Thursday, August 25, 2016

WASIO HAKI NA WAOVU WAKISTAWI

WASIO HAKI NA WAOVU WAKISTAWI
Samson Mollel 0767 – 664 338

WASIOHAKI NA WAOVU NI NANI?

Wasio haki na waovu ni watu wasiotenda mapenzi na makusudi ya Mungu, ni wale watu wanaotenda kinyume na maagizo ya BWANA. Ipo mifano mingi sana ya wasio haki, ifuatayo ni baadhi ya mifano ya wasio haki na waovu:-

Ø  Wasio haki na waovu ni wale wasio kwenda katika sahuri la BWANA

Zaburi 1:1-4 “1 Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha. 2 Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. 3 Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa. 4 Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.

Ø  Wasio haki na waovu ni wale wanaoshindana na wateule wa Mungu

Zaburi 11:2 “Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, Wanaitia mishale yao katika upote, Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.”

Ø  Wasio haki na waovu ni wauaji

Zaburi 37: 14 “ Wasio haki wamefuta upanga na kupinda uta, Wamwangushe chini maskini na mhitaji, Na kuwaua wenye mwenendo wa unyofu.”

Ø  Wasio haki na waovu ni wale wenye hila na wategao mitego

Yeremia 5:25-26 “25 Maovu yenu yameyageuza haya, na dhambi zenu zimewazuilia mema msiyapate. 26 Maana katika watu wangu wameonekana watu waovu; huotea kama vile watu wategao mitego; hutega mtego, na kunasa watu. 27 Kama tundu lijaavyo ndege, kadhalika nyumba zao zimejaa hila; kwa hiyo wamekuwa wakuu, wamepata mali. 28 Wamewanda sana, wang'aa; naam, wamepita kiasi kwa matendo maovu; hawatetei madai ya yatima, ili wapate kufanikiwa; wala hawaamui haki ya mhitaji.”


MALALAMIKO YA WATAKATIFU KWA MUNGU
Watakatifu wengi, yaani wale walioitwa kwa jina la Yesu na wamempokea Yesu wamekuwa na malalako/kilio kwa Mungu. Sababu ya kilio/malalamiko haya ni kumhoji Mungu kwamba kwanini wasio haki na waovu wanafanikiwa lakini watakatifu hawafanikiwi, na pia kwanini wanapata mali kwa njia isiyo halali na kuwaonea watoto wa Mungu?

Zaburi 94:3-5 “3 Bwana, hata lini wasio haki, Hata lini wasio haki watashangilia? 4 Je! Wote watendao uovu watatoa maneno, Na kusema majivuno, na kufanya kiburi? 5 Ee Bwana, wanawaseta watu wako; Wanautesa urithi wako;”

Watakatifu wanamlilia Mungu na kumweleza kuwa wasio haki na waovu wamewadharau hadi wanasema Mungu hasikii; Zaburi 94:7 “Nao husema, Bwana haoni; Mungu wa Yakobo hafikiri.”

Lakini Mungu anajibu na kusema na wasio haki na waovu na kuwaonya kuwa yeye anajua na kufahamu kila kitu kwakuwa ndiye muumbaji, Zaburi 94:8-11 “8 Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini; Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili? 9 Aliyelitia sikio mahali pake asisikie? Aliyelifanya jicho asione? 10 Awaadibuye mataifa asikemee? Amfundishaye mwanadamu asijue? 11 Bwana anajua mawazo ya mwanadamu, Ya kuwa ni ubatili.”

Zaidi sana BWANA anasema kuwa hakuna sababu ya kushangaa kwanini waovu na wasio haki wanafanikiwa kwanini huo ni mpango wake kwa kusudi lake; Zaburi 92:7 “Wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakistawi. Ni kwa kusudi waangamizwe milele;”


MUNGU HUSHUGHULIKA NA WASIO HAKI

Kama tunavyosoma katika Zaburi 92:7 “Wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakistawi. Ni kwa kusudi waangamizwe milele;”

Mungu mwenyewe anawashughulikia wasio haki na waovu ambao wamekuwa wakiwatesa watakatifu wa Mungu.

Zaburi 3:7 “Bwana, uinuke, Mungu wangu, uniokoe, Maana umewapiga taya adui zangu wote; Umewavunja meno wasio haki.”

Zaburi 17:8-9 “8 Unilinde kama mboni ya jicho, Unifiche chini ya uvuli wa mbawa zako; 9 Wasinione wasio haki wanaonionea, Adui za roho yangu wanaonizunguka.”

Zaburi 37:10, 13 “10 Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo, Utapaangalia mahali pake wala hatakuwapo.13 Bwana atamcheka, Maana ameona kwamba siku yake inakuja.”

Zaburi 75:10 “Pembe zote za wasio haki nitazikata, Na pembe za mwenye haki zitainuka.”

Mithali 13:22 “22 Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi; Na mali ya mkosaji huwa akiba kwa mwenye haki.”


MAOMBI YA KUWAPIGA WASIO HAKI

Zekaria 2:8-9 “8 Kwa maana Bwana wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake. 9 Kwa maana, tazama, nitatikisa mkono wangu juu yao, nao watakuwa mateka ya hao waliowatumikia; nanyi mtajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma.”

Hesabu 23:22 “Lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao.”

1Samwel 2:10 “Washindanao na Bwana watapondwa kabisa; Toka mbinguni yeye atawapigia radi; Bwana ataihukumu miisho ya dunia; Naye atampa mfalme wake nguvu, Na kuitukuza pembe ya masihi wake.”


WASIO HAKI NA WAOVU WAKISTAWI
Samson Mollel 0767 – 664 338


No comments: