Friday, August 12, 2016

KONGAMANO LA MAOMBI YA KITAIFA 2016 KUOMBEA NCHI YA TANZANIA MAHALI:CHUO KIKUU CHA DODOMA (2ND – 6TH August, 2016) Mwl. Chistopher & Diana Mwakasege Imeandikwa na Samson Mollel (www.uzimawamileleministries.com)

SIKU YA PILI.............................

KUOMBA MBINGU ZIWE WAZI KWAAJILI YA KUSIMAMISHA KUSUDI LA MUNGU KATIKA NCHI

Isaya 66:1 “Bwana asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?”

Isaya 48:12-13 “12 Nisikilize mimi, Ee Yakobo; na Israeli, niliyekuita; mimi ndiye. Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho pia. 13 Naam, mkono wangu umeuweka msingi wa dunia, na mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo husimama pamoja.”

Mbingu na nchi zina wito na Mungu anaziita husimama pamoja, na kati ya wito mmojawapo wa mbingu ni mbingu kuwa kiti cha enzi, kiti maana yake nafasi inayotumika kwaajili ya kutawala na kumiliki, kwahiyo kazi mojawapo ambayo Mungu aliamua mbingu zitumike ni kuwa kiti cha chake enzi, anapotaka kutawala dunia na vitu vyote vilivyopo chini ya mbingu anatumia mbingu kama kiti chake cha enzi. Pamoja na kuwa mbingu na nchi zina wito maalum kwa Mungu, Yakobo (Israel) ameitwa. Mungu anapomuita mtu anaita na Mbingu anaita na nchi kwa wakati mmoja, Mungu akiita nchi uwe na uhakika Mbingi zinaitika na akiita Mbingu nchi inaitika, kwahiyo ameweka mbingu na chi ili zifanye kazi kwa pamoja na kwa karibu ili kulitimiza kusudi la Mungu.

Mathayo 3:16-17 “16 Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake; 17 na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.”

Marko 1:10-11 “10 Mara alipopanda kutoka majini, akaona mbingu zinapasuka, na Roho, kama hua, akishuka juu yake; 11 na sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.”

Luka 3:21-22 “21 Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka; 22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.”

Hawa waandishi wamendika jambo moja kwa utofauti na sio kimakosa, Roho Mtakatifu anataka tuone kuhusika kwa mbingu na maisha ya watu na maisha ya nchi. Luka 3:21-22, inazungumzia juu ya hali ya mbingu ilikuwa ngumu ilikuwa imefungwa ndio maana ametumia neno kupasuka, mbingu kumfunukia ni kwaajili yake binafsi ndio maana si kila aliyebatizwa mbingu zilimfunukia, mbingu kufunuka ni “for general purpose” kwa ujumla, maana yake zilifunuka kwaajili ya watu wengine ili kutumia kilichopo ndani yake.

Ayubu 38:33 “Je! Unazijua amri zilizoamuriwa mbingu? Waweza kuyathibitisha mamlaka yake juu ya dunia?”

Zaburi 19:1 “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake.”

Zaburi 50:6 “Na mbingu zitatangaza haki yake, Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu.”

Utagundua kwamba waandishi wa vitabu 3 vya injili (Mathayo, Marko na Luka) walipokuwa wanaandika habari za mbingu, Roho alishuka kiasi cha kwamba Yohana aliweza kumtambua jinsi alivyokuja na maneno yale aliyosema Baba hayakuwa kwaajili ya Yesu kwani hata kama asingesema Yesu alifahamu kuwa Baba anampenda, maneno yale yalisemwa kwaajili yetu, kuna kitu kilikuwa kinaachiliwa

Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.”
Kama tulivyojifunza kuwa mbingu ni kiti cha enzi, unaweza kuusoma mstari huu kwa jinsi hii “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya kiti cha enzi.” Kiti cha enzi ni nafasi ambayo Mungu anayo ya kutawala na kumiliki ambayo ameamua kuiweka katika mbingu ili kutawala mambo yote yaliyoko chini ya mbingu ili kutawala na kuyaratibu katika utaratibu na msingi ambao Mungu amekusudia

Matendo 17:26-28 “26 Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao; 27 ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.”

Habakuki 2:1-4 “1 Mimi nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara, nitaangalia ili nione atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu katika habari ya kulalamika kwangu. 2 Bwana akanijibu, akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma kama maji. 3 Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia. 4 Tazama, roho yake hujivuna, haina unyofu ndani yake; lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake.”

Kati ya vitu vilivyopo ndani ya mbingu ambavyo ni muhimu sana kuachiliwa kwaajili ya nchi na kikae sawasawa

Amri zilizoamriwa mbinguni, amri haizungumzii juu ya sheria inatokana na “ordinances” neno linalotokana na “order” yaani utaratibu; kwahiyo utaratibu wa mambo yaliyopo duniani upo kwenye mbingu, maana yake kile kilichopangiwa kwaajili yako wewe binafsi (by order) kwa utaratibu wa kimbingu kimefichwa katika mbingu. Mbingu zikifungwa juu yako huwezi kujua taratibu za Mungu kwenye maisha yako; mbingu zikifungwa juu ya nchi, nchi itakuwepo lakini haiwezi kwenda kwenye “order”, kama mbingu zimefungwa kwenye familia yako utaishi lakini sio kwa “order” au kwa hatua za Mungu, kama mbingu zimefungwa juu ya huduma yako uwe na uhakika utabahatisha, utaiga, utatafuta msaada kwa watu wengine lakini hutajua kutembea kwa ujasiri kwenye hatua za BWANA kwasababu mbingu zikifungwa, amri zilizoamriwa mbingu kwaajili vitu vilivyopo hapa hazitoki, hazionekani, hazifamiki, hazijulikani, zimefichwa kwenye mbingu. Na ndio maana ni muhimu sana hata watu waliookoka kuhakikisha kuwa Yesu ni Bwana, sio kwamba ni BWANA tu lakini ni mfalme, kwasababu ukishakubali namna hiyo unampa Mungu nafasi ya kuketi kwenye nafasi yake ya kuongoza hatua, Mungu kama amekuumba akakuleta Duniani ameshatayarisha kila hatua, suala la hatua alilokupangia kwaajili ya kufanikisha halina majadiliano; hii ni kwasababu Mungu ametupa kuchagua na majibu ya uchaguzi wetu ametupa pia kwamba kama ukichagua jambo Fulani matokeo yake ni haya na kama ukichagua jambo jingine matokeo yake ni haya, basi sasa hakuna haja ya kuchagua kwakuwa matokeo yote tayari unayo. Yaani ni sawasawa na asingekupa uchaguzi ulio mbaya na akakupa uchaguzi ulio mzuri na kakaupa na tiki. Kwa lugha nyingine hauna uchaguzi kwakuwa lile jambo sahihi tayari umepewa.

Biblia inasema “Mbingu zikamfunukia”; inamaanisha Mungu alikuwa anafungua order aliyokuwa amekusudia kwaajili ya Yesu, ndio maana Yesu ana miaka 33 lakini huoni vitu vingi vimerekodiwa, hivyo unavyoona ni baada ya mbingu kumfunukia Yesu kabla ya hapo mbingu zilikuwa zimefungwa na baada ya mbingu kumfunukia vikaandikwa maana vilikuwa kwenye order. Kabla mbingu hazijamfunukia hakujua amri zilizoamrikwa na kiti cha enzi kwaajili yake. Lakini kwasababu kuja kwa Yesu duniani kulikuwa kunafungua kurasa si kwasababu tu ya kuja kwa Yesu duniani lakini kwasababu ya watu wengine wanaotaka kuingia kwenye order kwahiyo mbingu zilifunuka “for general use”

Zaburi 16:1 “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake.”
Utukufu kazi yake ni kutengeneza mazingira ya kiroho yanayoruhusu kufanya na kusimamia kusudi la Mungu katikati ya wanadamu kwa uhuru anaotaka “spiritual atmosphere”, ndio maana wale makuhani walipokuwa wanaimba kwa Mungu kuja ndani ya hekalu, walijua amekuja kwasababu utukufu ulibadilisha hali ya mazingira/hali ya uhusiano wako na Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu pamoja na kwamba amekuja kwaajili ya kila mtu, utukufu wa BWANA ukifunguliwa utajua kabisa kuna upako wako binafsi na upako wa kijumla. Ndio maana haijalishi unasali kanisa gani jambo la Muhimu ni kuhakikisha mbingu zinzfunguka kwaajili yako na utamsikia Mungu akisema “Wewe ni mwangu mpendwa nimependezwa na wewe” na hakuna mtu anaweza akakunyang’anya hicho kwasabu mbingu zinaachilia haki, zinaachilia utukufu. Biblia inasema mbingu zinatangaza haki yako, huwezi kupoteza haki kwasababu Mungu ndiye mwenye kukuhesabia haki, usifikiri mazingira hayatakuwepo ya kutafuta namna ya kukunyang’anya haki yako, yatatokea mengi tu yatakusumbua lakini ukishajua kwamba mbingu zimekufunukia (sio kwamba zimefunuka tu kwa kila mtu) unajua kuna za kwako, wanaweza wakanyimwa wengine lakini wewe utapata kwasababu unajua.

Kutoka 12:2 “Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu; utakuwa ni mwezi wa kwanza wa mwaka kwenu.”

Kwa miaka mia nne mbingu zilifungwa kwa wana wa Israeli, hapo ndipo mbingu zilipowafunukia wana Israeli. Unapoona watu wanaishi kama jana ni kwasababu wamepoteza saa zao, wamepoteza order ujue mbingu zimefungwa.

Mafanikio ya nchi ya Tanzania zipo kwenye mbingu zilizoamriwa kwaajili ya Tanzania, ni kazi yetu sisi kama waombaji kwenda mbele za Mungu kuomba mbingu zifunguke kwaajili ya nchi, na zikifunguka kwaajili ya nchi uwe na hakika mbingu zinawasiliana na ardhi iliyoko Tanzania na ghafla kunakuweko namabadiliko Fulani kwasababu haitaachilia tu amri, lazima ikutengenezee na mazingira ambayo itakuwa rahisi kwako kutekeleza zile amri ambazo umewekewa na Mungu.

Daniel 4:26 “Na kwa kuwa waliamuru kukiacha kisiki cha shina lake; ufalme wako utakuwa imara kwako, baada ya wewe kujua ya kuwa mbingu ndizo zinazotawala.”

Kazi yako, biashara, huduma, familia, kanisa litakuwa imara kwako hapo utakapojua yakuwa mbingu ndizo zinaweka order na pale utakapokubali kukaa chini ya kiti cha Mungu, ndio maana shetani akikuvuruga kwenye mbingu amekuvuruga mahali pabaya, akisababisha mbingu zikafungwa amekubania vitu vingi.

Uwe makini na mafundisho unayopokea/unayosikia kwakuwa imani huja kwa kusikia na inategemea unasikia nini. Kuna watu wengine wanazo mbingu 4 wengine 7, hao ni wale waliojaribu kushindana na kiti cha enzi cha Mungu na kila katika kila mbingu wanaweka pepo. Biblia inazungumza kuwa zipo mbingu tatu tu (2Wakorintho 12:1-51 Sina budi kujisifu, ijapokuwa haipendezi; lakini nitafikilia maono na mafunuo ya Bwana. 2 Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu. 3 Nami namjua mtu huyo, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua); 4 ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi, akasikia maneno yasiyotamkika, ambayo haijuzu mwanadamu ayanene. 5 Kwa habari za mtu kama huyo nitajisifu; lakini kwa ajili ya nafsi yangu sitajisifu, isipokuwa katika habari ya udhaifu wangu.”)



KONGAMANO LA MAOMBI YA KITAIFA 2016 KUOMBEA NCHI YA TANZANIA MAHALI:CHUO KIKUU CHA DODOMA (2ND – 6TH August, 2016) Mwl. Chistopher & Diana Mwakasege Imeandikwa na Samson Mollel (www.uzimawamileleministries.com)

SIKU YA PILI

MAENEO YA KUOMBEA YALIYO NDANI YA MBINGU ILI YASITUMIKE KUVURUGA NCHI

        i.            Mbingu kama kiti cha enzi

Isaya 66:1 “Bwana asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?”

     ii.            Hekima zilizo katika mbingu

Zaburi 136:5 “5 Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.” Ukisoma kwa tasfsiri ya kiingereza inasema “To him that by wisdom made the heavens: for his mercy endureth for ever - KJV.” Neno fahamu zake linasimama badala ya hekima, kuna hekima zilizowekwa katika mbingu

   iii.            Mbingu kama mtoa Amri

Ayubu 38:33 “Je! Unazijua amri zilizoamuriwa mbingu? Waweza kuyathibitisha mamlaka yake juu ya dunia?”

   iv.            Mbingu kama Mahakama

Daniel 7:9-10 “9 Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mzee wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao. 10 Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.”
Zaburi 50:3-6 “3 Mungu wetu atakuja wala hatanyamaza, Moto utakula mbele zake, na tufani yavuma sana ikimzunguka pande zote. 4 Ataziita mbingu zilizo juu, Na nchi pia awahukumu watu wake. 5 Nikusanyieni wacha Mungu wangu Waliofanya agano nami kwa dhabihu. 6 Na mbingu zitatangaza haki yake, Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu.”

      v.            Viapo katika mbingu

Mathayo 5:33-35 “33 Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako; 34 lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu; 35 wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu.”
Hesabu 30:2 “Mtu atakapomwekea Bwana nadhiri, au, atakapoapa kiapo ili kufunga nafsi yake kwa kifungo, asilitangue neno lake; atafanya sawasawa na hayo yote yamtokayo kinywani mwake.”

   vi.            Wito wa mbingu

Zaburi 19:1 “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake.”
Utukufu maana yake ni Mungu kujidhihirisha kwa namna ambayo inajulikana katika mwili yakwamba Mungu yuko upande wako (Yohana 1:14 “Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.”). Utukufu wa Mungu unaweza kupungua (Rumi 3:23 “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;”)
Fahamu kwamba shetani anapoamua kuvuruga haki yako anavuruga kwenye Mbingu

MBINGU KAMA KITI CHA ENZI

Kuna tofauti kati ya Mbinguni na mbingu. Ukisoma Mwanzo 1:1,7-8 “1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. 7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo. 8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.”

Isaya 66:1 “Bwana asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?”

Dhambi ilipotokea shetani alichukua umiliki wa nafasi ya kiti cha enzi alichopewa mwanadamu, ndio maana Mungu alipomuangalia Adamu baada ya anguko pale Eden hakumuona kwenye nafasi yake (Mwanzo 3:9 “Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi?”)

Daniel 4:24-26 “24 tafsiri yake ni hii, Ee mfalme, nayo ni amri yake Aliye juu, iliyomjia bwana wangu, mfalme; 25 ya kuwa utafukuzwa mbali na wanadamu, na makao yako yatakuwa pamoja na wanyama wa kondeni, nawe utalazimishwa kula majani kama ng'ombe, nawe utatiwa maji kwa umande wa mbinguni, na nyakati saba zitapita juu yako; hata utakapojua ya kuwa Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa yeye amtakaye, awaye yote. 26 Na kwa kuwa waliamuru kukiacha kisiki cha shina lake; ufalme wako utakuwa imara kwako, baada ya wewe kujua ya kuwa mbingu ndizo zinazotawala.”

Anaposoma shetani hilo Neno “baada ya wewe kujua ya kuwa mbingu ndizo zinazotawala.” Hahitaji kwenda mbinguni ili kufunga Baraka zako, anachohitajio ni kukamata mbingu na hapo anakuwa amekumaliza kabisa.

Isaya 33:22 “Kwa maana Bwana ndiye mwamuzi wetu; Bwana ndiye mfanya sheria wetu; Bwana ndiye mfalme wetu; ndiye atakayetuokoa.”

Mungu kuwa mwamuzi maana yake ni kuwa Mahakama, na Mungu kuwa Mfanya sheria maana yake ni kuwa Bunge la nchi na pia kuwa Mfalme wetu maana yake ni Mungu kuwa Raisi wan chi. Maana yake ni kwamba Mungu anataka mihimili ya nchi ili aweze kumiliki. Vilevile Mungu ndiye msimamizi wa uchaguzi katika nchi (Mithali 16:33 “Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za Bwana.”)

Kama nchi ukitaka kuimarisha/kuusimamisha uchumi ni mfumo wa ufalme/utawala. Ndio maana Neno la Mungu linasema katika Mathayo 6:31-33 “31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? 32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. 33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.” Kwahiyo sio kumtafuta Yesu peke yake bali tafuta haki ya ufalme iliyopotea katikakti ya wanadamu (Mfumo), na uchumi wako utakuwa sawa.

Mtu akikorofisha mfumo mlinzi kutoka mbinguni (Waombaji) anaweka pingu kwenye kiti kama ilivyokuwa kwa mfalme Nebukadreza.

KONGAMANO LA MAOMBI YA KITAIFA 2016 KUOMBEA NCHI YA TANZANIA MAHALI:CHUO KIKUU CHA DODOMA (2ND – 6TH August, 2016) Mwl. Chistopher & Diana Mwakasege Imeandikwa na Samson Mollel (www.uzimawamileleministries.com)

SIKU YA KWANZA

HASARA INAYOWEZA KUTOKEA MUNGU ANAPOKOSA KUMPATA MTU WA KUOMBEA NCHI KWA JINSI MUNGU ANAVYOTAKA IOMBEWE

Ezekiel 22:30 “Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu.”

Kwanini Mungu atafute mtu wakati Biblia inatuambia kuwa Mungu anaona kila mahali?

Zaburi 139:7-12 “7 Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako? 8 Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko. 9 Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari; 10 Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika. 11 Kama nikisema, Hakika giza litanifunika, Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku; 12 Giza nalo halikufichi kitu, Bali usiku huangaza kama mchana; Giza na mwanga kwako ni sawasawa.”

Kama Mungu anaona kila kitu kila mahali na anasema akatafuta mtu lakini hakuona mtu; basi itakuwa ni zaidi ya kutafuta ya kawaida tunayoifahamu, yaani katika maneno kutafuta yapo mambo (kuna kitu) yamejificha ndani yake. Utaona katika Biblia Mungu anaongea habari ya kutafuta waliopotea, kutafuta watendakazi (mtu anweza kuwa mtumishi wa Mungu lakini sio mtenda kazi, Mungu kupata watumishi sio jambo gumu ila kupata watenda kazi sio jambo rahisi)

Wanaoombea nchi wengi wanaombea nchi bila kujua nafasi zao katika hayo maombi ili Mungu naye afanye nafasi yake.

Mwanzo 3:9 “Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi?”

Mungu anamuita Adamu na kumuuliza yuko wapi wakati alikuwa anazungumza naye. Kitu cha kwanza kilichoharibika dhambi ilipoingia ni nafasi ya mtu aliyopewa na Mungu

Ø  Utaratibu wa ki-Mungu ni kwamba, Mungu anakupa nafasi kisha anatengeneza mahusiano

Ø  Ukitaka Mungu akupe unachokiomba tafuta kwanza nafasi ndipo utengeneze mahusiano, watu wengi wanaomba bila kujali nafasi

Kabla dhambi haijaingia hapakuwa na maombi kulikuwa na ushirika (fellowship). Ukitaka kumualika Mungu katika nafasi fulani lazima ujue mamlaka ya nafasi hiyo

Dhambi sio kwamba ilitutoa kwenye nafasi tu, lakini pia ilituharibu kiasi kwamba ukitaka kurudi kwenye nafasi lazima utengeneze kwanza

Daniel 17:17-21 “17 Basi, kwa habari za hao vijana wanne, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekima; Danieli naye alikuwa na ufahamu katika maono yote, na ndoto. 18 Hata mwisho wa siku zile alizoziagiza mfalme za kuwaingiza, mkuu wa matowashi akawaingiza mbele ya mfalme Nebukadreza. 19 Naye mfalme akazungumza nao; na miongoni mwao wote hawakuonekana waliokuwa kama Danieli, na Hanania, na Mishaeli, na Azaria; kwa hiyo wakasimama mbele ya mfalme. 20 Na katika kila jambo la hekima na ufahamu alilowauliza mfalme, akawaona kuwa walifaa mara kumi zaidi ya waganga na wachawi waliokuwa katika ufalme wake. 21 Tena, Danieli huyo akadumu huko hata mwaka wa kwanza wa mfalme Koreshi.”

Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria walipewa maarifa ya kila namna na Mungu. Ni kwanini Ashpenazi (Mkuu wa matowashi) alichukua vijana wengi wakati mfalme alikuwa anahitaji watu wanne tu? Nikama kujiuliza ni kwanini serikali isomeshe wanafunzi wengi chuo kikuu wakati inahitaji wachache tu kuwaajiri katika fani wanazowasomesha

Ezekiel 22:30-31 “30 Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu. 31 Kwa sababu hiyo nimemwaga ghadhabu yangu juu yao; nimewateketeza kwa moto wa hasira yangu; nami nimeileta njia yao wenyewe juu ya vichwa vyao, asema Bwana MUNGU.”

Unapotaka kutengeneza chombo Fulani lazima umpate fundi sahihi wa kutengeneza chombo hicho.  Mfano huwezi kumchukua fundi wa gari atengeneze ndege, ndege inapoharibika inabidi utafute fundi wa ndege aitengeneze. Au mtu anapoumwa anahitaji daktari sahihi na vifaa sahihi ndio maana mtu anaweza kuumwa akapelekwa India kuwafuata wataalam sahihi.
Kwa kusema hayo inamaana ya kwamba Mungu anatafuta waombaji, sio tu waombe kwaajili ya uharibifu uliotokea lakini kutengeneza mahali palipoharibika (Kwamfano ni kazi ya daktari kushona mguu wako ukipata ajali, lakini ni kazi ya polisi aliyesababisha ajali)
Kipimo kwamba boma limetengenezwa ni kuona limekamilika (Mfano kama ulipeleka gari kwa fundi kwasababu ya ubovu Fulani, lishishatengenezwa utaangalia kama lile tatizo limeisha)

Zaburi 106: 26, 23 “26 Ndipo alipowainulia mkono wake, Ya kuwa atawaangamiza jangwani, 23 Akasema ya kuwa atawaangamiza Kama Musa, mteule wake, asingalisimama, Mbele zake kama mahali palipobomoka, Ili aigeuze hasira yake asije akawaharibu.”

Musa alisimama mahali palipobomoka na kulitengeza boma, na kuiepusha hasira ya Mungu juu ya wana wa Israeli (Kutoka 32)

Mwanzo 18:17-33 “17 Bwana akanena, Je! Nimfiche Ibrahimu jambo nilifanyalo,…….. 20 Bwana akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana, 21 basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua. …………. 23 Ibrahimu akakaribia, akasema, Je! Utaharibu mwenye haki pamoja na mwovu? 24 Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu, wala hutauacha mji kwa ajili ya hao hamsini wenye haki waliomo? .....................26 Bwana akasema, Nikiona katika Sodoma wenye haki hamsini mjini, nitapaacha mahali pote kwa ajili yao……………. 28 Huenda wakapunguka watano katika wale hamsini wenye haki, je! Utaharibu mji wote kwa kupungua watano? Akasema, Sitauharibu, nikiona humo arobaini na watano. 29 Akazidi tena kusema naye, akinena, Huenda wakaonekana humo arobaini? Akasema, Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini. 30 Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema, Huenda wakaonekana huko thelathini? Akasema, Sitafanya, nikiona humo thelathini. 31 Akasema, Tazama, nimeshika kusema na Bwana, huenda wakaonekana huko ishirini? Akasema, Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini. 32 Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema mara hii tu, Huenda wakaonekana huko kumi? Akasema, Sitaharibu kwa ajili ya hao kumi. 33 Basi Bwana alipokwisha kuzungumza na Ibrahimu, akaenda zake; Ibrahimu naye akarudi mahali pake”

Ibrahimu alishindwa kusimama mahali palipobomoka na hivyo mji ule na watu wake ukaangamizwa.

Mungu hawezi kuwapita wakina Musa na Ibrahimu bila kuwaambia anachotaka kufanya. (Yeremia 5:1 “Pigeni mbio huku na huku katika njia za Yerusalemu, mkaone sasa, na kujua, na kutafuta katika viwanja vyake, kwamba mwaweza kumpata mtu mmoja, kwamba yuko mtu mmoja awaye yote atendaye kwa haki, atafutaye uaminifu; nami nitausamehe mji huo.”)

Isaya 62:6-7 “6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha Bwana, msiwe na kimya; 7 wala msimwache akae kimya, mpaka atakapoufanya imara Yerusalemu, na kuufanya kuwa sifa duniani.”

Je? Ni mlinzi wa namna gani? Ni mwombaji aliye mlinzi ambaye yupo tayari kubeba mzigo wa Mungu aliowekewa kwaajili ya Mji au Nchi, kwasababu BWANA mwenyewe ameahidi tusikae kimya (Isaya 58:2 “Walakini wanitafuta kila siku; hupenda kujua njia zangu; kama vile taifa waliotenda haki, wasioacha sheria ya Mungu wao, hutaka kwangu amri za haki; hufurahi kumkaribia Mungu.”).

  •         Huwezi kuwa mlinzi juu ya mji kama hauna mzigo wa kuuombea mji huo
  • ü    Lazima ujue maono/sababu ya Mungu kuufanya mji huo
  • ü  Usiende mbele za Mungu kwa kulalamika kwani Mungu atajibu malalamiko yako na sio sababu za kulalamika kwako (Habakuki 1 & 2)
  • ü  Tangu anguko la mwanadamu ni sheria katika ulimwengu wa roho kumkumbusha Mungu
  • ü  Unapotaka kuombea taifa/nchi lazima ujue maono (vision) ya eneo unalotaka kuliombea

Nchi/ardhi ikipata shida kunakuwa na shida ya mvua/Ukame, tauni (magonjwa).

MAOMBI YA KUOMBEA NCHI YA TANZANIA
2Nyakati 7:13-15 “13 Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; 14 ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao. 15 Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa.”