Thursday, July 23, 2015

PIGO LITOKANALO NA MANENO YA KUNENEWA/KUTAMKIWA (Samson Mollel - Uzima wa Milele International Ministries)

YALIYOMO


NENO NI NINI?

Neno ni matamshi yenye maana yanayotoka kwenye kinywa cha mtu au kiumbe.
Kibiblia neno ni yale mambo yaliyojaza moyo wa mtu, ukisoma injili ya Luka 6:45
Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.

NENO LA MUNGU
Neno la Mungu ni lile neno linalotoka kwa Mungu, Neno la Mungu ni Mungu mwenyewe hivyo si la kulifanyia mzaha. Yohana 1:1 Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Kwa hiyo neno la Mungu ndilo kweli na limejaa imani hata ya kuumba/kufanya yasiyokuwepo yakawepo. Kama tusomavyo katika Waebrania 11: 3 Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri.

NENO LA MUNGU LINATIMIZA MAPENZI YA MUNGU

Tangu mwanzo Mungu Baba ameliweka Neno lake kama mwongozo wa utimilifu wa kusudi lake ambalo msingi wake ni kulitimiza Neno lake. Tunasoma katika Yeremiah 1:12…… kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize. Yapo mambo mengi ambayo katika hayo Mungu ulitimiza neno lake katika kutupatia ushindi kwa maisha yetu ya hapa duniani. Mfano, Zaburi 107:20….. Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao.

Hivyo neno likitoka katika kinywa cha Mungu haliwezi kumrudia bure, bali lazima litimiza mapenzi yake.  Isaya 55:10 – 11 Maana kama vile mvua ishukavyo, na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; bali huinywesha ardhi, na kuizalisha na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma

Katika kitabu cha Isaya tumeona ya kuwa Neno la Mungu linatimiza Mapezi ya Mungu, na ukisoma Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.” Biblia inasema mawazo ya Mungu ni ya Amani. Kwa mistari hiyo katika kitabu cha Isaya na Yeremia tunamuona Mungu ambaye analiangalia Neno lake ambalo ni la Amani kwa watu wake ili alitimize.

SHETANI NAYE NI MUNGU

Baada ya kuona ya kwamba Neno la Mungu litatimiza mapenzi ya Amani; kumbuka kilichomfanya shetani kutupwa duniani ni ile hali ya kujiinua na kutaka nafasi ya Mungu, yaani alitaka awe kama Mungu alivyo (Isaya 14:12 – 17)Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa! 13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. 14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu. 15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo. 16 Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme; 17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?” Vilevile habari hii tunaisoma katika kitabu cha nabii Ezekieli 28:14 – 18; 14 “Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto. 15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako. 16 Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa Mungu, kama kitu kilicho najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto. 17 Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya mwangaza wako; nimekutupa chini, nimekulaza mbele ya wafalme, wapate kukutazama. 18 Kwa wingi wa maovu yako, katika uovu wa uchuuzi wako, umepatia unajisi patakatifu pako; basi nimetokeza moto kutoka ndani yako, nao umekuteketeza, nami nimekufanya kuwa majivu juu ya nchi, machoni pa watu wote wakutazamao”. Baada ya kushindwa kwa mpango huo na kuangushwa na Malaika Mikaeli tunasoma katika Biblia kwamba shetani ameitwa Mungu wa dunia hii 2Kor 4:4 4 “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.
Kutokana na maelezo katika mistari tuliyoisoma hapo juu tunaona kuwa shetani alitafuta cheo cha Mungu na kushindwa, baada ya kushindwa akatupwa duniani na kuitwa Mungu wa dunia hii, kwasababu hiyo shetani ameigiza tabia za uungu katika hali ya uharibifu (Negatively), hivyo anamuiga Mungu (Jehova) lakini lengo la shetani ni kuharibu kabisa na kuwachukua watu wa Mungu mateka kama linavyosema Neno la Mungu kutoka katika chuo cha Isaya 42:22 “22 Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha.” Vilevile Neono hili linapatikana katika Isaya 14:16-17 “16 Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme; 17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?” Lakini sasa tunao ushindi kwakuwa Yesu Kristo amepakwa mafuta kwa kazi ya kutukomboa, kutufungua na kutuweka huru kutoka katika umateka wa shetani na mawakala zake kama linenavyo Neno la Mungu kutoka Injili ya Luka 4: 18-19 “18 Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, 19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.”
Sasa basi; Kama tulivyoona ya kuwa Neno la Mungu litatimiza mapenzi ya Mungu ambayo ni ya Amani kwetu sisi vivyo hivyo neno linalotoka kwa shetani na mawakala wake (waganga, wachawi, wasoma nyota, wapiga ramli nk) litatimiza mapenzi ya uovu wa shetani ikiwa ni pamoja na kuwaua watakatifu wake Mungu na kuipinga injili ya Yesu Kristo.

NAMNA SHETANI ANAVYOSHAMBULIA KWA MANENO

Zaburi 57:4Nafsi yangu i kati ya simba, Nitastarehe kati yao waliowaka moto. Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale, Na ndimi zao ni upanga mkali”.
Wanadamu hawa wanaoongelewa katika zaburi hii ni wale mawakala wa mauti yaani wachawi, washirikina, waganga nk. Wanatumia sana ndimi zao (Vinywa vyao kusababisha madhara makubwa kwa watumishi wa Mungu na wanafanya hivyo kwa siri (Faraghani) wakisema hakuna atakayeiona Zaburi 64:3-5 “3 Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu, 4 Wapate kumpiga mkamilifu faraghani, Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi. 5 Walijifanya hodari katika jambo baya; Hushauriana juu ya kutega mitego; Husema, Ni nani atakayeiona?”.
Ninakuombea mtu wa Mungu katika Jina la Yesu kuanzia leo fahamu zako zifunguke na uyaone hata yale manuizo ya kipepo yanayorushwa kwako kwa njia usiyoifahamu kwa jinsi ya kibinadamu. Fuatilia ushuhuda huu kisha utajifunza jambo namna shetani anavyowashambulia watu kwa njia ya maneno (Ndimi) kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Yakobo 3:5-9 “5 Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana. 6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum……………. 8 Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti. 9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.”

USHUHUDA


Tarehe 11/04/2015 jioni muda wa saa kumi nikiwa Kanisani nafanya usafi akaja binti mmoja ili kufanya usafi kwani ilikuwa ni zamu ya jumuiya yetu; kabla hajaanza tuliongea kidogo huku nikimuuliza kwanini hafiki kwenye maombi na pia nilimuuliza ni kwanini alipata mimba akiwa mdogo sana “alipata mimba akiwa na miaka 16”. Yule binti akaniambia “kaka unataka kufahamu maisha yangu?” nikamjibu ndio, akaniambia “twende tukakae nikueleze habari zangu”. Yule binti alinieleza habari za maisha yake takribani muda wa saa mbili na nusu, aliniambia namna alivyoacha shule akiwa darasa la nne kutokana na umasikini, alinieleza kuwa hakuwahi kumfahamu baba yake mzazi mpaka alipofikisha miaka 16, aliniambia namna mama yake mzazi anavyosumbuliwa na nguvu za giza na jinsi alivyo masikini pia alinieleza jinsi alivyotangatanga katika maisha yake ya kufanya kazi za ndani kutoka nyumba moja hadi nyingine na pia aliniambia jinsi watu walioonesha mapenzi kwake ghafla waligeuka na kumchukia sana wakiwepo baadhi ya dada zake, vilevile alinieleza jinsi alivyopata mimba na matatizo makubwa aliyonayo. Baada ya kunieleza yote hayo nilimuuliza kama ameokoka kasema hajaokoka, nikamuuliza kama yuko tayari akasema yuko tayari. Ndani yangu Roho wa BWANA akanielekeza kuomba naye na maeneo ya kumfungua. Tukaendelea na usafi wa maeneo ya kanisa na baada ya usafi tukaingia katika maombi ya Ukombozi, baada ya maombi yule binti akafunguliwa na kutueleza kuwa yeye hakuwepo duniani bali alikuwa mahali penye giza sana na taa za kule ni macho ya nyoka na kunguru na ndio walikuwa walinzi wake, alituambia kuwa magari ya kule ni majeneza na ndani ya hayo magari “majeneza” ndio kuna taa. Alitueleza jinsi alivyokuja mara tatu kumchukua mchungaji wa kanisa la KKKT – Ngudu bila mafanikio na baada ya kushindwa alipewa adhabu ya kutokula kwa muda wa wiki tatu. Tulipomuhoji ya kuwa ni chakula gani wanakula huko alisema ni nyama na damu za watu, alitueleza hata namna ya kuchukuwa nyama na namna wanavyochukua damu za watu, alitueleza namna wanavyofanya kazi katika maeneo mbalimbali ya Tanzania, na mambo mengine mengi sana kuhusu ufalme wa giza (Binti huyu alieleza mambo mengi sana ambayo hapa sijayataja ili kutopoteza lengo la somo hili). Baada ya ukombozi tulimrudisha nyumbani kwao na kuwaeleza mambo yanayowapasa kufanya. Siku moja baadae (Tarehe 13/04/2015) nilipigiwa simu na dada wa huyo binti ambaye ndiye anayekaa naye, alinigombeza sana kwa njia ya simu na kuniambia nikome kabisa kuombea watoto wa watu bila ridhaa ya wazazi wao, nikajitahidi kuongea nae kwa upole na kumueleza kuwa huyo binti anahitajika kuendelea kufanyiwa maombi na kufundishwa ili kuimarishwa zaidi kiroho; Lakini huyo dada mtu akazidi kuwa mkali na kunikemea sana hadi nikanyamaza kimya kisha akakata simu. Baada ya kukata simu ghafla hali yangu ilibadilika na kuwa kama mgonjwa mwenye homa kali hadi nilishindwa kuendelea na kazi za ofisi, nikajitenga chumba tofauti na kutafakari nini kimetokea lakini sikupata jibu hadi baada ya saa moja wazo likanijia nikampigia simu mtumishi mmoja (Mwalimu Samson wa Ukombozi Ministries for All Nations) na baada ya kumueleza akaniambia nimeshambuliwa na silaha nisiyoifahamu ambayo ni maneno ya kichawi na yalikuwa na lengo la kunidhoofisha ili wanimalize kwa silaha nyingine. Nilipofahamu hivyo nikawajulisha wanamaombi wenzangu kwa ujumbe mfupi wa maneno (Message) nami nikaanza kuomba kwa kuchomoa mishale yote ya kipepo niliyorushiwa kwa njia ya maneno, baada ya maombi hayo nikapata nguvu mpya na kuendelea na kazi kama kawaida.

Baada ya haya yote ndipo nikapata maarifa ya kuandika somo hili ili watu wa Mungu wajifunze

NAMNA DAUDI NA GOLIATHI WALIVYOPAMBANA KWA MANENO

1Samweli 17:44-47 44 Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni. 45 Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana. 46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli. 47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu.

Tunaona vita ya Daudi na Goliathi ilianzia katika maneno, Goliathi alianza kumtisha Daudi kwa maneno ya kudhoofisha na kumuonesha kwamba hawezi na atampiga Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni” lakini Daudi alifahamu kuwa vita tayari ilikuwa imeanzia katika maneno kwahiyo akaanza kukiri maneno ya ushindi na kumuonesha Goliathi kwamba atamshinda kwa jina la BWANA ……Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana. Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli……..

Ninataka kukutia moyo mtu wa Mungu kuwa usinyamaze kimya unaposhambuliwa kwa maneno na watesi wako bali wewe ukiri ushindi kama vile Daudi alivyokiri ushindi na kisha kumuua Goliathi

WATU WA MUNGU HUPIGWA KWA MANENO

Watumishi wengi wa Mungu hupigwa kwa maneno na hata kuangushwa katika utumishi na wao (watumishi wa Mungu) huacha kulitumikia kusudi la Mungu na kuanguka kabisa. Nabii Yeremia alifanyiwa mpango wa kupigwa na watesi wake kwa maneno (Yeremia 18:18  Hapo ndipo waliposema, Njoni na tufanye mashauri juu ya Yeremia; maana sheria haitampotea kuhani, wala shauri halitampotea mwenye hekima, wala neno halitampotea nabii. Njoni, na tumpige kwa ndimi zetu, wala tusiyaangalie maneno yake yo yote.). Mawakala wa shetani (wachawi, waganga, nk) hukaa vikao na kutamka maneno yenye nguvu za giza (manuizo ya kipepo), maneno hayo huja kutumika katika hali ya maisha ya kawaida na pale unaponenewa maneno hayo, hali yako ya kiroho huanza kuporomoka ghafla na kupungukiwa nguvu za kiroho kama ilivyonitokea katika ushuhuda huo hapo juu; hali hii hutokana na ukweli kwamba yapo mapepo (roho za kuzimu) ambazo huchukua maneno yote ya uovu yaliyonenwa na kuyasimamia kuhakikisha yanatimia katika uovu uliotamkwa. Kumbuka kila wakati unapokuwa katika kuomba, futa kila maneno ya kipepo uliyonuiziwa kwa kufahamu au pasipo kufahamu.

TUNALO TUMAINI NA USHINDI MKUU

1Yohana 3: 8 “……. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.”
Pamoja na mawakala wa shetani (Wachawi, waganga, wapiga ramli, nk) kutumia maneno kama mishale ya kuwapiga wenye haki wa Mungu kama tunavyosoma katika Zaburi 64:3-6 “3 Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu, 4 Wapate kumpiga mkamilifu faraghani, Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi. 5 Walijifanya hodari katika jambo baya; Hushauriana juu ya kutega mitego; Husema, Ni nani atakayeiona? 6 Hutunga maovu; husema, Tumefanya shauri kamili; Na mawazo ya ndani ya kila mmoja wao, Na moyo wake, huwa siri kabisa”; Uhakika ni kwamba tunalo tumaini ya kuwa BWANA atatupigania na kuwakwaza watesi wetu na kuwapiga kwa maneno yao wenyewe; yaani yale maneno (Manuizo ya kipepo) yanayotoka katika vinywa vyao yatawapata wenyewe na kuwapiga wao; ikiwa utafahamu haya mtu wa Mungu unayo nguvu na ujasiri wa kupambana na kila nguvu za giza na mishale yote ya yule adui Zaburi 64:7-10 (7 Kwa hiyo Mungu atawapiga shabaha, Kwa mshale mara watapigwa. 8 Ndivyo watakavyokwazwa, Ulimi wao wenyewe ukishindana nao. Wote wawaonao watatikisa kichwa. 9 Na watu wote wataogopa, Wataitangaza kazi ya Mungu, Na kuyafahamu matendo yake. 10 Mwenye haki atamfurahia Bwana na kumkimbilia, Na wote wenye moyo wa adili watajisifu.)

MAOMBI YA KUFUTA MANENO YA KIPEPO/KICHAWI

1.     Omba Rehema
ü  Tumia Zaburi ya 51:1 – 19
2.     Jifunike kwa Damu ya Yesu, Vaa Silaha na Omba Nguvu za Mungu
ü  Katika Jina la Yesu najifunika kwa Damu ya Yesu kuanzia utosini mpaka unyayoni, naifunika familia yangu yote, kazi, biashara, mashamba na huduma yangu (Taja na vingine); Sawasawa na Neno lako kutoka Waefeso 6:14 – 18 nina vaa silaha zote za Mungu (14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani, 15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani; 16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu. 17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu; 18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;). Ninaipokea ile nguvu kwakuwa Roho Mtakatifu yu ndani yangu sasa (Matendo1:8 8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.)
3.       Msihi Mungu akutie nguvu na upako wa kumshinda adui.
ü  Zaburi 89:20-24 Nimemwona ………..(taja jina lako), mtumishi wangu, Nimempaka mafuta yangu matakatifu. 21 Ambaye mkono wangu utakuwa thabiti kwake, Na mkono wangu utamtia nguvu.  22 Adui hatamwonea, Wala mwana wa uovu hatamtesa.  23 Bali nitawaponda watesi wake mbele yake, Nitawapiga wanaomchukia. 24 Uaminifu wangu na fadhili zangu atakuwa nazo, Na kwa jina langu pembe yake itatukuka.
4.     Anza maombi ya VITA
ü  Katika Jina lenye uweza Mkuu, Jina la Yesu; Ninabatilisha kila maneno yaliyonenwa kwa faragha kwaajili yangu katika ulimwengu wa giza
ü  Kwa Damu ya Yesu; Ninayafuta maneno yote yaliyonakiliwa au kuandikwa na makatibu wa wachawi katika ulimwengu wa giza
ü  Katika Jina la Yesu; Ninaichomoa mishale yote ya ibilisi na mawakala wake katika Ndoa, Kazi, Biashara, Mashamba, Uchumi, Afya, Mahusiano (Endelea kutaja na maeneo mengine)
ü  Mahali popote nilipochomwa mshale wa kipepo kwa njia ya maneno najiosha kwa Damu ya Yesu inenayo mema (Waebrania 12:24 na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.)
5.     Omba ulinzi kwa kujifunika kwa Damu ya Yesu na Moto wa Roho Mtakatifu
6.     Mshukuru Mungu kwa matendo yake makuu kwako.

7.      Mwimbie Mungu wimbo wa ushindi (Zaburi 144)

No comments: