Tuesday, August 30, 2016

HISTORIA YA MAISHA YAKO INABADILIKA LEO Isaac Ridhiwan Omary


Imefundishwa na Mtumishi Isaac Ridhiwan Omary (Semina ya MVUMO – Morogoro, 28th August 2016)
Imeandikwa na Samson Mollel – 0767 664 338 (www.uzimawamileleministries.blogspot.com)

*Yohana 9:1-9* _“1 Hata alipokuwa akipita alimwona mtu, kipofu tangu kuzaliwa. 2 Wanafunzi wake wakamwuliza wakisema, Rabi, ni yupi aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hata azaliwe kipofu? 3 Yesu akajibu, Huyu hakutenda dhambi, wala wazazi wake; bali kazi za Mungu zidhihirishwe ndani yake. 4 Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana, usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi. 5 Muda nilipo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu. 6 Alipokwisha kusema hayo, alitema mate chini, akafanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho, 7 akamwambia, Nenda kanawe katika birika ya Siloamu, (maana yake, Aliyetumwa). Basi akaenda na kunawa; akarudi anaona. 8 Basi jirani zake, na wale waliomwona zamani kuwa ni mwombaji, wakasema, Je! Huyu siye yule aliyekuwa akiketi na kuomba? 9 Wengine wakasema, Ndiye. Wengine wakasema, La, lakini amefanana naye. Yeye mwenyewe alisema, Mimi ndiye.”_

Unapokutana na Yesu Kristo, kubadilisha historia ya maisha yako sio jambo linalohitaji miaka mingi, ni dakika moja tu na historia ya maisha yako inabadilika kabisa.

Ilimchukua dakika moja tu mwizi pale msalabani kubadilisha historia nzima ya maisha yake. Yesu hakumuuliza umebatizwa wapi au umezaliwa na nani, ukikutana na Yesu dakika ileile maisha yako yanabadilika.

*Luka 23: 39-42* _“39 Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi. 40 Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo? 41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa. 42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako. 43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.”_

Fahamu yakwamba dunia hii inatafsiri mambo isivyofaa. Yaani ukipita katika changamoto/matatizo yoyote basi unaonekana wewe umetenda dhambi; inawezekana haujaolewa, haujapata mtoto, watoto wako wanaumwa, haujapata kazi, n.k. Basi hapo watu husema kuwa wewe au wazazi wako wametenda dhambi.

*Yohana 9:1-2* _“1 Hata alipokuwa akipita alimwona mtu, kipofu tangu kuzaliwa. 2 Wanafunzi wake wakamwuliza wakisema, Rabi, ni yupi aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hata azaliwe kipofu?_

Kuna mahali unapitia sasa katika maisha yako na watu wansema maneno mengi na hayo wanyoyasema yankufikia na kukuumiza. Umejitahidi kufanya toba za kila namna kwa habari ya maovu na makosa na dhambi za kwako na za familia yako lakini bado uko kwenye hali ile ile.

Nakuambia leo kama umeshatubu usiitafute hiyo dhambi kwako na hizo hatia ulizojibebesha uzifute kwa damu ya Yesu kwakuwa mambo hayo yameachiliwa na Mungu ili kazi za Mungu zidhihirishwe.

*Yohana 9:3* _“3 Yesu akajibu, Huyu hakutenda dhambi, wala wazazi wake; bali kazi za Mungu zidhihirishwe ndani yake.”_

Yesu unayekutana naye leo anaenda kubadilisha kabisa maisha yako, jambo la msingi ni kuheshimu anakuambia ufanye nini. Heshimu mambo ya Mungu hata kama unayaona ni ya kipumbavu *1Wakorintho 1:25* _“Kwa sababu upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.”_

Yesu alitema mate chini na kumpaka matope yule kipofu kama tunavyosoma katika *Yohana 9:6-7* _“6 Alipokwisha kusema hayo, alitema mate chini, akafanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho, 7 akamwambia, Nenda kanawe katika birika ya Siloamu, (maana yake, Aliyetumwa). Basi akaenda na kunawa; akarudi anaona._

Alipofika katika birika la Siloamu na kunawa, hakuona mara moja ila wakati akirudi kutoka Siloam kwenda kwa Yesu ndipo alipopata kuona

Inawezekana katika hali uliyopo sasa ndio unanawa, yaani upo Siloam unanawa na bado macho yako hayajafunguka, usikate tama endelea kunawa. Ondoa magonjwa, umasikini, kila aina ya udhaifu wewe endelea kunawa kwani umekutana na Yesu leo na nilazima maisha yako yatabadilika kabisa.


No comments: