Monday, March 21, 2016

SEMINA YA NENO LA MUNGU NA MWL. CHRISTOPHER MWAKASEGE (Viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es salaam) SOMO: UPONYAJI KWA WALIOVUNJIKA MOYO NA WALIO NA HAJA YA KUPONA.

SIKU YA SABA

Maneno ya msingi: Isaya 61:1 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.Luka 9:11 “Na makutano walipojua walimfuata; akawakaribisha, akawa akisema nao habari za ufalme wa Mungu, akawaponya wale wenye haja ya kuponywa.” Yeremia 6:14 “Wameiponya jeraha ya watu wangu kwa juu juu tu, wakisema, Amani, Amani, wala hapana amani.”

SOMO LA LEO: UPONYAJI WA JERAHA LA MOYO WA MTU BINAFSI UNAVYOTENGENEZA MAZINGIRA YA UPONYAJI WA JERAHA LA MOYO WA TAIFA.

Tuliangalie hili kwa mtiririko ufuatao.

1.     Kilichojeruhi moyo wa mtu mmoja kinaweza kusababisha jeraha kwenye mioyo ya watu wengi.

Tutaangalie kwa mifano ktk maeneo mawili

        i.            Uchungu
Efeso 4:26 “Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;”
Waebrania 12:14-15 “14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; 15 mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.”
Fahamu kuwa shina la uchungu linapochipuka linanajisi wengine wanaohusiana na huyo mtu. Maana linaambukiza kwa wengine.

     ii.            Dhambi
1 Yoh 3:4 “Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi.”
Rum 5:12 “Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi;”
Dhambi ni uasi.
·         Na penye dhambi/uasi pana mauti
·         Uasi unaweza kuanza kwa mtu kisha kuendelea kusambaa hadi kwenye taifa.

1.     Kiini cha uhai wa kitaifa kinapojeruhiwa ina maana moyo wa kitaifa umejeruhiwa.
Yeremia 30:4,12-14 “4 Na haya ndiyo maneno aliyosema Bwana, katika habari za Israeli, na katika habari za Yuda. 12 Maana Bwana asema hivi, Maumivu yako hayaponyekani, na jeraha yako ni kubwa. 13 Hapana mtu wa kukutetea; kwa jeraha yako huna dawa ziponyazo. 14 Wote wakupendao wamekusahau; hawakutafuti; maana nimekujeruhi kwa jeraha ya adui, kwa adhabu ya mtu mkatili; kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zilikuwa zimeongezeka.”
Taifa la Israel lilijeruhiwa na kugawanyika, hii inaonesha kuwa taifa linaweza kujeruhiwa.
2.     Kufuatana na Biblia kiini cha taifa lolote ni cha kiroho
Mungu ndiye aliyefanya taifa. Kuna mambo kadhaa yanayofanya taifa kuwepo/ kuunda taifa; nayo ni:
a.      Lango/ Mwanzilishi ambaye ni mtu mmoja.
Matendo 17:26 “Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao;”

b.     Majira/Nyakati
Matendo 17:26 “Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao;”

c.      Mipaka
Matendo 17:26 “Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao;”

d.     kabila
Kufuatana na biblia kila kabila lina baraka zake.
Mwanzo 49:1, 2, 28 “1 Yakobo akawaita wanawe, akasema, Kusanyikeni, ili niwaambie yatakayowapata siku za mwisho. 2 Kusanyikeni, msikie, enyi wana wa Yakobo, Msikilizeni Israeli, baba yenu. 28 Hizo zote ndizo kabila za Israeli kumi na mbili. Na hayo ndiyo aliyowaambia baba yao, na kuwabariki; mmoja mmoja kwa mbaraka wake aliwabariki.”
Kumb 4:34 “Au Mungu amekwenda wakati gani akajitwalia taifa toka kati ya taifa lingine, kwa majaribu, na kwa ishara, na kwa maajabu, na kwa vita, na kwa mkono hodari, na kwa mkono ulionyoshwa, na kwa maogofya makuu, kama vile Bwana, Mungu wenu, alivyowatendea ninyi katika Misri, mbele ya macho yenu?”

e.      Hali ya kiroho ya kitaifa
Zaburi 33:12 “Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, Watu aliowachagua kuwa urithi wake.”

f.        Familia
Ufunuo 5:9-10 “9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, 10 ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.”
Kabla halijawa taifa kwanza, inaanza familia

g.      Lugha
Ufunuo 5:9-10 “9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, 10 ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.”

3.     Mifumo ya majeraha inaweza kuumiza moyo wa mtu na moyo wa taifa kwa pamoja
Mfano:
·         Moyo unapojeruhiwa na kushindwa kuelewa lugha ya walio karibu nawe
Mwanzo 11:1, 6-9 “1 Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja. 6 Bwana akasema, Tazama, watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja; na haya ndiyo wanayoanza kuyafanya, wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya. 7 Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao. 8 Basi Bwana akawatawanya kutoka huko waende usoni pa nchi yote; wakaacha kuujenga ule mji. 9 Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli; maana hapo ndipo Bwana alipoichafua lugha ya dunia yote; na kutoka huko Bwana akawatawanya waende usoni pa nchi yote.”

Ufunuo 13:2 “Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha simba, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi.”
Fahamu:
·         Lugha moja inaleta usemi mmoja.
·         Lugha inaleta kusikilizana.
·         Lugha inaleta umoja.
·         Lugha inaleta kushirikiana na kufanya kazi kwa kufanikiwa.
·         Kwa hiyo lugha ikiharibika ni hatari sana katika taifa.

Ø  Mioyo ya watu ikijeruhiwa, watu wanakuwa na lugha tofauti katika taifa.
Ø  Haki inapoondolewa katika taifa, hupelekea watu kujeruhiwa kunakopelekea watu kutofautiana katika lugha

Mithali 14:34 “Haki huinua taifa; Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.”
Ø  Kiu ya udini kwenye uongozi pia inaweza kujeruhi mioyo ya watu katika taifa
Ø  Kutokuelewana juu ya mfumo wa kupata viongozi
Ø  Hii pia inaweza kujeruhiwa mioyo ya watu kisha kuharibu moyo wa taifa



No comments: