 Abramu akaanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema, 4 Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi, 5 wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi. 6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako.”
Kuitwa Ibrahim Mungu alimaanaisha kuwa ndani ya jina hilo limebeba Baraka ya ubaba wa mataifa

Ø  Sara (Mama wa Mataifa)
Mwanzo 17:15-17“15 Mungu akamwambia Ibrahimu, Sarai mkeo, hutamwita jina lake Sarai, kwa kuwa jina lake litakuwa Sara. 16 Nami nitambariki, na tena nitakupa mwana kwake, naam, nitambariki, naye atakuwa mama wa mataifa, na wafalme wa kabila za watu watatoka kwake.”
Jina la Sara lina maana ya kuwa mama wa mataifa na kwake watatoka wafalme
Kurithi majina kuna madhara (Usirithi majina ovyo ovyo)

Nahumu 1:14“Tena Bwana ametoa amri katika habari zako, ya kwamba asipandwe tena mtu awaye yote mwenye jina lako; toka nyumba ya miungu yako nitakatilia mbali sanamu ya kuchora, na sanamu ya kuyeyusha; nitakufanyia kaburi lako; kwa maana u mbovu.”

Ø  Hivyo ni vyema kutowafuatilisha watoto majina ya miungu au majina yasiyojulikana madhabahu zake. Unapoomba Mungu akupe mtoto umuombe akupe na jina la mtoto huyo kama vile bikira Mariam alivyoambiwa na Malaika Gabrieli (Mathayo 1:23“Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.”)

1Samweli 25:3, 25“3 Na jina la mtu huyo aliitwa Nabali; na jina la mkewe aliitwa Abigaili, na huyo mwanamke alikuwa mwenye akili njema, mzuri wa uso; bali yule mwanamume alikuwa hana adabu, tena mwovu katika matendo yake; naye alikuwa wa mbari ya Kalebu. 25 Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.”

Ø  Nabali ilimaanisha upumbavu na ni kweli mtu huyu akawa ni mpumbavu sawa sawa na jina lake
Danieli 1:6-7“6 Basi katika hao walikuwapo baadhi ya wana wa Yuda, Danieli, na Hanania, na Mishaeli, na Azaria. 7 Mkuu wa matowashi akawapa majina; alimwita Danieli, Belteshaza; na Hanania akamwita Shadraka; na Mishaeli akamwita Meshaki; na Azaria akamwita Abednego.”

Ø  Neno la Mungu linatuambia kwamba Danieli, na Hanania, na Mishaeli, na Azaria walibadilishwa majina yao na kupewa majina sawa sawa utawala ule waliowachukua mateka
Mwanzo 1:41-45“41 Farao akamwambia Yusufu, Tazama, nimekuweka juu ya nchi yote ya Misri. 42 Farao akavua pete yake ya muhuri mkononi mwake, akaitia mkononi mwa Yusufu; akamvika mavazi ya kitani nzuri, na kumtia mkufu wa dhahabu shingoni mwake. 43 Akampandisha katika gari lake la pili alilokuwa nalo. Na watu wakapiga kelele mbele yake, Pigeni magoti. Hivyo akamweka juu ya nchi yote ya Misri. 44 Farao akamwambia Yusufu, Mimi ni Farao, na bila amri yako, mtu asiinue mkono wala mguu katika nchi yote ya Misri. 45 Farao akamwita Yusufu, Safenath-panea; akamwoza Asenathi, binti Potifera, kuhani wa Oni, kuwa mkewe Yusufu akaenda huko na huko katika nchi yote ya Misri.”

Ø  Yusufu anapewa jina kuendana na miungu ya Misri ili atawale Misri na wakamuoza binti wa kuhani, yaani Yusufu aliungamanishwa na na miungu ya Misri

Isaya 26:13-14“13 Ee Bwana, Mungu wetu, mabwana wengine zaidi ya wewe wametumiliki; lakini kwa msaada wako peke yako tutalitaja jina lako. 14 Wao wamekufa, hawataishi; wamekwisha kufariki, hawatafufuka; kwa sababu hiyo umewajilia, na kuwaangamiza, na kuupoteza ukumbusho wao.”
Kupitia jina unaweza kuendelea kumilikiwa na waliokufa, yaani unaelekezwa na kusukumwa (na nguvu ya kiroho) kuishi maisha ya mwenye jina japo alikwisha kufa





SIKU YA PILI – SEHEMU YA TATU
UKOMBOZI WA ARDHI – Mwl Melechzedech Shalua

Ø  Katika kitabu cha Mwanzo tunaona kuwa ardhi inalaaniwa kwaajili ya Adamu
Mwanzo 3:17-19“17 Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; 18 michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; 19 kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.”

Ø  Ardhi inaposemeshwa kwa habari za mtu Fulani au kitu Fulani inaweza kutunza kumbukumbu za maisha yako
Yeremia 22:29-30“29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana. 30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.”

Ø  Ardhi inaandika na kutoa taarifa juu yako
Yeremia 17:13”Ee Bwana, tumaini la Israeli, wote wakuachao watatahayarika. Wao watakaojitenga nami wataandikwa katika mchanga, kwa sababu wamemwacha Bwana, kisima cha maji yaliyo hai.”

Ø  Ardhi inaweza kuolewa na miungu mingine
Isaya 62:4“Hutaitwa tena Aliyeachwa, wala nchi yako haitaitwa tena, Ukiwa; bali utaitwa Hefsiba; na nchi yako Beula;kwa kuwa Bwana anakufurahia ,na nchi yako itaolewa.”

Ø  Unaweza kutumia njia panda kuongelesha watu wa eneo husika
Ezekiel 21:18-24“18 Neno la Bwana likanijia tena, kusema, 19 Tena, mwanadamu, ujiwekee njia mbili, upanga wa mfalme wa Babeli upate kuja; hizo mbili zitatoka katika nchi moja; ukaandike mahali, upaandike penye kichwa cha njia iendayo mjini. 20 Utaagiza njia, upanga upate kufikilia Raba wa wana wa Amoni, na kufikilia Yuda katika Yerusalemu, wenye maboma. 21 Maana mfalme wa Babeli alisimama penye njia panda, penye kichwa cha njia hizo mbili, ili atumie uganga; aliitikisa mishale huko na huko, akaziuliza terafi, akayatazama maini. 22 Katika mkono wake wa kuume alikuwa na kura ya Yerusalemu, kuviweka vyombo vya kubomolea, kufumbua kinywa katika machinjo, kuiinua sauti kwa kupiga kelele sana, kuweka vyombo vya kubomolea juu ya malango, kufanya maboma, na kujenga ngome. 23 Jambo hili litakuwa kwao kama uganga wa ubatili, mbele ya macho yao waliowaapia viapo lakini ataufanya uovu ukumbukwe, ili kwamba wakamatwe. 24 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kwa kuwa mmeufanya uovu wenu ukumbukwe, kwa maana makosa yenu yamefunuliwa, hata dhambi zenu zikaonekana kwa matendo yenu; kwa sababu mmekumbukwa, mtakamatwa kwa mkono.”


Kwa habari ya nyayo katika ardhi
Zaburi 56:5-6“5 Mchana kutwa wanapotosha maneno yangu, Mawazo yao yote ni juu yangu kunitakia mabaya. 6 Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu, Kwa kuwa wameniotea nafsi yangu.”

-          Wachawi hutumia nyayo za watu kuwaloga
-          Mipango yote unayoipanga inaweza kuharibiwa na wachawi kupitia nyayo zako
-       Kwa mtu uliyeokoka unapaswa kuombea nyayo zako ili kila unapokanyaga unaaachilia moto wa Mungu

Ayubu 13:27“Waitia miguu yangu katika mkatale, na kuyaaua mapito yangu yote; Wajiandikia alama kuzizunguka nyayo za miguu yangu;”

-      Mikatale ni kitu kinachofunga, watu wanaweza kuzichukua nyayo zako na kuzifunga ili wewe usifanikiwe
-          Mapito yako yote wanayaua na mipango yako ya mafanikio inateketea kabisa
-          Wanaandika na kusemesha nyayo za miguu yako ili usifanikiwe
 Ayubu 33:11“Hunitia miguu yangu katika mkatale, Na mapito yangu yote huyapeleleza.”

-         Kupitia ardhi ambapo ndipo zinpokanyaga nyayo, shetani anafunga watu na mafanikio yao yote.

UKO MAHALI SAHIHI AMBAPO MUNGU AMEKUSUDIA? (Mwl Melechzedech Shalua)

SOMO: UKO MAHALI SAHIHI AMBAPO MUNGU AMEKUSUDIA?/UKOMBOZI WA ARDHI

(Somo limefundishwa na Mwl Melechzedeck Shalua – Huduma ya MANA Mwanza)

SEMINA YA NENO LA MUNGU YA SIKU TATU (TAR 05-07/02/2016) KATIKA UKUMBI WA KWIDEKO – NGUDU KWIMBA. IMEANDALIWA NA NURU FELLOWSHIP NA UZIMA WA MILELE INTERNATIONAL MINISTRIES KWA KUSHIRIKIANA NA HUDUMA YA MANA MKOA WA MWANZA.

SIKU YA KWANZA TAREHE 05/FEBRUARI/2016

UKO MAHALI SAHIHI AMBAKO MUNGU AMEKUKUSUDIA KUWA ?

3Yohana 1:2“Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo.”

Isaya 1:18-20“18 Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu. 19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi; 20 bali kama mkikataa na kuasi mtaangamizwa kwa upanga; maana kinywa cha Bwana kimenena haya.”

Zab 16:3“Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.”
Umeokoka ndiyo,  unamtumikia Mungu, na unasoma Neno la Mungu na mafanikio yote yaliyoandikwa ndani ya biblia. Swali; Je, Kwanini hauli mema ya nchi?

Ø Kwakweli kila aliyeamua kumfuata Yesu anaamini kuwa ndani ya Yesu kuna mafanikio ya kiroho na kimwili na huu ni ukweli. Ingawa sijui kama tunafaidi Baraka ambazo Mungu ameziweka kwaajili yetu, maana pamoja na ahadi nyingi za Baraka hatujawa sehemu ya mafanikio hayo.

Luka 11:5-13“5 Akawaambia, Ni nani kwenu aliye na rafiki, akamwendea usiku wa manane, na kumwambia, Rafiki yangu, nikopeshe mikate mitatu, 6 kwa sababu rafiki yangu amefika kwangu, atoka safarini, nami sina kitu cha kuweka mbele yake; 7 na yule wa ndani amjibu akisema, Usinitaabishe; mlango umekwisha fungwa, nasi tumelala kitandani mimi na watoto wangu; siwezi kuondoka nikupe? 8 Nawaambia ya kwamba, ijapokuwa haondoki ampe kwa kuwa ni rafiki yake, lakini kwa vile asivyoacha kumwomba, ataondoka na kumpa kadiri ya haja yake. 9 Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa. 10 Kwa kuwa kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. 11 Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka? 12 Au akimwomba yai, atampa nge? 13 Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”

Ø  Kuna wakati hatutapewa mahitaji yetu kwasababu ya urafiki wetu na Yesu, bali kwa vile usivyoacha kuomba. Kuomba na kutafuta ni vitu viwili tofauti, Kutafuta ni kujua kanuni, taratibu na sheria za Mungu unazopaswa kufuata ili ukutane na Mungu, Bisheni maana yake ni “Zungumza na Mungu mara kwa mara”

Rumi 8:12-17 “12 Basi, kama ni hivyo, ndugu, tu wadeni, si wa mwili tuishi kwa kufuata mambo ya mwili, 13 kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi. 14 Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu. 15 Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba. 16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; 17 na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.”

Ø  Wakati mwingine unaingia kuomba na unaona kabisa Mungu hajajibu maombi yako na kama kajibu ni kwa kiwango kidogo, Kwanini hajajibu? Tatizo ni kwangu au kwa Mungu?

Rum 7:14-25 “14 Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi. 15 Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda. 16 Lakini kama nikilitenda lile nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema. 17 Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu 18 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati. 19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 21 Basi nimeona sheria hii, ya kuwa kwangu mimi nitakaye kutenda lililo jema, lipo lililo baya. 22 Kwa maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani, 23 lakini katika viungo vyangu naona sheria iliyo mbali, inapiga vita na ile sheria ya akili zangu, na kunifanya mateka ya ile sheria ya dhambi iliyo katika viungo vyangu. 24 Ole wangu, maskini mimi! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti? 25 Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.”

Ø  Ndani ya mtu mmoja kuna sheria mbili zinatawala, Mwili umefungiwa sheria ambayo inatuzuia kumtafuta Mungu, sheria ya mwili imeweka kizuizi ambacho hakuna unavyoweza kutenda sawa sawa na mapenzi ya Mungu. Kuna mikataba/maagano yaliyofungwa katika maisha yako yanayokuzuia kutenda sawa na mapenzi ya Mungu. Tazama maisha ya ndugu zako yanafanana na yako (wewe uliye okoka) na wengine ni wapagani wanakuzidi.

Zaburi 11:1-3“1 Bwana ndiye niliyemkimbilia. Mbona mnaiambia nafsi yangu, Kimbia kama ndege mlimani kwenu? 2 Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, Wanaitia mishale yao katika upote, Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo. 3 Kama misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini?”

Ø  Msingi wa maisha yako umejengwaje? (Vizuri au Vibaya)
Yeremia 1:4-9“4 Neno la Bwana lilinijia, kusema, 5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa. 6 Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto. 7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru. 8 Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana. 9 Ndipo Bwana akaunyosha mkono wake, akanigusa kinywa changu; Bwana akaniambia, Tazama, nimetia maneno yangu kinywani mwako;”

Uchafu wa kwanza ambao ungemzuia Yeremia kutumika ulikuwa tumboni, Msingi wa Yeremia ungeweza kuharibika tangu tumboni. Kuna misingi ambayo ingemzuia Yeremia maombi yake yasijibiwe ambayo imetokea tangu tumboni.

Zaburi 51:1-5“1 Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu. 2 Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu. 3 Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima. 4 Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, Na kufanya maovu mbele za macho yako. Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo, Na kuwa safi utoapo hukumu. 5 Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani.”

Daudi anaamua kuomba toba baada ya kuona kuna mlango unaomzuia asikutane na Mungu kwa viwango vya tofauti na mlango huo ni wa misingi ya kuzaliwa kwake (Zaburi 51:5 “Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani.”). Daudi aliamua kushughulikia uovu baada ya kujua kuwa kuna misingi ya uzinzi inagharimu maisha yake ya kiutumishi, alishughulikia uovu ili aweze kula mema ya nchi, yaani kufikia kiwango cha juu cha mafanikio