Friday, September 2, 2016

TOA SADAKA YAKO KWAAJILI YA SEMINA YA NENO LA MUNGU NGUDU - KWIMBA, MWANZA (Tarehe 30/09/2016 hadi 02/10/2016)

Shalom!!!

Semina ya Neno la MUNGU, kwa muda wa siku tatu, kuanzia tarehe 30/09/2016 hadi 02/10/2016

Huduma ya Uzima wa Milele International Ministries (UMIM) kwa kushirikiana na huduma ya MANA mkoa wa Mwanza imeandaa semina ya Neno la MUNGU, kwa muda wa siku tatu, kuanzia tarehe 30/09/2016 hadi 02/10/2016 katika mji wa NGUDU wilaya ya Kwimba. Semina itakuwa ni semina ya tatu kufanyika katika mji huu wa Ngudu, semina zingine zilifanyika Februari na Mei mwaka huu (2016). Semina hizi zimekuwa za mafanikio makubwa sana kiroho na hata kimwili.

Tunamshukuru Mungu kwaajili ya watu wa MANA Mwanza kwa jinsi wanavyojitoa kwa muda wao na mali zao katika kuhakikisha semina hizi zinafanikiwa kila zinapopangwa, Mungu wa mbinguni azidi sana kuwabariki na kuwainua katika huduma aliyoiweka ndani yenu

Makadirio ya bajeti kwaajili ya semina hii ni shilingi milioni 3.Tunaomba sadaka yako ili tufanikishe semina hii. Pia ungana nasi kufunga na kuomba siku za Jumanne na Ijumaa ili kuombea semina hii ili kusudi la Mungu litimie.

Unaweza kutuma sadaka yako kwa njia ya:-

M-pesa namba 0752 606 041 Lucy Lusoloja (Mratibu UMIM - Kwimba, Mwanza) au 

0759 565 600 - Levina Deogratius, 

Tigo pesa 0713 664 338 Samson Mollel


Mungu akubariki kwa sadaka yako.

No comments: