Thursday, August 25, 2016

ZIFUTE NA KUZIKATAA KALENDA ZA KIPEPO ZISIFUATILIE MAISHA YAKO WALA UZAO WAKO

Imefundishwa na Mtumishi Isaac Ridhiwan Omary (Semina ya MVUMO – Morogoro, 24th August 2016)

Imeandikwa na Samson Mollel – 0767 664 338 (www.uzimawamileleministries.blogspot.com)

Mwanzo 24:63-67 “63 Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni; akainua macho yake, akaona, kuna ngamia wanakuja. 64 Rebeka akainua macho, naye alipomwona Isaka, alishuka juu ya ngamia. 65 Akamwambia mtumishi, Ni nani mtu huyu ajaye kondeni kutulaki? Mtumishi akasema, Huyu ndiye bwana wangu. Basi akatwaa shela yake akajifunika. 66 Yule mtumishi akamwambia Isaka mambo yote aliyoyatenda. 67 Isaka akamwingiza Rebeka katika hema ya mama yake, Sara, akamtwaa Rebeka, akawa mkewe, akampenda; Isaka akafarijika kwa ajili ya kufa kwa mamake.”

Mwanzo 25:21 “Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba.”

Matendo 12:1-4 “1 Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa. 2 Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga. 3 Na akiona ya kuwa imewapendeza Wayahudi akaendelea akamshika na Petro. Siku hizo zilikuwa siku za mikate isiyochachwa. 4 Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu.”

Unapoongelea habari ya uzao ni kila aina ya mbaraka ambazo Mungu ameruhusu zizaliwe ndani yako iwe katika Afya, ndoa, Elimu, Biashara……

Shetani ndiye adui yetu mkubwa (Mratibu wa  kila aina ya uovu), ndiye chanzo cha kila aina ya uharibifu.

Anapofanya uharibifu shetani, kila tarehe anayofanya huo uharibifu anaweka kumbukumbu (anarekodi). Kumbukukumbu hiyo ya uharibifu au ya jambo baya kutoka kuzimu hujirudia kila mwaka wakati na majira yaleyale kama ilivyorekodiwa katika kalenda za kipepo.

Tunachokitafuta hapa leo ni hiyo nguvu inayopelekea hilo tatizo kujirudia
Kwamfano Ibrahimu alimdanganya mfalme wa Gerari (Abimeleki) kuwa Sara ni dada yake na Mungu akamuonya Yule mfalme kwa habari ya dhambi ambayo alikaribia kuifanya. Mazingira kama yale yale (Majira yale yale) Isaka naye akamdanganya Abimeleki (Mfalme wa wafilisti huko Gerari) Kuwa Rebeka ni dada yake.

Mwanzo 24: 67 “Isaka akamwingiza Rebeka katika hema ya mama yake, Sara, akamtwaa Rebeka, akawa mkewe, akampenda; Isaka akafarijika kwa ajili ya kufa kwa mamake.”

Isaka hata kabla ya kumtwaa Rebeka kama mke wake (Kabla ya kulala naye) alimuingiza kwenye hema ya mama yake Sara ambaye alikuwa ni tasa kwa muda mrefu, baada ya kumuingiza katika hema ya mama yake ndipo akamtwaa (akalala naye) katika hema ya mama yake. Hapo Rebeka akachukua ile roho ya utasa iliyomsumbua Sara mama yake Isaka

Swali lililopo hapa, Ni nguvu gani iliyompeleka Isaka akalala na Rebeka kwenye hema ya mama yake Sara, na nguvu hii inatumwa na nani?

Shetani anayotabia ya kufuatilia panapo majira yaleyale, Yesu aliuawa majira yaleyale, akafuata Stephano, akafuata Yakobo hala akakamatwa na Petro majira yaleyale.

Ni kwanini Stephano hakuokolewa, ni kwanini Yakobo hakuokolewa na ni kwanini Petro aliokoka na kifo kutoka kwa Herode? Ni kwasababu kanisa lilimlilia Mungu na kuomba kwaajili ya Petro.

Matendo 12:5, 7 “5 Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake. 7 Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwanguka mikononi.”

Kumbe kabla ya hapo kanisa lilikuwa limepigwa usingizi wa kipepo hata lisikumbuke kuomba kwaajili ya Stephano na Yakobo. Lakini kanisa lilipoamka likafuta kalenda ya kipepo/kishetani ya kurudia matukio ya uharibifu majira yale yale

Isaka naye baada ya muda mrefu alimlilia BWANA na Mungu akamsikia na kufuta kalenda za kishetani juu ya maisha yake

Mwanzo 25:21 “Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba.”

Kumbe ukinyamaza wewe na mbingu zinanyamaza na ukitaa kalenda za kipepo na mbingu zinakataa, ukifunga wewe na mbingu zinafunga, ukifungua na mbingua zinafungua. Hivyo ukikaa kimya ukanyamaza na Mungu naye ananyamaza.

Wapo watu wamewekewa nembo mbalimbali katika maisha yao na uzao wao na wamenyamaza, na kila yakifika majira yaleyale mambo mabaya huwapata kulingana na kalenda ya uharibifu ya kuzimu ilirekodi jambo gani, inawezekana ni kutokuolewa, kutokujenga nyumba, kuzaa nyumbani, utasa, ajali, kansa n.k.



MAOMBI YA KUFUTA NA KUKATAA KALENDA ZA KIPEPO

No comments: