Monday, June 13, 2016

SEMINA YA MANA - MOROGORO Na Mwl. Chritopher Mwakasege (08-12/06/2016) SOMO:KUA KATIKA NEEMA ILI UNUFAIKE NA MSALABA (Imeandikwa na Samson&Joan Mollel, 0767 664 338 – www.uzimawamileleministries.blogspot.com)

SIKU YA TANO (12/06/2016)

Somo linaongozwa na Neno kutoka:- 2Petro 3:18 “Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata milele.” 2Timoth 2:1 “Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu.”
Kumbuka kuwa NEEMA ni jambo unalopewa bila ya kulifanyia kazi (Warumi 4:4-6 “4 Lakini kwa mtu afanyaye kazi, ujira wake hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni. 5 Lakini kwa mtu asiyefanya kazi, bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauwa, imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki. 6 Kama vile Daudi aunenavyo uheri wake mtu yule ambaye Mungu amhesabia kuwa na haki pasipo matendo,” )

JINSI NEEMA NA DAMU YA YESU INAVYOWEZA KUKUPA HAKI ULIYOPOTEZA KWASABABU YA HISTORIA YA KITU ULICHOFANYA AU KILICHOFANYWA NA MTU ANAYEHUSIKA NA WEWE.

Yeremia 22:29-30 “29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana. 30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.”

Kuna tofauti kati ya taifa na nchi, ukisema taifa unaongelea watu na ukisema nchi unaongelea ardhi (land/earth).

Hebu tuangalie habari ya watoto ambao wamejitahidi sana kusonga mbele lakini hata wafanye vipi hawatoki, yaani hawawezi kuvuka kile kiwango cha wazazi wao, wakijitahidi sana wanaishia palepale wazazi wao walipoishia.

Hesabu 30:2-6 “2 Mtu atakapomwekea Bwana nadhiri, au, atakapoapa kiapo ili kufunga nafsi yake kwa kifungo, asilitangue neno lake; atafanya sawasawa na hayo yote yamtokayo kinywani mwake. 3 Tena mtu mke atakapomwekea Bwana nadhiri, na kufunga nafsi yake kwa kifungo, naye aketi katika nyumba ya babaye, katika ujana wake; 4 babaye naye akasikia nadhiri yake, na kile kifungo chake alichofungia nafsi yake, na babaye akamnyamazia; ndipo nadhiri zake zote zitathibitika, na kila kifungo alichofungia nafsi yake kitathibitika. 5 Lakini kama huyo babaye akimkataza siku hiyo aliyosikia; nadhiri zake ziwazo zote, wala vifungo vyake alivyoifungia nafsi yake havitathibitika; na Bwana atamsamehe, kwa kuwa babaye alimkataza. 6 Tena kama amekwisha kuolewa na mume, wakati huo wa nadhiri zake, au wa neno hilo alilolitamka kwa midomo yake pasipo kufikiri, alilojifungia;”

Inawezekana mtu alinena bila kufikiri maneno yale yakampa Mungu nafasi au yakampa shetani nafasi katika maisha yake. Yawezekana hayo yalinenwa na wazazi wake, au mababu zake na yakampa shetani nafasi katika familia yao na hali hiyo inaendela kuwatesa familia.

Waebrania 7:5, 9-10 “5 Na katika wana wa Lawi nao, wale waupatao ukuhani, wana amri kutwaa sehemu ya kumi kwa watu wao, yaani, ndugu zao, kwa agizo la sheria, ijapokuwa wametoka katika viuno vya Ibrahimu. 9 Tena yaweza kusemwa ya kuwa, kwa njia ya Ibrahimu, hata Lawi apokeaye sehemu ya kumi alitoa sehemu ya kumi; 10 kwa maana alikuwa katika viuno vya baba yake, hapo Melkizedeki alipokutana naye.”

Kutokana na andiko hili; wastani wa kizazi kibiblia ni miaka 100, kutoka Ibrahim mpaka Lawi ni vizazi vine (Ibrahimu – Isaka – Yakobo – Lawi), kwahiyo sadaka aliyoitoa Ibrahimu hata kabla Isaka hajazaliwa ilitolewa mpaka na Lawi. Kama mababu zako walitoa sadaka au walifanya agano na miungu maana yake hata wewe umefanya hilo agano.

Ezekieli 21:21-23 “21 Maana mfalme wa Babeli alisimama penye njia panda, penye kichwa cha njia hizo mbili, ili atumie uganga; aliitikisa mishale huko na huko, akaziuliza terafi, akayatazama maini. 22 Katika mkono wake wa kuume alikuwa na kura ya Yerusalemu, kuviweka vyombo vya kubomolea, kufumbua kinywa katika machinjo, kuiinua sauti kwa kupiga kelele sana, kuweka vyombo vya kubomolea juu ya malango, kufanya maboma, na kujenga ngome. 23 Jambo hili litakuwa kwao kama uganga wa ubatili, mbele ya macho yao waliowaapia viapo lakini ataufanya uovu ukumbukwe, ili kwamba wakamatwe.”

Mfalme wa Babeli alienda kufanya uganga kwenye njia panda na sadaka aliyoitoa katika uganga huo ni maini. Sasa fikiria kwamba uganga na sadaka hiyo ulifanywa na babu yako na wewe hujui chochote na BWANA anasema ataufanya uovu ukumbukwe katika familia hiyo. Baadae kwasababu wewe hukujua habari ya kutoa sadaka walizotoa babu zako na ndugu zako unaanza kushangaa magonjwa yanaanza, kama walikuwa wakitoa sadaka za miguu ya wanyama familia inasuimbuliwa na tatizo la miguu, kama ni maini kunakuwa na tatizo la maini n.k.

Agano ni mapatano yanayomfunga mtu kwenye mahusiano (Mwanzo 17:1-2, 7, 9, 20-21 “1 Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini na kenda, Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu. 2 Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe, nami nitakuzidisha sana sana…7 Agano langu nitalifanya imara kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako…….9 Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada yako……20 Na kwa habari za Ishmaeli nimekusikia, nimembariki, nitamzidisha, nami nitamwongeza sana sana. Atazaa maseyidi kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kuu. 21 Bali agano langu nitalifanya imara kwa Isaka, ambaye Sara atakuzalia majira kama haya mwaka ujao.”)

Katika uzao wa Ibrahimu, Ishamaeli mtoto wa kijakazi alipewa Baraka nje ya agano la Mungu na Isaka alipewa Baraka ndani ya agano na Mungu, sasa kwakuwa Agano ni mapatano yanayomfunga mtu kwenye mahusiano, Isaka (Taifa la Israeli) akivunja agano lazima apate shida kwakuwa anayo mahusiano na Mungu na Mungu hawezi kukubali kirahisi rahisi mahusiano yavunjike. Lakini Ishmaeli hata akienda tofauti na maelekezo ya Mungu ataendelea kufanikiwa tu kwakuwa yuko nje ya agano.

Hii ndio maana, kama kuna mahali wazazi waliingia katika agano wakapata mali halafu watoto wakavunja agano lililowapa wazazi mali hiyo, hiyo mali inapotea yote na hata kama ni kampuni inaanguka yote.

Rumi 5:12 “Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi;”

Kutoka 20:5 “Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,”

Uovu ni udhaifu unaotokea unapomkataa Mungu na akaondoa uwekezaji wake katika maisha yako.

Daniel baada ya kukisoma kitabu cha Yeremia alikubali kwamba amefanya dhambi yeye na taifa lote (kimsingi yeye hakuishiriki moja kwa moja ila aliikubali kuwa nayeye ameifanya kwakuwa ilifanywa na wazee/baba wake).

Daniel 9:4-9 “4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake; 5 tumefanya dhambi, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu, tumeasi, naam, hata kwa kuyaacha maagizo yako na hukumu zako; 6 wala hatukuwasikiliza watumishi wako, manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, na wakuu wetu, na baba zetu, na watu wote wa nchi. 7 Ee Bwana, haki ina wewe, lakini kwetu sisi kuna haya ya uso, kama hivi leo; kwa watu wa Yuda, na kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa Israeli wote, walio karibu na hao walio mbali, katika nchi zote ulikowafukuza, kwa sababu ya makosa yao waliyokukosa. 8 Ee Bwana, kwetu sisi kuna haya ya uso, kwa wafalme wetu, na wakuu wetu, na baba zetu, kwa sababu tumekutenda dhambi. 9 Rehema na msamaha ni kwa Bwana Mungu wetu, ingawa tumemwasi;”

Baada ya kukiri kumtenda Mungudhambi kwakuwa walifanya uasi, Danieli alimuomba Mungu awasamehe

Danieli 9:16-19 “16 Ee Bwana sawasawa na haki yako yote, nakusihi, hasira yako na ghadhabu yako zigeuzwe na kuuacha mji wako Yerusalemu, mlima wako mtakatifu; maana kwa sababu ya dhambi zetu, na maovu ya baba zetu, Yerusalemu na watu wako wamepata kulaumiwa na watu wote wanaotuzunguka. 17 Basi sasa, Ee Mungu wetu, yasikilize maombi ya mtumishi wako, na dua zake, ukaangazishe uso wako juu ya patakatifu pako palipo ukiwa, kwa ajili ya Bwana. 18 Ee Mungu wangu, tega sikio lako, ukasikie; fumbua macho yako ukautazame ukiwa wetu, na mji ule ulioitwa kwa jina lako; maana hatukutolei maombi yetu kwa sababu ya haki yetu, lakini kwa sababu ya rehema zako nyingi.”

Haijalishi umezaliwa jangwani/ Misri/ Babeli au umejikuta kwenye shida gani ya kifamilia iliyosababishwa na makosa/dhambi/maovu, unaweza kwenda mbele za Mungu na kuziungama dhambi zote na damu ya Yesu Kristo ikapita na kufuta yote na ukawa mtu huru.

Hata kama umefanya kazi ya Mungu chini ya kiwango unakuwa umekosa mbele za Mungu hivyo inakupasa kuomba toba kwa damu ya Yesu (Warumi 3:23-26 “23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; 24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; 25 ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili aonyeshe haki yake ,kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi zote zilzotangulia kufanywa. 26 apate kuonyesha haki yake wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kumhesabu haki yeye amwaminiye Yesu.”)

Waebrania 9:14-15 “14 basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai? 15 Na kwa sababu hii ni mjumbe wa agano jipya, ili, mauti ikiisha kufanyika kwa kukomboa makosa yaliyokuwa chini ya agano la kwanza, hao walioitwa waipokee ahadi ya urithi wa milele.”

Damu ya Yesu inapoachiliwa inapita na kufungua mafaili yako yote mpaka pale bustani ya Eden na kuanza kukagua mambo yote yaliyofanyika yanayoleta shida, wakati damu ikifungua mafaili yako kwa kipindi hicho Yesu Kristo (KUHANI MKUU) anasimama kama mdhamini wakati kesi yako ikiendelea wewe unakuwa uko huru nje ya kifungo na damu inakuwakilisha (yaani damu ya Yesu inasimama kama wakili mahali pako ikenena mema juu yako).

Kuna watu wanaota ndoto kuwa wanakula chakula, kula chakula kwenye ndoto ni ishara ya agano la ukumbusho; yaani wafu wanakukumbusha kuwa walifanya agano na mizimu na wewe upo katika agano hilo. Agano ni urithi, hivyo lazima afe mtu ili agano lirithishwe kwenda kwa mtu mwingine aliye hai.

MAOMBI YA KUVUNJA MAAGANO KWAAJILI YA WATU WANAOOTA WANAKULA KWENYE NDOTO…………………….. MAOMBI YANAENDELEA………..

MAELEFU ELFU YA WATU WAMEMPOKEA YESU……. HALELUYAAA….


*****MWISHO WA SEMINA*****

Sunday, June 12, 2016

SEMINA YA MANA - MOROGORO Na Mwl. Chritopher Mwakasege (08-12/06/2016) SOMO:KUA KATIKA NEEMA ILI UNUFAIKE NA MSALABA (Imeandikwa na Samson&Joan MolleL, 0767 664 338 – www.uzimawamileleministries.blogspot.com)

SIKU YA NNE – SEMINA YA VIJANA (ASUBUHI - MCHANA)
Ezekiel 22:30-31 “30 Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu. 31 Kwa sababu hiyo nimemwaga ghadhabu yangu juu yao; nimewateketeza kwa moto wa hasira yangu; nami nimeileta njia yao wenyewe juu ya vichwa vyao, asema Bwana MUNGU.”
SOMO: WITO KWA KIJANA ILI MUNGU AMTUMIE KATIKA KUOMBEA NCHI
1.     Unapoitwa kuombea nchi unaitwa na Mungu ili uingizwe katika kundi maalum sana kwa Mungu. Ni kwanini Mungu atafute mtu (Ezekiel 22:30-31) wakati anaona na kumjua kila mtu? Ni kwasababu jambo analotaka ulifanye ni zito sana na sio kila mtu anaouwezo wa kulibeba
·         Kundi lingine maalum ni pale Yesu aliposema amekuja kutafuta waliopotea (Ambao sasa ndio watu waliookoka) Mathayo 15:24 “Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.”
·         Kundi lingine maalum ni wale watakaomwabu Mungu katika roho na kweli, Yohana 4:23 “Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.” Kuna tofauti kati ya kumsifu na kumuabudu Mungu, Kusifu ni kueleza matendo makuu ya Mungu na kuabudu ni kumwelezea Mungu ni nani kwako.
·         Kundi lingine maalum ni watenda kazi (Luka 10:2 “Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.”). Watumishi katika nyumba ya BWANA ni wengine lakini watenda kazi ni wachache, mtenda kazi siku zote anatafuta kufanya mapenzi ya Mungu.
Isaya 59:16a “Akaona ya kuwa hapana mtu, akastaajabu kwa kuwa hapana mwombezi…………”. Kuna watu wengi sana wanaomba kwaajili ya mahitaji yao binafsi na shida zao, lakini ni wachache sana wanaoweza kuwa na mzigo kwaajili ya nchi
Kwasababu ya kukosa mtu wa kuiombea nchi, Mungu ameipiga nchi kwa ghadhabu yake
2.     Maombi ya kuombea nchi yanayomkaribisha Mungu awe mmoja wa wawekezaji muhimu kwaajili ya maendeleo na mafanikio ya nchi husika
Matendo 17:26-28 “26 Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao; 27 ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.”
Katika hali ya kawaida viongozi wan chi wanapotaka wawekezaji waje ili nchi iweze kuwa na maendeleo makubwa; lazima nchi itaingia kwenye gharama kubwa za kuweka sera za kuwavuta/kuwavutia wawekezaji ikiwa ni pamoja na kufanya matangazo katika vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa.
Inapofika wakati wa kumkaribisha Mungu au miungu katika uwekezaji, sio rahisi sana ukasikia peupe wakisema kama nchi kuwa wanamkaribisha Mungu/miungu kuwekeza katika nchi isipokuwa kwa nchi chache sana ambazo zimeweza kufanya hivyo kama vile Japan na baadhi ya nchi kiarabu.
Katika baadhi ya nchi kama Tanzania, kumkaribisha Mungu/miungu kama muwekezaji vipo katika viwango vya mtu mmoja mmoja na wanamkaribisha Mungu/miungu katika biashara/kazi……. Nk.
Tunasoma katika Biblia kuwa mfalme Uzia alimkaribisha Mungu kuwa muwekezaji katika uongozi wake, katika mashamba na mifugo yake na Mungu alimfanikisha sana (2Nyakati 26:1-5 “1 Na watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia, naye alikuwa mwenye miaka kumi na sita, wakamfanya awe mfalme mahali pa Amazia babaye. 2 Huyo akajenga Elathi, akaurudisha kwa Yuda, baada ya kulala mfalme pamoja na babaze. 3 Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala; akatawala huko Yerusalemu miaka hamsini na miwili; na jina la mamaye aliitwa Yekolia wa Yerusalemu. 4 Akafanya yaliyo ya adili machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyafanya Amazia babaye. 5 Akajitia nia amtafute Mungu katika siku za Zekaria, aliyekuwa na fahamu katika maono ya Mungu; na muda alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.”)
Yeremia 29:7-11 “7 Kautakieni amani mji ule, ambao nimewafanya mchukuliwe mateka, mkauombee kwa Bwana; kwa maana katika amani yake mji huo ninyi mtapata amani. 8 Maana Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Manabii walio kati yenu, na wabashiri wenu, wasiwadanganye ninyi, wala msisikilize ndoto zenu, mnazootesha. 9 Kwa maana kwa jina langu hutabiri maneno ya uongo kwenu; mimi sikuwatuma, asema Bwana. 10 Maana Bwana asema hivi, Babeli utakapotimiziwa miaka sabini, nitawajilia ninyi, na kulitimiza neno langu jema kwenu, kwa kuwarudisha mahali hapa. 11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.”
Mungu aliwapeleka wana wa Israeli mateka huko Babeli, lakini anawaambia wamkaribishe awe muwekezaji katika mji waliochukuliwa mateka ndipo watakapofanikiwa.
Tukimfanya Mungu kuwa muwekezaji katika nchi na ikatoakea shida/janga, tukimlilia Mungu kwa habari ya tatizo letu iwe ni Ukame, mafuriko, tetemeko n.k. Mungu atatuambia kama ameleta yeye au ni shetani ameleta au ni uzembe wetu, yeye Mungu atatuambia na kutupa njia sahihi ya kutatua tatizo hilo kwakuwa nay eye amewekeza kwetu.

3.     Usikubali kikwazo chochote kikuzuie katika kuukubali wito
Unapofanya kazi ya Mungu, fanya kama vile hakuna mtu mwingine anayefanya ila ni wewe peke yako, uwe mwaminifu katika eneo ulilopewa. Usiruhusu kikwazo chochote kikuzuie
        i.            Umri usiwe kikwazo
2Nyakati 26:1-5 “1 Na watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia, naye alikuwa mwenye miaka kumi na sita, wakamfanya awe mfalme mahali pa Amazia babaye. 2 Huyo akajenga Elathi, akaurudisha kwa Yuda, baada ya kulala mfalme pamoja na babaze. 3 Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala; akatawala huko Yerusalemu miaka hamsini na miwili; na jina la mamaye aliitwa Yekolia wa Yerusalemu. 4 Akafanya yaliyo ya adili machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyafanya Amazia babaye. 5 Akajitia nia amtafute Mungu katika siku za Zekaria, aliyekuwa na fahamu katika maono ya Mungu; na muda alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.” Yeremia 1:6 “Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.”
Uzia alikuwa na miaka 16 alipoanza kutawala na Yeremia alijiona ni mdogo sana kuifanya kazi ya Mungu, lakini Mungu anapokuletea wito anafahamu yote hayo na anajua kwamba atakufanikisha.
     ii.            Nikikubali kuomba inamaanisha sitafanya kazi nyingine?
Angalia habari ya Uzia, alikuwa mfalme na alifanya majukumu ya kifalme (kiungozi) lakini pia alikuwa ni mkulima na mfugaji, 2Nyakati 26:10 “Akajenga minara tena nyikani, akachimba mabirika mengi, maana alikuwa na ng'ombe tele; katika Shefela pia, na katika nchi tambarare; tena alikuwa na wakulima na watunza mizabibu milimani, na katika mashamba ya neema; maana yeye alipenda ukulima.” pamoja na mambo yote hayo mfalme uzia aliweza kumuomba Mungu kwa bidii  . 2Nyakati 26:4-5 “4 Akafanya yaliyo ya adili machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyafanya Amazia babaye. 5 Akajitia nia amtafute Mungu katika siku za Zekaria, aliyekuwa na fahamu katika maono ya Mungu; na muda alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.”
Fahamu kwamba maombi ya kuombea nchi hayakutoi kwenye nafasi yako au kazi yako
Angali pia habari za nabii Danieli (soma kitabu cha Daniel), aliandaliwa kwa miaka 3 ili atumike kwa Nebukadreza. Kilichomsaidia Daniel na wenzake kupata kazi iliyokuwa na changamoto nyingi ni kwasababu walikuwa wanaomba, ukisoma sura ya pili Daniel ameanza kazi alidumu katika awamu nne za uongozi yaani awamu ya mfalme Nebukadreza, Belshaza, Dario na Koreshi. Lakini Daniel alifanikiwa katika vipindi vyote hivyo kwakuwa alidumu katika kuomba.


   iii.            Mimi sijui kuomba
Watu wengi wanapoitwa na Mungu huwa na visingizio vingi, Musa alijitahidi sana kujitetea kwa visingizio vingi lakini mwisho Mungu ndiye aliyemuwezesha kuutumia wito huo. Hata kama hujui kuomba, Mungu aliyekuita yeye atakupeleka “kindergatten” ya maombi mpaka utajua kuomba, Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.”.



SIKU YA NNE (11/06/2016)
Somo linaongozwa na Neno kutoka:- 2Petro 3:18 “Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata milele.” 2Timoth 2:1 “Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu.”
Kumbuka kuwa NEEMA ni jambo unalopewa bila ya kulifanyia kazi (Warumi 4:4-6 “4 Lakini kwa mtu afanyaye kazi, ujira wake hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni. 5 Lakini kwa mtu asiyefanya kazi, bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauwa, imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki. 6 Kama vile Daudi aunenavyo uheri wake mtu yule ambaye Mungu amhesabia kuwa na haki pasipo matendo,” )
Inaendelea………………..Mungu anavyotumia Damu ya Yesu kukurudishia na kukupa haki zako ulizonyimwa/zilizopotea
   iv.            Damu inampa Mungu uhalali wa kukulinda na kukupigania dhidi ya adui
Kutoka 12:21-23, 12-13 “21 Hapo ndipo Musa akawaita wazee wa Israeli, na kuwaambia, Nendeni, mkajitwalie wana-kondoo kama jamaa zenu zilivyo mkamchinje pasaka. 22 Nanyi twaeni tawi la hisopu, mkalichovye katika ile damu iliyo bakulini na kukipiga kizingiti cha juu, na miimo miwili ya mlango, kwa hiyo damu iliyo katika bakuli; tena mtu ye yote miongoni mwenu asitoke mlangoni mwa nyumba yake hata asubuhi. 23 Kwa kuwa Bwana atapita ili awapige hao Wamisri; na hapo atakapoiona hiyo damu katika kizingiti cha juu, na katika ile miimo miwili, Bwana atapita juu ya mlango, wala hatamwacha mwenye kuharibu aingie nyumbani mwenu kuwapiga ninyi. 12 Maana nitapita kati ya nchi ya Misri usiku huo, nami nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, wa mwanadamu na wa mnyama; nami nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya Misri; Mimi ndimi Bwana. 13 Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba mtakazokuwamo; nami nitakapoiona ile damu, nitapita juu yenu, lisiwapate pigo lo lote likawaharibu, nitakapoipiga nchi ya Misri.”
Paska sio jina la sikukuu, pasaka ni jina la sadaka ambayo BWANA aliwaagiza wana wa Israeli wajitwalie wana-kondoo na ndio sadaka hiyo ikaitwa pasaka, Mungu naye alimtoa pasaka (sadaka) yaani Kristo 1Wakorintho 5:7 “Basi, jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo;”
·         Mungu alisema nitakapoiona hiyo damu nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya Misri; pigo halikuwapata Israeli, sio kwasababu wao ni Israeli ni kwasababu ya damu na imani walioiweka katika damu ile (Waebrania 11:8 “Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako.”)
·         Damu haikuenda kiujumla jumla, iliekezwa kwa kila familia na pale ilipobidi familia ziliungana
·         Kuna jambo la muda, damu iliwekewa muda wa kuifanya kazi ile (Usiku hawakuruhusiwa kutoka nje) kwahiyo damu ilibana muda
·         Damu ilibeba eneo, eneo la nyumba za wana wa Israeli ndani kulikuwa ni salama, yaani kama wangetoka nje hawangekuwa salama
Damu ya Yesu ukiitumia kwa imani inafanya ofisi ya Kuhani Mkuu (Yesu) iingie kazini. Mahali popote ambapo unataka damu ilinde au ifanye kazi lazima ulitambulishe hilo eneo katika ulimwengu wa roho, kwa lugha nyingine ni kuweka wakfu.
LEO TUTAFANYA ZOEZI KWA VITENDO, TUTAMWAGA DAMU YA DAMU YA YESU HAPA UWANJANI, BWANA YESU AMENIRUHUSU KUFANYA HILO ZOEZI NA AMENIAHIDI KWAMBA YEYE MWENYE (KUHANI MKUU) ATAINGIA KAZINI.
Yeremia 22:29-30 “29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana. 30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.”
Kuna watu ambao maisha yao yamefungwa katika ardhi, hii imetokana na ibada za miungu au laana nyingine. Inawezekana umefungwa kwenye ardhi ya nyumbani kwenu na hauwezi kupiga tena hatua kwenda mbele katika maisha yako. Leo tunamwaga damu ya Yesu inayonena mema ili kuondoa uhalali wa nguvu za giza zilizokufunga katika ardhi……………………..
MAOMBI YAMEFANYIKA KWA SEHEMU KUBWA SANA LEO, WATU WAMEFUNGULIWA, MAPEPO YALIYOKAA KATIKA ARDHI NA KUWAFUNGA WATU YANAKIMBIA OVYO OVYO UWANJANI NA WATU WANAZIDI KUFUNGULIWA…………….



***KARIBU TENA SIKU YA KESHO JUMAPILI AMBAYO NI MWISHO WA SEMINA***

SEMINA YA MANA - MOROGORO Na Mwl. Chritopher Mwakasege (08-12/06/2016) SOMO:KUA KATIKA NEEMA ILI UNUFAIKE NA MSALABA

SIKU YA TATU (10/06/2016)
Somo linaongozwa na Neno kutoka:- 2Petro 3:18 “Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata milele.” 2Timoth 2:1 “Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu.”
Kumbuka kuwa NEEMA ni jambo unalopewa bila ya kulifanyia kazi (Warumi 4:4-6 “4 Lakini kwa mtu afanyaye kazi, ujira wake hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni. 5 Lakini kwa mtu asiyefanya kazi, bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauwa, imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki. 6 Kama vile Daudi aunenavyo uheri wake mtu yule ambaye Mungu amhesabia kuwa na haki pasipo matendo,” )
Kama unataka kuipokea hii NEEMA mpokee Yesu ndani yako (Yohana 1:14, 16 “14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli. 16 Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.”)
Inaendelea………………..Mungu anavyotumia Damu ya Yesu kukurudishia na kukupa haki zako ulizonyimwa/zilizopotea
Warumi 4:25, 3:22-28 “25 ambaye alitolewa kwa ajili ya makosa yetu, na kufufuliwa ili mpate kuhesabiwa haki. 22 ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti; 23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; 24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; 25 ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili aonyeshe haki yake ,kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi zote zilzotangulia kufanywa. 26 apate kuonyesha haki yake wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kumhesabu haki yeye amwaminiye Yesu. 27 Ku wapi, basi, kujisifu? Kumefungiwa nje. Kwa sheria ya namna gani? Kwa sheria ya matendo? La! Bali kwa sheria ya imani. 28 Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.”
Kinachotufanya tuhesabiwe haki ni kwaajili ya imani tuliyonayo katika damu ya Yesu, (Warumi 10:17 “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.” Waebrani 11:1 “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.”)
Ile kwambauna imani kwa Yesu haina maana kuwa unayo imani kwa damu yake, unaweza kumwamini Yesu lakini usiamini katika damu yake, au ukaamini nusu nusu katika damu yake au ukaamini nusu katika Neno lake.
Kuna mambo kadha wa kadha ya kuangalia jinsi Mungu anavyoitumia damu ya Yesu kutufanya tukubalike kwake
a.      Mungu anaangalia na kusikiliza damu ya Yesu inasema nini juu ya dhambi zako
Walawi 17:11 “Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi.”
Kwa sheria za kimbingu ili utake kupatana na Mungu lazima kuwe na damu itakayonena kwa niaba yako (niaba ya nafsi yako) mbele za Mungu, hivyo ni damu pekee yenye kuweza kukupatanisha na Mungu kwa sheria aliyojiwekea katika ulimwengu wa roho. Hii ni kwasababu damu inabeba uhai lakini pia damu inaongea/ina nena (Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.”)
Waebrani 9:22-24 “22 Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo. 23 Basi ilikuwa sharti nakala za mambo yaliyo mbinguni zisafishwe kwa hizo, lakini mambo ya mbinguni yenyewe yasafishwe kwa dhabihu zilizo bora kuliko hizo. 24 Kwa sababu Kristo hakuingia katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu;” Mungu haangalii mtu anaangalia damu inasema nini, Yesu hakuingia patakatifu mwenyewe aliingia kwa damu yake aliyoimwaga
1Yohana 5:8-9 “8 Kwa maana wako watatu washuhudiao mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja. 9 Kisha wako watatu washuhudiao duniani, Roho, na maji, na damu; na watatu hawa hupatana kwa habari moja. Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe.” Kwa lugha nyingine kuna mashahidi Mbinguni na duniani, damu haipo mbinguni ilimwagika duniani ili upatane nayo ukiisha kupatana nayo ROHO anabeba ushuhuda na kuupeleka Mbinguni
b.     Anasamehe dhambi akishasikia damu inataja jina lako
Mungu anaisikiliza damu inayonena mema (Damu ya Yesu) ili ikutetee na ndio maana ya toba, Warumi 4:4-8 “4 Lakini kwa mtu afanyaye kazi, ujira wake hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni. 5 Lakini kwa mtu asiyefanya kazi, bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauwa, imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki. 6 Kama vile Daudi aunenavyo uheri wake mtu yule ambaye Mungu amhesabia kuwa na haki pasipo matendo, 7 Heri waliosamehewa makosa yao, Na waliositiriwa dhambi zao. 8 Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi.” (Msisitizo upo katika mstari wa 7a)
Baraka zinaachiliwa kwa waliosamehewa dhambi ndipo wanapewa haki zao, Wakolosai 1:13-14 “13 Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; 14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;”
Ukombozi maana yake ni kufunguliwa kutoka kwenye adhabu uliyopewa na ukashindwa kuilipa wewe ile adhabu (ukashindwa kulipa malipo stahiki ya adhabu ile), na baada ya wewe kushindwa akatokea mtu mwingine na kukulipia malipo stahiki kwa adhabu uliyoistahili wewe, na hivyo ndivyo Yesu alivyofanya kwa kutulipia malipo stahiki ya adhabu ya mauti kutokana na dhambi zetu. Neno la Mungu linasema mshahara wa dhambi ni mauti (na hii ni sheria ya Mbinguni), na hivyo imekuwa ni sheria katika ulimwengu wa roho, sasa Mungu anadai na shetani anadai mauti (kwakuwa mauti ndio malipo stahiki) ili kukumbolewa na dhambi. Ukikombolewa, damu inaenda na jina lako kwa Mungu kwamba umekombolewa tayari na umeachwa huru na adhabu ya mauti.
Ndani ya msamaha wa dhambi kuna ukombozi, Luka 5:17-26 “………….. 18 Na tazama, wakaja watu wanamchukua kitandani mtu mwenye kupooza; wakataka kumpeleka ndani na kumweka mbele yake. 19 Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu. 20 Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako……………….. 24 Lakini, mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (alimwambia yule mwenye kupooza). Nakuambia, Ondoka, ujitwike kitanda chako, ukaende zako nyumbani kwako. 25 Mara hiyo akasimama mbele yao, akajitwika kile alichokilalia, akaenda zake nyumbani kwake, huku akimtukuza Mungu……………..”
Kwakuwa ndani ya msamaha wa dhambi kuna ukombozi, Yesu alimwambia “Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako” na mara ile akapona ugonjwa wa kupooza. Ni muhimu kushughulika na dhambi ilikufunga, amini katika damu ya Yesu. Mungu anaangalia damu ya Yesu inasema nini, ikisema msamehe tu huyo anafunguliwa.
c.      Anasitiri dhambi
Warumi 4:7 “Heri waliosamehewa makosa yao, Na waliositiriwa dhambi zao
Isaya 43:25, 44:22 “Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako. Nimeyafuta makosa yako kama wingu zito, na dhambi zako kama wingu; unirudie; maana nimekukomboa.”
Ukisitiri kitu maana yake hujakiondoa, yaani kipo ila kimefunikwa kwa muda fulani tu.
Zaburi 19:12-14 “12 Ni nani awezaye kuyatambua makosa yake? Unitakase na mambo ya siri. 13 Umzuie mtumishi wako asitende mambo ya kiburi, Yasinitawale mimi. Ndipo nitakapokuwa kamili, Nami nitakuwa safi, sina kosa lililo kubwa. 14 Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mwokozi wangu.” Zaburi 90:8 “Umeyaweka maovu yetu mbele zako, Siri zetu katika mwanga wa uso wako.”
Dhambi inapokuwa siri ni siri kwa wanadamu lakini sio siri kwa Mungu maana anaiona na kuisitiri, anaifunika kwa muda huku akitafuta namna ya kuufikia moyo wako uachane na dhambi, muda huu wa kuisitiri dhambi yako Mungu anakunyanyulia watu wa kukuombea (waombaji) watakaobeba kwa mzigo shida yako.
Zakaria 3:1-10 “1 Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye. 2 Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni? 3 Basi, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu sana, naye alikuwa akisimama mbele ya malaika. 4 Naye huyo akajibu, akawaambia wale waliosimama mbele yake, akisema, Mvueni nguo hizi zenye uchafu. Kisha akamwambia yeye, Tazama, nimekuondolea uovu wako, nami nitakuvika mavazi ya thamani nyingi………………”
Matendo ya mtu kujihesabia haki mbele za Mungu ni mavazi machafu, damu ilisimama kumsitiri Yoshua mpaka hapoYoshua alipoondolewa dhambi yake. Kumbuka kusitiriwa dhambi ni kwa muda tu.
Kumbuka habari ya Yesu na Yule mwanamke aliyezini katika Biblia, Yohana 8:3-11 “3 Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati. 4 Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini. 5 Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje? 6 Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi. 7 Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe. 8 Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi. 9 Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati. 10 Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Je! Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia? 11 Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.”
Waandishi na Mafarisayo hawakujua kwamba zao zilikuwa zimesitiriwa kwaajili ya nafasi zao ili wapate muda wa kutengeneza na BWANA, na ndio maana walipomleta Yule mwanamke dhambi zao zikafunuliwa ndani yao na hakuna hata mmoja wao aliyebaki pale.

Usiwe kama Waandishi na Mafarisayo, Roho Mtakatifu akikushudia dhambi yako unayofanya kwa siri rudi kwa Yesu usikimbie mbali na Yesu.