Saturday, August 27, 2016

TAIFA TAKATIFU

JITAMBUE YAKUWA WEWE NI TAIFA TAKATIFU KWA MUNGU ALIYE HAI/MPATE YESU ILI UWE TAIFA TAKATIFU KWA MUNGU ALIYE HAI
Imefundishwa na Mtumishi Isaac Ridhiwan Omary (Semina ya MVUMO – Morogoro, 26th August 2016)
Imeandikwa na Samson Mollel – 0767 664 338 (www.uzimawamileleministries.blogspot.com)

Kumbukumbu la torati 26:16-19 “16 Leo hivi akuamuru Bwana, Mungu wako, kuzifanya amri hizi na hukumu; basi uzishike na kuzifanya kwa moyo wako wote na roho yako yote. 17 Umemwungama Bwana leo, kuwa ndiye Mungu wako, na kuwa yakupasa kutembea katika njia zake, na kushika amri zake na maagizo yake, na hukumu zake, na kusikiza sauti yake; 18 naye Bwana amekuungama hivi leo kuwa taifa iliyotengwa iwe yake yeye, kama alivyokuahidi, na kuwa yakupasa kushika maagizo yake yote; 19 na kuwa atakutukuza juu ya mataifa yote aliyoyafanya, kwa sifa, na jina, na heshima, nawe upate kuwa taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako, kama alivyosema.”

Kumbukumbu la torati 7:6 “Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako; Bwana Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi.”

Somo la leo lina vichwa viwili kama ifuatavyo
         i.            Kama umeokoka – “JITAMBUE YAKUWA WEWE NI TAIFA TAKATIFU KWA MUNGU ALIYE HAI”
       ii.            Kama haujaokoka -  “MPATE YESU ILI UWE TAIFA TAKATIFU KWA MUNGU ALIYE HAI”

Ukizungumza kuwa wewe ni Taifa kwa Mungu bila ya kujua thamani ya utaifa hauwezi kuelewa vizuri.

Kama leo ungepewa na Mungu nafasi ya kuchagua uzaliwe bara/nchi ipi, na ukaangalia duniani kila nchi ilivyo ndipo uchague, kila mtu anayosababu ya msingi angechagua nchi gani (Wengi katika mkutano wamechagua nchi za ulaya na Marekani)

Nchi za wenzetu (ulaya na Marekani) wanayotabia ya kuwajali sana watu wa taifa lao mahali popote walipo. Kwamfano pakitokea vurugu yoyote ambayo hata haijafikia kuwa ni vita katika nchi yoyte ambayo raia wa Marekani wapo, mara moja utasikia Marekani inawarudisha raia wake; hivyo watawatumia ndege na wanajeshi wa kuwarejesha kutoka mahali popote duniani walipo ili wasije wakadhurika na machafuko.

Sasa kama nchi za wanadamu wanaweza kufanya hivyo; si zaidi sana ukiwa taifa la Mungu?

Wewe haijalishi katika mwili umezaliwa wapi, kuzaliwa Tanzania ni kusudi la Mungu. Mungu anakufanya wewe kuwa Taifa lake.

Unapotaka kwenda kwenye taifa Fulani (mfano marekani), hauwezi kujiamulia tu kwenda bila kufuata taratibu za kuingia katika taifa hilo. Hii ni kwasababu nchi ya Marekani inayo mipaka yake na sheria zake na utaratibu wa namna ya kupokea wageni.

Hivyo basi unapotaka kwenda marekani lazima uwe na kusudio linalofahamika na kukubalika na taifa la marekani ili uruhusiwe kuingia katika nchi yao.

Kuwa taifa la Mungu ni zaidi ya kuwa mtumishi wa Mungu. Kuwa taifa maana yake unakuwa na watu wako, unakuwa na mipaka yako, unakuwa na utaratibu na kanuni na sheria za kufuata. Na kwasababu hiyo huwezi kuruhusu kila mtu kuingia katika taifa lako bila ya kufuata taratibu na sheria za taifa lako.

Unapokuwa taifa la Mungu unakuwa umekubali kufuata sheria na taratibu za taifa la Mungu kama ilivyoandikwa kuwa umemkubali BWANA na sheria zake nayeye amekukubali ili uzifuate hizo sheria/maagizo yake:

Kumbukumbu la torati 26:17-18 “17 Umemwungama [UMEMKUBALI] Bwana leo, kuwa ndiye Mungu wako, na kuwa yakupasa kutembea katika njia zake, na kushika amri zake na maagizo yake, na hukumu zake, na kusikiza sauti yake; 18 naye Bwana amekuungama [AMEKUKUBALI ]hivi leo kuwa taifa iliyotengwa iwe yake yeye, kama alivyokuahidi, na kuwa yakupasa kushika maagizo yake yote;”

Na kwasababu hiyo; kwakuwa umekubali kufuata sheria na taratibu za Taifa la Mungu naye Mungu amekukubali wewe, basi umekuwa Taifa la Mungu na unaishi kwa kufuata sheria za Taifa la Mungu.

Kumbukumbu la torati 7:6 “Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako; Bwana Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi.”

Ukiwa taifa mbele za BWANA wewe ni mmoja katika ya wengi “Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa Bwana” na wengi katika mmoja “amekuchagua kuwa watu wake hasa


TANGU UMERUHUSU WATU KUINGIA KATIKA MIPAKA YAKO UMEKWAMA
Basi sasa kwakuwa umefahamu kuwa wewe ni Taifa kwa Mungu, huwezi kuruhu kila mtu akaingia katika mipaka yako.

Tangu umekaribisha watu fulani katika maisha yako mambo yako yamekwama, tangu umeruhusu watu Fulani washauri kwenye ndoa yako ndoa imekwama, tangu uwaruhusu watu fulani kwenye biashara, kazi, masomo, huduma vyote vimekwama.

Wewe haukujua kwamba ni Taifa, na haupaswi kumruhusu mtu yoyote kuingia kwenye taifa lako bila kufuata sheria ya ufalme wa Mungu hata kama mtu huyo ameokoka. Pale ulipowaruhusu watu waingie wameingia na miungu yao na umepata matatizo katika Taifa lako.

Kuna watu umewakaribisha katika huduma yako kwasababu wameokoka kumbe wao sio wa Taifa lako.

Kuna watu umewashirikisha kwenye biashara, kazi, masomo, uchumi na mambo mengi ya maisha yako kumbe sio wa Taifa lako na mambo yako yameharibika, wewe ulidhani ni ndugu zako au watu wa karibu yako lakini wamekusababishia matatizo makubwa (Mathayo 10:36 “na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.”)

Fahamu yakuwa watu wote wanaoingia ndani ya mipaka yako wanayo nafasi kubwa ya kuathiri maamuzi yako.

Ukishakuwa Taifa la Mungu mbingu ndio zinatawala, serikali ya Mungu ndio inatawala ndani ya utaifa wa ki-Mungu

Hao watu walioingia ndani ya mipaka usigomabne nao wewe kwakuwa kuna mkono wa BWANA utawachomoa na kuwatoa nje ya mipaka yako kwa jina la YESU, mkono wa BWANA unawatoa sasa nje ya ndoa yako, nje ya kazi yako, nje ya huduma yako, nje ya ukoo na familia yako, nje ya miradi yako, nje ya kila mpaka waliongia wanatolewa sasa kwa mkono wa BWANA kwa jina la YESU.

KWA MASOMO MENGINE BOFYA HAPA: www.uzimawamileleministries.blogspot.com

No comments: