Thursday, September 22, 2016

MAOMBI YA KUFUNGULIWA MACHO YA ROHONI

MAOMBI YA KUFUNGULIWA MACHO YA ROHONI
(Maombi haya yametoka Waefeso 1:17-23, 2:6)

Mungu wa Bwana wangu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, unipe mimi roho ya hekima na ya ufunuo katika kukujua wewe; macho ya moyo wangu yatiwe nuru, nijue tumaini la mwito wako jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wako kwangu mimi mtakatifu jinsi ulivyo; Nijue  ubora wa ukuu wa uweza wako ndani yangu mimi niaminie jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wako; ulioutenda katika Kristo ulipomfufua katika wafu, ukaniketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho. Ukamweka mkono wako wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; ukavitia vitu vyote chini ya miguu yake, ukamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo ndilo mwili wake.

Samson Mollel
Uzima wa Milele International Ministries +255 767 664 338
www.uzimawamileleministries.blogspot.com