Thursday, September 22, 2016

BARAKA NA LAANA HADI KIZAZI CHA NNE (Samson Mollel 0767 664 338)

BARAKA NA LAANA HADI KIZAZI CHA NNE
Samson Mollel 0767 664 338
Uzima wa Milele International Ministries (Yohana 17:3)

www.uzimawamileleministries.blogspot.com


UTANGULIZI


Baraka na laana ni maneno yanayotumiwa mara kwa mara na watumishi wengi wa Mungu nahii ni kwasababu katika maisha ya kiroho na kimwili kuna aina mbili tu za maisha ambazo ni maisha ya Baraka au maisha ya laana. Baraka maana yake ni kupata mema au mafanikio, Baraka ni neno linalobeba nguvu Fulani ya kufanya maneno ya heri yawe kweli au ni nguvu inayobeba mafanikio kutokana na kufuata maelekezo uliyopewa. Laana nayo ni nguvu inayobeba taabu na mateso kutokana na maneno yasiyo mema au kutokana na kutofuata maelekezo uliyopewa. Haijalishi umeokoka kiasi gani, unaweza kuwa umeokoka lakini bado ukaishi kwenye laana ambayo hukuisababisha wewe ilisababishwa na baba/babu zako (Kutoka 20:5 “……….nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,”).
Fahamu kwamba Baraka au laana inaweza kutolewa kwa kinywa cha Mungu au cha shetani kwa njia ya vinywa vya wanadamu na pia wanadamu wanaweza kutoa Baraka au laana kwa kumtaja Mungu au miungu yao.
Melkizedeki alimbariki Abramu kwa jina la Mungu aliye juu “Mwanzo 14:18-19 “18 Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana. 19 Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi.”
Ndugu za Rebeka walimbariki Rebeka Mwanzo 24:60 “Wakambarikia Rebeka, wakamwambia, Ndugu yetu, uwe wewe mama wa kumi elfu, mara elfu nyingi, na wazao wako waurithi mlango wa hao wawachukiao.”

BARAKA NA LAANA KUTOKA KWA MUNGU (JEHOVA)

Neno la Mungu limeshaweka wazi kabisa kuwa Baraka zinapatikana kwa njia gani na laana zinapatikana kwa njia gani kama tunavyosoma katika maandiko matakatifu.
Kumb 30:15-20 “15 Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya; 16 kwa hivi nikuagizavyo leo kumpenda Bwana, Mungu wako, kuenenda katika njia zake, na kushika maagizo yake, na amri zake, na hukumu zake, upate kuwa hai na kuongezeka; Bwana, Mungu wako, apate kukubarikia katika nchi uingiayo kuimiliki. 17 Lakini moyo wako ukikengeuka, usipotaka kusikiza, lakini ukavutwa kando kwenda kuabudu miungu mingine, na kuitumikia; 18 nawahubiri hivi leo hakika mtaangamia; hamtazifanya siku zenu kuwa nyingi juu ya nchi, uivukiayo Yordani, uingie kuimiliki. 19 Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; 20 kumpenda Bwana, Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wako, na wingi wa siku zako; upate kukaa katika nchi Bwana aliyowaapia baba zako, Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kuwa atawapa.”
Vilevile ukisoma kitabu cha Kumbukumbu la torati mlango wa 28 utaona maelekezo na maagizo aliyoyatoa Mungu ili kujipatia Baraka kutoka kwake na mambo ambayo mtu akifanya atapata laana; Kumb 28:1-2, 151 Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; 2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako…….. 15 Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.”
Kimsingi katika ulimwengu wa roho Mungu anaviona vizazi vyote katika sehemu moja, yaani katika ulimwengu wa roho hakuna umbali wa kutoka kizazi kimoja kwenda kizazi kingine na ndio maana Mungu alipombariki Adamu na sisi tulibarikiwa wote, Mwanzo 1:27-28 “27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. 28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.”
Lakini pia hata Adamu alipolaaniwa na sisi sote tulipokea hiyo laana kwakuwa tumezaliwa na Adamu, yaani tulikuwa katika viuno vyake nasisi tukapokea hiyo laana; Mwanzo 3:16- 16 “Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala. 17 Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; 18 michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; 19 kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.” Bada ya laana hii hata wewe ambaye haukuwepo wakati huo leo umerithi laana ambayo Adamu alipewa baada ya kuasi.

LAANA NA BARAKA INAVYOWEZA KUHAMA KUTOKA KIZAZI KWENDA KIZAZI

Kutoka 20:4-5 “4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. 5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,”
Mungu wetu (JEHOVA) ni Mungu mwenye wivu, yaani hataki kushirikiana vile vitu vinavyompa yeye utukufu na kiumbe au kitu chochote. Anapenda aabudiwe na kusifiwa na kutukuzwa YEYE peke yake tu na sio kumchanganya. Neno la Mungu linasema Mungu hashirikiani utukufu wake na mwingine yeyote (Isaya 42:8 “Mimi ni Bwana; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.”)
Inapotokea mtu hakufuata maagizo ya BWANA na kufanya ibada za miungu na kuacha kumwabudu Mungu pekee, basi mtu huyo au familia hiyo na vizazi vyake vyote vinaingia katika laana “…… kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao…………”

BARAKA KUTOKA KIZAZI KIMOJA KWENDA VIZAZI VINGINE

Katika kipengele hiki nataka ujifunze kwa habari ya Baraka inavyoweza kutoka kizazikimoja kwenda kizazi kingine hata kama hicho kizazi hakikufanya mema lakini zile Baraka zinawafuata tu.

Baraka za Mungu kwa Ibrahimu

Biblia inatuambia habari za Abramu (Ibrahimu) alipotoa sadaka (sehemu ya kumi) kwa Melkizedeki mfalme wa Salemu na Melkizedeki akambariki Abramu (Ibrahimu) “Mwanzo 14:18-19 “18 Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana. 19 Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi.”
Neno la Mungu linatufundisha kuwa Abramu (Ibrahimu) alibarikiwa na Melkizedeki ambaye ni kuhani wa Mungu aliye juu sana (JEHOVA) kwasababu alitoa sadaka kwake. Baada ya kutoa sadaka hiyo kuna jambo lilitokea ambalo halionekani vizuri pale katika kitabu cha Mwanzo ila tunaona kwa uzuri katika Agano Jipya kitabu cha Waebrania;
Waebrania 7:9-10 “9 Tena yaweza kusemwa ya kuwa, kwa njia ya Ibrahimu, hata Lawi apokeaye sehemu ya kumi alitoa sehemu ya kumi; 10 kwa maana alikuwa katika viuno vya baba yake, hapo Melkizedeki alipokutana naye.”
Fahamu kwamba Lawi anayetajwa ni uzao wa nne kutoka kwa Ibrahimu kwani Ibrahim alimzaa Isaka, Isaka akamzaa Yakobo, Yakobo akamzaa Lawi. Tunajifunza kwamba unapotoa sadaka wewe hata vitukuu wako walioko katika viuno vyako wanakuwa wametoa hiyo sadaka, na Baraka unazopata zinamfikia mpaka na kitukuu cha yaani zinafika mpaka kizazi cha nne.

Baraka za Mungu kwa Mfalme Daudi

Daudi ni mfalme aliyewakuwa na mahusiano mazuri na Mungu kuliko mfalme mwingine yeyote katika historia ya ulimwengu kiasi cha Mungu mwenyewe kuweka agano la chumvi na Daudi na kumuahidi kuwa ufalme utadumu milele katika uzao wake kama tunavyosoma katika 2Nyakati 13:5 “je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi?”; Vilevile Mungu alimuimarisha sana Daudi mbele ya maadui zake, tunasoma Zaburi 89:20-24 “20 Nimemwona Daudi, mtumishi wangu, Nimempaka mafuta yangu matakatifu. 21 Ambaye mkono wangu utakuwa thabiti kwake, Na mkono wangu utamtia nguvu. 22 Adui hatamwonea, Wala mwana wa uovu hatamtesa. 23 Bali nitawaponda watesi wake mbele yake, Nitawapiga wanaomchukia. 24 Uaminifu wangu na fadhili zangu atakuwa nazo, Na kwa jina langu pembe yake itatukuka.”
Kwasababu ya Mfalme Daudi kumpendeza sana Mungu, Mungu alimbariki na kumuahidi kuwa ufalme hautatoka katika uzao wake. Lakini alitokea mtoto wa Mfalme Daudi aliyeitwa Sulemani  ambaye aliziacha njia za BWANA na kuanza kufuata miungu mingine na kuiabudu.
1Wafalme 11:1-13 “1 Mfalme Sulemani akawapenda wanawake wengi wageni, pamoja na binti yake Farao, wanawake wa Wamoabi, na wa Waamoni, na wa Waedomi, na wa Wasidoni, na wa Wahiti, 2 na wa mataifa Bwana aliyowaambia wana wa Israeli, Msiingie kwao, wala wasiingie kwenu; kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu kuifuata miungu yao. Sulemani akaambatana nao kwa kuwapenda. 3 Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo. 4 Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake. 5 Kwa kuwa Sulemani akamfuata Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni na Milkomu, chukizo la Waamoni. 6 Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake. 7 Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni. 8 Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa nchi za kigeni, waliofukiza uvumba, wakawatolea miungu yao dhabihu. 9 Basi Bwana akamghadhibikia Sulemani kwa sababu moyo wake umegeuka, naye amemwacha Bwana, Mungu wa Israeli, aliyemtokea mara mbili, 10 akamwamuru katika habari ya jambo lilo hilo asifuate miungu mingine; lakini yeye hakuyashika aliyoyaamuru Bwana. 11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Sulemani, Kwa kuwa umefanya hayo, wala hukuyashika maagano yangu, na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme usiwe wako, nami nitampa mtumishi wako. 12 Walakini katika siku zako sitafanya haya, kwa ajili ya Daudi baba yako; nitaurarua utoke katika mkono wa mwana wako. 13 Lakini sitauondoa ufalme wote pia; nitampa mwana wako kabila moja, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu niliouchagua.”
Pamoja na mfalame Sulemani kumuasi Mungu, Mungu anamrehemu mafalme Sulemani na kuacha kumuadhibu kwasababu ya ahadi ambazo Mungu alizifanya na mfamle Daudi baba yake 1Wafalme 11:11-12 “11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Sulemani, Kwa kuwa umefanya hayo, wala hukuyashika maagano yangu, na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme usiwe wako, nami nitampa mtumishi wako. 12 Walakini katika siku zako sitafanya haya, kwa ajili ya Daudi baba yako; nitaurarua utoke katika mkono wa mwana wako”; lakini sio hivyo tu, hata katika adhabu ambayo Mungu ameitoa kwa mfalme Sulemani juu ya mtoto wa Mfalme Sulemani, adhabu hiyo imepunguzwa kidogo kwasababu ya mahusiano mazuri kati ya Mungu na Daudi 1Wafalme 11:13Lakini sitauondoa ufalme wote pia; nitampa mwana wako kabila moja, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu niliouchagua.
Pamoja na makosa yote aliyoyafanya mfalme Sulemani na kumkasirisha Mungu, bado tunaona Mungu anaacha kumuadhibu mfalme Sulemani kwaajili ya kumbukumbu nzuri za Baraka alizomuahidia mfalme Daudi.

LAANA KUTOKA KIZAZI KIMOJA KWENDA VIZAZI VINGINE

Katika kipengele hiki nataka ujifunze kwa habari ya laana inavyoweza kutoka kizazi kimoja kwenda kizazi kingine (Kibiblia) hata kama hicho kizazi hakikufanya jambo baya lakini ubaya uliofanywa na watangulizi wao unawafuata na kuwatesa.

Laana ya kutoisikiliza sauti ya BWANA

Neno la Mungu limeweka waziwazi kuwa ikiwa wewe haujaisikiliza sauti ya BWANA na kuyaacha maagizo ya BWANA basi utalaaniwa katika uzao wa tumbo lako, Kumbukumbu 28:15, 18 “15 Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata. 18 Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.” Imeandikwa kuwa dhambi/makosa utakayofanya, laana yake inageuzwa kwenda kwa uzao wa tumbo lako na sio kwako wewe uliyefanya kosa hilo. Sasa unaweza kuelewa kwanini inakubidi ushughulikie sana makosa na dhambi walizofanya baba/babu zako kuliko ulivyodhani hapo kabla kwani laana zinazoleta ugumu wa maisha sasa zilisababishwa na wazazi wako au watangulizi wako.

Laana zilizompata mtoto wa mfalme Sulemani

Mtoto wa mfalme Sulemani (Rehoboamu) alirithi laana kwa kosa alilolifanya baba yake (Sulemani), yaani inamaana kuwa laana aliyoipata Rehoboamu ilitokana na dhambi/maovu/makosa ambayo yeye hakuyafanya. Sulemani alijikuta akipokea sehemu ndogo ya urithi wa ufalme (yaani kabila ya Yuda pekee na mji wa Yerusalemu) kutoka kwa baba yake bila kujua kwamba ilikuwa ni laana kwa alistahili kuongoza kabila kumi na mbili.
1Wafalme 11:1-12 “……………. 6 Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake. 7 Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni. ………………. 9 Basi Bwana akamghadhibikia Sulemani kwa sababu moyo wake umegeuka, naye amemwacha Bwana, Mungu wa Israeli, aliyemtokea mara mbili, ………………. 11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Sulemani, Kwa kuwa umefanya hayo, wala hukuyashika maagano yangu, na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme usiwe wako, nami nitampa mtumishi wako. 12 Walakini katika siku zako sitafanya haya, kwa ajili ya Daudi baba yako; nitaurarua utoke katika mkono wa mwana wako.
Wakati Rehoboamu anakuwa mtu mzima ili aanze kumiliki kama mfalme katika nafasi ya baba yake (Mfalme Sulemani) yeye hakujua kuwa kwa dhambi na makosa ya baba yake na yeye amefanya hiyo dhambi na kuayabeba maovu na adhabu ya baba yake ijapokuwa hakutenda kosa lolote (Maombolezo 5:7 “Baba zetu walitenda dhambi hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao.”), hivyo Rehoboamu hakuomba toba na ile laana ikamkuta kama tuanavyosoma katika Neno la Mungu.
1Wafalme 12:18-20 “18 Ndipo mfalme Rehoboamu akampeleka Adoramu, aliyekuwa juu ya shokoa, nao Israeli wote wakampiga kwa mawe hata akafa. Mfalme Rehoboamu akafanya haraka kupanda katika gari, ili akimbilie Yerusalemu. 19 Hivyo Israeli wakaasi juu ya nyumba ya Daudi hata leo. 20 Ikawa, Israeli wote waliposikia ya kwamba Yeroboamu amerudi, wakapeleka watu wakamwita aje mkutanoni, wakamfanya mfalme juu ya Israeli wote; wala hapakuwa na mtu aliyeshikamana na nyumba ya Daudi, ila kabila ya Yuda peke yake.”
Hivyo laana aliyoinena BWANA juu ya mtoto wa Mfalme Sulemani (Rehoboamu) kwa dhambi ya baba yake ikatimia. Inawezekana hata wewe unaishi katika laana inayotokana na dhambi/maovu/makosa yaliyofanywa na wazazi au mababu zako na wewe hujui kwanini umekwama, omba toba na msamaha.

Laana zilizompata Gideoni

Gideoni aliishi katika maisha ya shida na dhiki na umasikini mkubwa hata kiasi cha kuona kwamba Mungu amewaacha lakini tatizo ni baba yake kuwa kuhani wa baali na madhabahu ya baali imejengwa katika kijiji/mji wao. Na kwasababu hiyo badala ya Gideoni kubarikiwa na Mungu na kupokea  ahadi za Mungu katika maisha yake, kwamba inafahamika kuanzia Mbinguni kuwa Gideoni ni shujaaa, anapendwa na Mungu nani tajiri japokuwa yeye Gideoni aliona hapendwi na Mungu na kwamba Mungu amemuacha napia yeye ni masikini kama tunavyoona Gideoni akiongea na Malaika wa Bwana.
Waamuzi 6:1-16 “1 Kisha wana wa Israeli walifanya yaliyo maovu mbele za macho ya Bwana; Bwana akawatia mikononi mwa Midiani muda wa miaka saba 2 Mkono wa Midiani ulikuwa na nguvu juu ya Israeli; tena kwa sababu ya Midiani wana wa Israeli walijifanyia hayo mashimo yaliyo milimani, na hayo mapango, na hizo ngome. ………………….. 7 Kisha ikawa, hapo wana wa Israeli walipomlilia Bwana kwa sababu ya Midiani, 8 Bwana akamtuma nabii aende kwa hao wana wa Israeli; naye akawaambia, Bwana, yeye Mungu wa Israeli, asema hivi, Mimi niliwaleta ninyi mkwee kutoka Misri, nikawatoa katika nyumba ya utumwa; …………. 11 Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani. 12 Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa. 13 Gideoni akamwambia, Ee Bwana wangu, ikiwa Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu, waliyotuhadithia baba zetu, wakisema, Je! Siye Bwana, aliyetuleta huku kutoka Misri? Ila sasa ametutupa, naye ametutia katika mikono ya Midiani. ………. 15 Akamwambia, Ee Bwana, nitawaokoa Israeli kwa jinsi gani? Tazama, jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase, na mimi ndimi niliye mdogo katika nyumba ya baba yangu. 16 Bwana akamwambia, Hakika nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kama mtu mmoja.”
Kumbe tatizo lililo kwamisha maisha ya Gideoni na kushindwa kuishi kama vile Mungu alivyompangia ni madhabahu ya baali katika eneo lile ambayo baba yake na Gideoni alikuwa ndiye kuhani wa madhabahu. Sasa unaweza kuona kuwa Gideoni hakuwa na uhusiano wa moja kwa moja na madhabahu ya baali ila baba yake ndiye aliyekuwa kuhania wa madhabahu na hali hiyo ikakwamisha maisha ya Gidioni mpaka alipoivunja ile madhabahu.
Waamuzi 6:25-31 25 Ikawa usiku uo huo Bwana akamwambia, Mtwae ng'ombe wa baba yako, yaani ng'ombe wa pili, wa miaka saba, ukaiangushe madhabahu ya Baali, aliyo nayo baba yako, ukaikate Ashera ile iliyo karibu nayo; 26 ukamjengee Bwana, Mungu wako, madhabahu juu ya ngome hii, kwa taratibu zake; ukamtwae yule ng'ombe wa pili na kumtoa awe sadaka ya kuteketezwa, kwa kuni za ile Ashera uliyoikata. 27 Ndipo Gideoni akatwaa watu kumi miongoni mwa watumishi wake, akafanya kama Bwana alivyomwambia; lakini ikawa kwa sababu aliwaogopa watu wa nyumba ya baba yake, na watu wa mji, hakuweza kuyatenda hayo wakati wa mchana, basi aliyatenda usiku. 28 Hata watu wa mji walipoondoka asubuhi na mapema, tazama, madhabahu ya Baali imebomolewa, na ile Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwa, na yule ng'ombe wa pili ametolewa sadaka juu ya ile madhabahu iliyojengwa. 29 Wakaambiana, Ni nani aliyetenda jambo hili? Hata walipotafuta habari na kuuliza, wakasema, Gideoni, mwana wa Yoashi, ndiye aliyetenda jambo hili. 30 Ndipo watu wa mji wakamwambia Yoashi Mlete mwanao, afe; kwa sababu ameibomoa madhabahu ya Baali na kwa sababu ameikata ile Ashera iliyokuwa karibu nayo. 31 Yoashi akawaambia watu wote waliokuwa wakishindana naye, Je! Mtamtetea Baali? Au mtamwokoa ninyi? Yeye atakayemtetea na auawe hivi asubuhi; kama yeye ni Mungu, na ajitetee nafsi yake, kwa sababu mtu mmoja ameibomoa madhabahu yake.
Baada ya Gidioni kugundua tatizo na kuvunja madhabahu ya baali na kumtumikia Mungu wa kweli tunaona mambo yanabadilika na maisha ya Gidioni yanakuwa mazuri na Israeli wanaondoka katika mikono ya Wamidiani na kuishi kwa amani kama tunavyosoma katika Waamuzi 8:28 “Hivyo Midiani walishindwa mbele ya wana wa Israeli, wala hawakuinua vichwa vyao tena. Nayo nchi ilipata kuwa na amani muda wa miaka arobaini katika siku za Gideoni.”

Laana zilizompata Kaanani kwa kosa la baba yake, Hamu.

Neno la Mungu linatufundisha kuwa baada ya gharika kipindi Nuhu, Nuhu alikuwa mkulima mzuri na alilima zabibu na kutengeneza divai akalewa akawa uchi, akiwa uchi mtoto wake Hamu (Baba yake Kaanani) akamuona uchi wake lakini hakumfunika akaenda kuwaambia ndugu zake (Shemu na Yafethi) na hao ndugu zake ndio walio kuja kumsitiri baba yao (Nuhu). Mwanzo 9:20-23 “20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu; 21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake. 22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje. 23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
Jambo alilolifanya Hamu lilimuudhi sana baba yake “yaani Nuhu”, hivyo Nuhu akatamka laana; Mwanzo 9:24-27 “24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea. 25 Akasema,Na alaaniwe Kaanani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake. 26 Akasema,Na atukuzwe Bwana,Mungu wa Shemu;Na kaanani awe mtumwa wake. 27 Mungu akamnafisishe Yafethi,Na akae katika hema za Shemu; Na kaanani awe mtumwa wake.” Jambo la kushangaza hapa ni kwamba kwanini laana haikutamkwa kwa Hamu aliyefanya kosa? Tunachokiona hapa ni kwamba laana zinamuendea Kaanani mtoto wa Hamu ambaye hakuhusika na kosa hilo. Hivi ndivyo laana zilizotamkwa na watu kwa wazazi wako zilivyokufikia hata kama hukushiriki katika kufanya jambo hilo.

FAHAMU KWAMBA YESU ALICHUKUA LAANA ZETU

Neno la Mungu linasema katika waraka wa mtume Paulo kwa Wagalatia 3:13-14, 29 “13 Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti; 14 ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani……..29 Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.”
Wakati mwingine katika maisha ya ukristo, wakristo wamekuwa wakiishi maisha yenye taabu na mateso mengi kutokana na laana ambazo wamerithi kutoka kwa wazazi/mababu na mabibi/wahenga (vizazi vya zamani sana). Hata wewe unayesoma sasa; hebu jaribu kurudi nyuma miaka 150 hadi 200, mababu zako wote walikua waabudu miungu (walimwabudu shetani) nasema hivyo kwani ukristo uliingia Afrika na Tanzania kati ya miaka 100 – 150 iliyopita na kabla ya hapo babu zetu walimwabudu shetani (kupitia mizimu). Kama ndivyo basi kuna laana ambayo ilisababishwa na mababu zetu nasi tumeirithi hiyo laana na inaleta madhara makubwa katika maisha yetu kama madhara yaliyompata Gideoni na Rehoboamu kama tulivyojifunza hapo awali.
Lakini unapompokea Yesu Kristo yeye anayabeba maovu na makosa yetu ambayo yalisababisha laana katika maisha yetu na sisi tunapokea uponyaji wa laana zote sawa na Neno la Mungu kutoka Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”
Ni ukweli kwamba baba zetu walitenda dhambi na sisi tumerithishwa maovu yao (Maombolezo 5:7 “Baba zetu walitenda dhambi hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao.”) lakini ni ukweli kwamba baada ya kifo cha Yesu dhambi zetu zote zimefutwa kwa damu ya Yesu na hakuna laana yoyote tena inayoweza kukushinda, wewe unapaswa kuamini kuwa damu ya Yesu inaweza kukuosha uovu wote.


MAOMBI

1.      Omba toba kwa dhambi na maovu na makosa waliyofanya wazazi na mababu (Soma Zaburi 51 na Daniel 9:1-11
2.      Fanya ukiri wa nguvu ya damu ya Yesu katika kukusafisha dhambi, maovu, makosa na laana zote (Soma Isaya 1:18, Waebrania 12:24, Isaya 53:5, Wagalatia 3:13)
3.      Kwa jina la Yesu kata laana zote ulizosababisha mwenyewe, ulizorithishwa na wazazi/mababu au ulizorushiwa na mawakala wa shetani, achilia damu ya Yesu kufuta historia mbaya zote zilizoandikwa kuzimu ili kukufuatilia (Soma Ufunuo 12:11)
4.      Mshukuru Mungu kwa kukuhamisha kutoka katika laana na kukuingiza katika Baraka na katika Nuru yake (Soma Wagalatia 3:-29, Wakolosai 1:12-14)

1 comment:

Jasmine said...

Nashkuru kwa MAFUNDISHO. Hakika nimejifunza mengi juu ya LAANA NA BARAKA zinazoeza kwenda mpaka kizazi cha 4